Adil_101
Senior Member
- Jul 26, 2022
- 110
- 345
PART 1:
[emoji100]Sio tu Marekani yote, we ukipata muda nenda kawaulize hata FBI kuwa huyu John Herbert Dillinger aliwafanya nini!!?, wasipokujibu nenda Kapitie Mafaili yao, Utapata majibu huko.
.
Dillinger alikuwa ni kiongozi wa kundi fulani la kihalifu lililofahamika kama, ‘Dillinger Gang’.
.
Kundi hilo linatajwa kuhusika na matukio mbalimbali, ikiwemo wizi katika benki zaidi ya 24 na pia uvamizi wa vituo vya polisi takribani 04.
.
John Dillinger alizaliwa June 22, 1903, pale 2053 Cooper Street, Indianapolis, Indiana.
.
Akiwa ni mtoto wa pili wa Mr John Wilson Dillinger (1864–1943) na Bibie Mary Ellen "Mollie" Lancaster (1870–1907).
.
Tabia chafu chafu za Dillinger zilianza kuchipua akiwa ‘Teenager’, ambapo mara kadhaa baba yake alisogezewa kesi za mwanae kupiga watoto wenzie na kuwafanyia ‘bullying’.
.
Dillinger aliacha shule mapema sana, na kisha akaanza kufanya kazi pale ‘Indianapolis machine shop’.
.
Baba yake na Dillinger akahisi kama kasi ya mitaa kumlea mwanae inazidi kuongezeka, hivyo akaamua kuihamishia familia yake yote kule Mooresville, Indiana mwaka 1921.
.
Huko sasa ndio mambo yakazidi kuwa mabaya, kwa maana mwaka 1922, Dillinger alikamatwa na Polisi kwa kosa la wizi wa vipuli vya magari, na hapo ndipo ukaribu wa yeye na baba yake ukayumba.
.
Kutokana na utundu wake wa kwenye vipuli vya mashine, Despite uhuni wake Dillinger aliajiriwa na United States Navy mwaka 1923 kama ‘Petty officer third class Machinery Repairman’.
.
Huko hakudumu sana, yakamshinda na akaona arejee Mooresville, ambako huko alikutana na bibie Beryl Ethel Hovious na kisha wakafunga pingu za maisha siku ya 12/04/1924.
.
Inasemeka mwana alijitahidi sana kutulia kwenye ndoa, ila inaaminika mambo ya ndoa yakawa kama yanamkataa hivi.
.
Kwasababu alikuwa ni Jobless, akaamua kumtafuta rafiki yake wa muda mrefu Ed Singleton na kisha wakapanga tukio lao la kwanza la uhalifu, na wawili hao wakafanikiwa kuvamia Grocery fulani, na kuiba kama $50 hivi.
.
Shuhuda Mmoja aliamua kutoa taarifa ya tukio hilo kwa Polisi.
.
Wawili hao wakakamatwa na polisi siku iliyofuata, Ed akasema yeye hakuhusika akakataa kata-kata, na kwa bahati mbaya/nzuri hakukuwa na vithibiti vyovyote eneo la tukio vilivyoweza kuthitisha kuwa Ed alihusika.
.
Ila kwa Dillinger, hali ilikuwa ni tofauti kidogo.
.
Siku ya tukio, Dillinger alimshambulia mmoja ya wafanyakazi wa kile ki Grocery kwa bolt ya mashine, kwaio kulikutwa na uthibitisho wa uwepo wake kwenye eneo la tukio.
.
Kabla hukumu haijatoka, Baba yake na Dillinger ambaye alikuwa ni mtumishi katika kanisa la ‘Mooresville Church’ aliongea na aliyekuwa mpelelezi wa kesi hio Omar O'Harrow, na wawili hao wakashauriana kumsihi Dillinger kukiri makosa ya kuhusika na tukio hilo, wakidhani labda hio ingesaidia kupunguza adhabu ya Dillinger baada ya hukumu.
.
Badala yake, kutoka miaka 10, Dillinger akachapwa miaka 20 Jela.
.
Baba yake alijitahidi sana Kumuomba hakimu ampunguzie adhabu mwanae, ila jitihada hizo ziligonga mwamba.
.
Mwana akatupwa Indiana State Prison Mwaka huo wa 1924
.
Mara tu ya kutupwa humo, katika siku za mwanzo kabisa, Dillinger aliwaambia wafugwa wenzake kuwa “I will be the meanest bastard you ever saw when I get out of here”.
.
Vipimo vya awali vya afya yake kama mfungwa, vilionesha kuwa Dillinger alikuwa na kipindupindu kikali sana ambacho hata matibabu yake pia yalikuwa ni special na yenye maumivu Makali.
.
