Pre GE2025 Maimuna Pathan akabidhi milioni 2 kusaidia ujenzi wa nyumba ya mtumishi UWT na Mitungi ya Gesi 68 kwa Wakazi wa Liwale

Pre GE2025 Maimuna Pathan akabidhi milioni 2 kusaidia ujenzi wa nyumba ya mtumishi UWT na Mitungi ya Gesi 68 kwa Wakazi wa Liwale

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

upupu255

Senior Member
Joined
Sep 4, 2024
Posts
119
Reaction score
144
Maimuna Pathan, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Lindi, mapema jana Februari 27, 2025, amekabidhi kiasi cha shilingi milioni 2 kwa ajili ya Ujenzi wa Nyumba ya Mtumishi wa UWT Wilaya ya Liwale katika jitihada za kuhakikisha Watumishi wanaishi katika makazi bora.

Snapinsta.app_482368803_18060559796051990_7732949077894595348_n_1080.jpg
Vilevile Mheshimiwa Pathan (Mb) akiwa sambamba na Mheshimiwa Tecla Ungele (Mb) wamekabidhi Majiko ya Gesi 68 kwa Wakazi wa Liwale ikiwa Sehemu ya Kuunga Mkono Jitihada Za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Katika kuhakikisha Watanzania wanatumia Nishati safi yakupikia na Kuondokana na Matumizi ya Mkaa ama Kuni ambapo kwa kiasi kikubwa yanaharibu Uoto wa Asili au uharibifu mkubwa wa maliasili ambapo zoeli hilo la makabidhiano limefanyika kwenye Baraza la UWT Liwale.

Snapinsta.app_482052263_18060559859051990_1312437203480611257_n_1080.jpg
Ameshukuru kwa dhamana waliyompa na UWT Wilaya ya Liwale wanaendelea kumuunga mkono kwa kazi nzuri anazozifanya na kujitolea kwake kwa maslahi mapana ya Wanaliwale.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Mheshimiwa Maimuna Pathan anajivunia ushirikiano wa karibu na Mbunge mwenzake wa Viti Maalum Mkoa wa Lindi, MheshimiwaTecla Ungele, ambaye pia walishirikiana pamoja katika zoezi la kugawa mitungi ya gesi 68 kwa UWT Wilaya ya Liwale ili kuwezesha matumizi ya nishati safi.

Snapinsta.app_481987295_18060559805051990_6383802734499220420_n_1080.jpg
Kwa upande wake, Bi. Anna Ndumbalo, Katibu wa UWT Wilaya ya Liwale, ametoa shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Maimuna Pathan mchango wake wa Milioni 2 kuwa utasaidia kumaliza ujenzi wa nyumba ya katibu na kusema kuwa bado wanahitaji nguvu za ziada kutoka kwa viongozi na wanaccm kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati.
 
Back
Top Bottom