Maisha ya Simba na somo la Unyenyekevu

Maisha ya Simba na somo la Unyenyekevu

Ben Zen Tarot

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2014
Posts
4,298
Reaction score
7,612
Hakuna kinacho dumu milele. Haijalishi ataishi kwa muda gani, Simba Mkuu hatimaye atakufa vibaya.
Hiyo ndiyo dunia.

Katika ujana wao, wanatawala, wanafukuza wanyama wengine, wanakamata, wanakula, wanameza na kuacha makombo yao kwa fisi. Lakini umri huja haraka siku hazigandi.

Mzee Simba hawezi kuwinda tena, hawezi kujiua wala kujilinda. Anazurura na kuunguruma hadi anaishiwa na bahati. Bahati ya simba Itahamia kwa fisi, simba analiwa na fisi akiwa hai. Hawamwachi wana mkata vipande vipande akiwa hai.

Maisha ni mafupi.
Nguvu zinakwisha.
Uzuri wa kimwili ni wa muda mfupi, hilo nimeliona kwa simba.
Nimeiona kwa wazee.
Kila mtu anayeishi kwa muda wa kutosha atakuwa dhaifu na atakuwa dhaifu sana wakati fulani.

Kwa hiyo, tuwe wanyenyekevu.

Tuwasaidie wagonjwa, wanyonge, wasiojiweza na muhimu zaidi usisahau kwamba siku moja tutaondoka katika jukwaa hili.

FB_IMG_1656934244481.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sikuwahi kufikiria kama Simba atakujakuliwa nayeye.. Nguvu zisituhadae
 
Fisi wakimkuta kachoka wanajua tayari msosi huu, ila fisi huwa hawajiamini kabisa wanapokuwa wanakula mzoga wa simba, wanaweza wakala kidogo halafu wakakimbia pembeni kusikilizia halafu wanarudi tena kula. Yaani unaona kabisa wanakula kwa wasiwasi, hapo ndo utaona hofu aliyoacha hadi mzoga wake unaogopwa.​
 
Fisi wakimkuta kachoka wanajua tayari msosi huu, ila fisi huwa hawajiamini kabisa wanapokuwa wanakula mzoga wa simba, wanaweza wakala kidogo halafu wakakimbia pembeni kusikilizia halafu wanarudi tena kula. Yaani unaona kabisa wanakula kwa wasiwasi, hapo ndo utaona hofu aliyoacha hadi mzoga wake unaogopwa.​
[emoji2][emoji28]
 
Back
Top Bottom