Maisha ndani ya Manga Kissa: Internet Café za ajabu nchini Japan

Maisha ndani ya Manga Kissa: Internet Café za ajabu nchini Japan

Underthesea

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2021
Posts
327
Reaction score
882
images (17).jpeg

Manga ni riwaya picha (Kwa Kiingereza comics au graphic novels) zenye mtindo wake wa kipekee kutokea nchini Japan. Manga ni maarufu sana nchini humo kiasi kwamba kuna mamia ya maktaba zilizojaa Manga tu. Maktaba hizi huitwa Manga Kissa

images (20).jpeg

images (43).jpeg

Manga Kissa nyingi ziko karibu na vituo vya treni.

Maktaba hizi ni tofauti na maktaba za kawaida, kwani pamoja na kuwa na sehemu ya umma ambapo watu wanaweza kujisomea, huwa kuna vyumba kwa ajili ya kujisomea. Vyumba vingi ni vidogo sana kwa ajili ya mtu mmoja tu, ingawa vipo vichache vya kuweza kutosha watu wawili au kikundi kidogo.

Vyumba hivi vidogo vina upana sawa na sehemu ya mtu mmoja kwenye Internet Café zetu huku Bongo. Huwa zinakuwa na kompyuta zenye internet na kunakuwa na headphones. Pia kwa juu huwa pako wazi.
images (16).jpeg
Collage_Fotornagomi6 (1).jpg


Kwa sasa umezuka mtindo wa watu kuishi kabisa kwenye vyumba hivi. Baadhi ya watalii wanaongia nchini Japan wanaona ni bei nafuu kulala kwenye Manga Kissa kuliko kulala hotelini.

Hata wazawa wenyewe wamefanya Manga Kissa kuwa sehemu ya kwenda kupumzikia.
images (15).jpeg


Kijana mmoja alisema kuwa wanaume wenye matatizo kwenye familia zao huwa wanakimbilia kwenye Manga Kissa kwa muda.

Kuhusu malipo, Manga Kissa, unaweza kulipia kwa saa au kwa siku.

Manga Kissa huwa zina huduma za bafu. Unaenda reception, unaacha funguo, unapewa sabuni ukaoge.

images (44).jpeg


Kwa mfano hiyo inayoonyeshwa kwenye interview hapo chini, kuoga kwa dakika 15 za mwanzo ni bure. Baada ya hapo Kila dakika 10 unayoongeza unalipa dola 1.

Kila baada ya mtu kuoga lazima bafu lisafishwe na mfanya usafi kabla ya mwingine kuingia. Pia ni kawaida kukuta foleni.

Watu husifia sana usafi wa watu wa Japan kwenye Manga Kissa.
images (9).jpeg

images (22).jpeg

Pia Sheria kubwa kwenye Manga Kissa ni ukimya. Hairuhusiwi kuongea kwa sauti.

Screenshot_20210716-105938.png

Kijana mmoja aitwaye Hagi mwenye umri wa miaka 31 alihojiwa akasema yeye bado anaishi kwao, lakini siku za kazi huwa anaona bora alale kwenye Manga Kissa kuliko kupoteza lisaa limoja kwenda ofisini na lingine kurudi nyumbani kwa treni. Hayo masaa mawili bora afanye kazi, kwahiyo mwisho wa juma ndo anarudi nyumbani.


Hagi anasema Manga Kissa ni kimbilio kwa watu wenye misongo ya maisha. Ameishasikia watu wakija na kulia kimya kimya kwenye vyumba vyao.
images (6).jpeg


Tatizo moja la Manga Kissa ni kuwa vyumba vina uwazi kwa juu. Kwahiyo ni rahisi kuambukizana magonjwa, mmoja akipata mafua wote wanaugua. Hagi aliwahi kupata "Norovirus", akaamua tu kununua vyakula na kuchukua Manga kadhaa na kujifungia kwenye kachumba kake kwa siku kadhaa.

images (10).jpeg

images (13).jpeg

Pia Hagi anasema kuwa watu wengi wanaona kuwa watu wanaoishi kwenye Manga Kissa ni watu wasiojiweza kiuchumi. Lakini anasema sio kweli, wengine kama yeye inawarahisishia tu maisha na wanapenda tu mtindo wa maisha ndani ya Manga Kissa, na yeye ana mpango wa kuja kumiliki Manga Kissa yake.
 
