Maisha lazima yaendelee: Maduka jirani na jengo lililoporomoka yafunguliwa Kariakoo

Maisha lazima yaendelee: Maduka jirani na jengo lililoporomoka yafunguliwa Kariakoo

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Maisha lazima yaendelee. Ni kauli za wafanyabiashara kwenye maghorofa mawili yaliyo pembeni ya lile lililoporomoka katika soko la Kariakoo ambao sasa wanaendelea na shughuli zao za kibiashara.

Majengo hayo mawili yalitakiwa kuchunguzwa usalama wake, mara baada ya ajali ya kuporomoka kwa jengo jirani na kusababisha vifo vya watu 29, majeruhi 88 na hasara ya mali.

Jengo la upande wa kulia katika harakati za uokoaji ndilo lilitobolewa matundu chini, yaliyotumiwa na waokoaji.

Soma Pia:
Lile lililopo upande wa kushoto nalo lilichimbwa pembezoni na kusababisha msingi wake kuwa wazi, jambo ambalo lilizua hufu kuwa huenda nayo si salama.

 
Back
Top Bottom