maisha na mahusiano

maisha na mahusiano

Tayo zeboss

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
467
Reaction score
196
habari wana jf
natumaini kwa uwezo wa MWENYEZI MUNGU kila mmoja yuko poa kwa nafasi yake; ingwa kunawengine hawapo vzuri sana kiafya muda huu pengine wapo vitandani wakiuguza majeraa mbali mbali yaliyotokana na pilika za utafutaji na wengine wakiwa mahospitalini wakiendelea kupata matibabu mbali mbali ya matatzo yao, huku wakiwa wanasoma post hii; ningependa kuwatia moyo kwamba "pamoja na matatizo yao yote yanayo wasumbua ila bado MUNGU ni mwema kwao! kwa sababu bado wanaishi hadi leo hii.

leo nilitaka ku-share na fulani idea hii ya "MAISHA NA MAHUSIANO" maisha ni safari moja ndefu sana ambayo hujulikana pale mwanzoni tu unapoachana na baba yako na mama yako, ila baada ya kuianza tu hii safari hatima yake huwa haijulikani ni wapi na nilini tutafika huko! kutokana na urefu wa safari hii ya maisha. kutokujua hatima ya safari hii inatufanya kupoteza tumaini nakujikuta tukikutana na vikwazo vingi sana ambavyo hutupelekea kuishia njiani kwa vifo!

Tatizo siyo umbali wa safari ila tatizo nikutokujua vikwazo vya safari ambavyo ndivyo chanzo cha kuona safari ni ndefu bila kuona hatima yake, na kuanza kukata tamaa na hatima yake kuishia njiani kwa kifo!
safari ya maisha ni ndefu sana kama hatutatambua vikwako, na sababu ya kuwepo kwa hivyo vikwazo

hivyo basi; nivema kuwa wapole na waelevu ili kutambua ni vikwazo gani vinavyo sababisha tusione muwafaka wa safari hii hatimaye kuona safari ni ndefu na kukata tamaa; maana, ufupi wa safari unatokana na vikwazo ambavyo ndani yake kuna mahitaji yasiyo na ulazima; pindi unapokosa hayo mahitaji matokeo yake ni ujambazi,ushirikina ukahaba, utapeli, uwongo, ulevi,wivu,hasira,magonjwa,dhiki,huzuni mwisho ukimwi na hatimaye tunaishia njiani kwa vifo vinavyo sababishwa na hayo matunda ya vikwazo.

maisha ni mepesi sana kama tukitambua vikwazo vilivyo mbele yetu na jinsi ya kuviepuka, ila maisha nimagumu sana kama tusipo tambua vikwazo vilivyo mbele yetu na kutokujua jisi ya kuviepuka! ila 99% tupo kwenye vikwazo na ndio mana maisha yetu magumu hata tuwe na bei gani lakini mahitaji hayaishi, hata tuwe na bei gani lakini madeni hayaishi, mawazo yetu ni hasi badala ya chanya; mwenye baiskeli anataka pikipiki, mwenye gari anataka ndege, wenye ndege anataka meli, ukiwa unaishi nyumbani utataka upange na ukipanga utataka ujenge na ukijenga utataka ujenge nyumba ya pili ujenga ya pili utataka zi fike kumi zikifika hiyo idadi, ghafla utataka ghorofa! hii yote ni kwa sababu tupo kwenye vikwazo! na ndio mana hatufiki mbali,


MUNGU aliyaona hayo yote na ndio mana akaumba viumbe viwili viwili ili kutiana moyo, kushauriana,kufarijiana na hatimaye kuyafika malengo na kusudio la lake kiujumla. MAISHA NA MAHUSIANO ni wazo ambalo nimependa ku-share na fulani ambaye anahisi yupo kwenye kikwazo na kujiona mpweke mwenye huzuni,kukata tamaa,kujutia nahajui ni vp atatoka kwa kukosa ushirikiano wa mawazo ushauri na hatimae kuendelea na safari kwa furaha na manani.

Fulani: siyo mtu ila ni mtu yoyote mwenye jinsi yoyote
location: siyo tanzania bali ni popote pale alipo yoyote

NB:njoo tushauriane tupeane mawazo na kutiana moyo katika safari hii ya maisha inayojulikana kama safari ndefu isiyoeleweka; wakati ni safari fupi inayoeleweka.
 
vikwazo vya kwanza ni ujinga na umaskini ,uoga wa kufanya mambo ,plus ushirikina vijijini
 
vikwazo vya kwanza ni ujinga na umaskini ,uoga wa kufanya mambo ,plus ushirikina vijijini
nikweli kabisa mkuu ila nadhani kama kipo kikwazo kikubwa vile, ambacho ndio kimebeba hayo yote! maana hayo mi nayachukulia kama matokea tu
 
Tanzania saiv ni usiku watu wamepumzika wewe unawaambia wako kwenye pilika!!

Wasiokuwa na kazi hawajui ata nyakati..yaani jua lizame na litokee..very sad!! Emu lala dogo kesho mwambie shemeji akupe mtaji ukalime korosho!!empty set
nilivyoanza kusoma hii reply yako nilidhani unabusara sana mkuu, kumbe ni heri mara mia asiye na busara; kwani kasoma alafu kapita kimya kimya.

wewe umelala usiku lakini kuna wengine wapo malindoni wanalinda huku wanaperuzi jf, wewe umelala usiku lakini kuna wengine wapo magodauni wanafanya kazi huku wana peruzi jf, wewe umelala usiku lakini kuna wengine wapo vitandani wanauguza majeraha huku wanaperuzi jf, wewe umelala usiku lakini kuna wengine wapo msibani huku wanaperuzi jf..

NB:usiishi kwa kukariri mkuu
 
Back
Top Bottom