Maisha ni kujituma na kutokuta tamaa

Jstar1

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2019
Posts
1,391
Reaction score
1,347
Achana na zile nyuzi zangu kuhusu watoto wa kike na kua na tamaa, wacha nishushe wasifu wangu.

Mimi ni kijana ambaye taeheer 04/07 nilitimiza miaka 22, yaani bado damu inachemka, naishi kwa ndugu yangu mkoa fulani na nyumbani ni mkoa X.

Aisee tangu nifike ndani ya hili jiji sijawai kuacha fursa inipita, kama mnakumbuka nyuzi zangu za kujilipua uarabuni,

Lakini pia kuna mwanajamiiforums, alikua tayari kunichukulia kama mdogo wake, yaani anipe kila kitu, ikiwemo nauli, chakula, ila nilale kwa baba mkubwa na pia ela ya matumizi anipe na nimsaidie kazi ndogondogo na baada ya chuo aniajiri kabisa.

Namshukuru sana uyu mwanaforums sitamsahau japo imeshindikana, ila ntamshukuru mpaka kesho.

Siku ya leo imebadilisha maono yangu, ya kukimbilia uarabuni, na nchi nyingine za nje, naamini nitaendelea kubaki tanzania, na siki ya leo naiona kesho ambayo ntaanza kujitegemea, nmepata kazi nzuri, ambayo itabadili kila kitu kwangu.

Nilikua nmeanza kuona aibu, mtu mzima naagizwa kinu cha vitunguu swaumu, mara naambiwa nioshe vyombo, kiukweli maisha yalikua magumu nilitamani ata aridhi ipasuke, ila ilikua ni sahihi kabisa, maana kisura naonekana mtoto ila mimi najiona nimekua.

Nawaasa wenzangu, kuanzia miaka 21 na kuendelea, pigania kujitegemea, usiogope kujitoa, tena usipigane kwa mdomo, pigana kwa vitendo, kama unasoma jitaidi ukusanye vyeti, alafu anza mapambano.
 
hongera mzee usisahau kutoa hicho hicho kidogo kwa wenye uhitaji
#kisalawe_oye
 
"Kwa hiyo umepata hcho kijikaz chako na kichumba kisichokuwa na mbele wala nyuma umeanza kutuandika mtandaoni sio" alisikika mwanamama mmoja kutoka mkoa x
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…