Japan ni kati ya nchi ambazo watu wanaongoza kujiua watu wana msongo wa mawazo, jamii inategemea kila mtu aishi kwa mfumoflani, pia hawana interaction sana kiasi kwamba jirani yako anaweza kuwa anaishi peke yako akafa ndani na usijue hata kwa mwaka mzima kuwa kuna maiti inaoza
 
Japan ni kati ya nchi ambazo watu wanaongoza kujiua watu wana msongo wa mawazo, jamii inategemea kila mtu aishi kwa mfumoflani, pia hawana interaction sana kiasi kwamba jirani yako anaweza kuwa anaishi peke yako akafa ndani na usijue hata kwa mwaka mzima kuwa kuna maiti inaoza
Kweli they're very strict, na katika kutafuta hiyo human affection/interaction wanafanya vituko vingi sana nitakuja kuleta thread za vituko vya wajapan, mfano Kuna huduma za baba wa kukodi kwa wasiokuwa na baba!!
 
Kweli they're very strict, na katika kutafuta hiyo human affection/interaction wanafanya vituko vingi sana nitakuja kuleta thread za vituko vya wajapan, mfano Kuna huduma Baba wa kukodi Kwa wasiokuwa na baba!!
Yes wanafanya vituko vya ajabu, halafu system zao za kimahakama ni complicated mpaka mtu aje kufungwa inabidi uwepo ushahidi ulioshiba. Kuna wengine wanageuka kuwa psychopathy
 
Yes wanafanya vituko vya ajabu, halafu system zao za kimahakama ni complicated mpaka mtu aje kufungwa inabidi uwepo ushahidi ulioshiba. Kuna wengine wanageuka kuwa psychopathy
Kwahiyo wahalifu wanakuwa free au umemaanishaje?
 
Kwahiyo wahalifu wanakuwa free au umemaanishaje?
Yes mpaka wakija kukamatwa washafanya maafa makubwa sana. Yani wana utamaduni wao wa uhuru wa mtu kuheshimiwa unafanya hata legal process zinakuwa complicated. Yani wana upweke pia. Watu kibao wamekufa kwenye nyumba zao lakini miaka inapita hakuna hata anayeshtuka hivi huyu mtu yuko wapi.
 
Yes mpaka wakija kukamatwa washafanya maafa makubwa sana. Yani wana utamaduni wao wa uhuru wa mtu kuheshimiwa unafanya hata legal process zinakuwa complicated. Yani wana upweke pia. Watu kibao wamekufa kwenye nyumba zao lakini miaka inapita hakuna hata anayeshtuka hivi huyu mtu yuko wapi.
Disturbing!!
 
Yes mpaka wakija kukamatwa washafanya maafa makubwa sana. Yani wana utamaduni wao wa uhuru wa mtu kuheshimiwa unafanya hata legal process zinakuwa complicated. Yani wana upweke pia. Watu kibao wamekufa kwenye nyumba zao lakini miaka inapita hakuna hata anayeshtuka hivi huyu mtu yuko wapi.


Pamoja na utajiri wa nchi yao lakini wanaishi kama Wanyama.
 
Mtu anakufa ndani ya nyumba, maiti inaoza kama mzoga wa kuku na hakuna anayejua!!, hayo ni maisha gani ukizingatia utajiri wa hiyo nchi, je hakuna mifumo ya kijamii itakayowekwa kuondoa hilo ??!🤔
Sasa unajua siwez sema hili ni tatzo la mfumo wa nchi bali unaweza kukuta ni tatzo la wananchi wenyewe hakuna mtu mwenye time na mwenzie kila mtu anaishi kama vile dunian yupo pekeake
 
Sasa unajua siwez sema hili ni tatzo la mfumo wa nchi bali unaweza kukuta ni tatzo la wananchi wenyewe hakuna mtu mwenye time na mwenzie kila mtu anaishi kama vile dunian yupo pekeake


Mfumo wa mtu, familia, jamii na mwisho nchi nzima, sasa wahusika wanaweza kukaa na kuanza kutatua hilo tatizo kutoka juu kwenda chini.

Mfano, leo Tanzania mfumo Umeamua kuleta kodi ya Uzalendo tunakatwa kodi kwenye miamala ya simu upende usipende kwa ajili ya maendeleo vijijini nk. Mfumo umeamua kutoka juu kuleta maendeleo chini.
 
Back
Top Bottom