Akiwa humo humo gerezani, Dillinger anakutana na wahuni wengine kama Harry "Pete" Pierpont, Charles Makley, Russell Clark, na Homer Van Meter, ambao wote hao kwa pamoja wanapanga tukio jingine la uhalifu wa kuivamia benki fulani, endapo kama watafanikiwa kutoka gerezani humo.
********** END OF PART 1 **********
[emoji100]Sio tu Marekani yote, we ukipata muda nenda kawaulize hata FBI kuwa huyu John Herbert Dillinger aliwafanya nini!!?, wasipokujibu nenda Kapitie Mafaili yao, Utapata majibu huko.
.
Dillinger alikuwa ni kiongozi wa kundi fulani la kihalifu lililofahamika kama, ‘Dillinger Gang’.
.
Kundi hilo linatajwa kuhusika na matukio mbalimbali, ikiwemo wizi katika benki zaidi ya 24 na pia uvamizi wa vituo vya polisi takribani 04.
.
John Dillinger alizaliwa June 22, 1903, pale 2053 Cooper Street, Indianapolis, Indiana.
.
Akiwa ni mtoto wa pili wa Mr John Wilson Dillinger (1864–1943) na Bibie Mary Ellen "Mollie" Lancaster (1870–1907).
.
Tabia chafu chafu za Dillinger zilianza kuchipua akiwa ‘Teenager’, ambapo mara kadhaa baba yake alisogezewa kesi za mwanae kupiga watoto wenzie na kuwafanyia ‘bullying’.
.
Dillinger aliacha shule mapema sana, na kisha akaanza kufanya kazi pale ‘Indianapolis machine shop’.
.
Baba yake na Dillinger akahisi kama kasi ya mitaa kumlea mwanae inazidi kuongezeka, hivyo akaamua kuihamishia familia yake yote kule Mooresville, Indiana mwaka 1921.
.
Huko sasa ndio mambo yakazidi kuwa mabaya, kwa maana mwaka 1922, Dillinger alikamatwa na Polisi kwa kosa la wizi wa vipuli vya magari, na hapo ndipo ukaribu wa yeye na baba yake ukayumba.
.
Kutokana na utundu wake wa kwenye vipuli vya mashine, Despite uhuni wake Dillinger aliajiriwa na United States Navy mwaka 1923 kama ‘Petty officer third class Machinery Repairman’.
.
Huko hakudumu sana, yakamshinda na akaona arejee Mooresville, ambako huko alikutana na bibie Beryl Ethel Hovious na kisha wakafunga pingu za maisha siku ya 12/04/1924.
.
Inasemeka mwana alijitahidi sana kutulia kwenye ndoa, ila inaaminika mambo ya ndoa yakawa kama yanamkataa hivi.
.
Kwasababu alikuwa ni Jobless, akaamua kumtafuta rafiki yake wa muda mrefu Ed Singleton na kisha wakapanga tukio lao la kwanza la uhalifu, na wawili hao wakafanikiwa kuvamia Grocery fulani, na kuiba kama $50 hivi.
.
Shuhuda Mmoja aliamua kutoa taarifa ya tukio hilo kwa Polisi.
.
Wawili hao wakakamatwa na polisi siku iliyofuata, Ed akasema yeye hakuhusika akakataa kata-kata, na kwa bahati mbaya/nzuri hakukuwa na vithibiti vyovyote eneo la tukio vilivyoweza kuthitisha kuwa Ed alihusika.
.
Ila kwa Dillinger, hali ilikuwa ni tofauti kidogo.
.
Siku ya tukio, Dillinger alimshambulia mmoja ya wafanyakazi wa kile ki Grocery kwa bolt ya mashine, kwaio kulikutwa na uthibitisho wa uwepo wake kwenye eneo la tukio.
.
Kabla hukumu haijatoka, Baba yake na Dillinger ambaye alikuwa ni mtumishi katika kanisa la ‘Mooresville Church’ aliongea na aliyekuwa mpelelezi wa kesi hio Omar O'Harrow, na wawili hao wakashauriana kumsihi Dillinger kukiri makosa ya kuhusika na tukio hilo, wakidhani labda hio ingesaidia kupunguza adhabu ya Dillinger baada ya hukumu.
.
Badala yake, kutoka miaka 10, Dillinger akachapwa miaka 20 Jela.
.
Baba yake alijitahidi sana Kumuomba hakimu ampunguzie adhabu mwanae, ila jitihada hizo ziligonga mwamba.
.
Mwana akatupwa Indiana State Prison Mwaka huo wa 1924
.
Mara tu ya kutupwa humo, katika siku za mwanzo kabisa, Dillinger aliwaambia wafugwa wenzake kuwa “I will be the meanest bastard you ever saw when I get out of here”.
.
Vipimo vya awali vya afya yake kama mfungwa, vilionesha kuwa Dillinger alikuwa na kipindupindu kikali sana ambacho hata matibabu yake pia yalikuwa ni special na yenye maumivu Makali.
.
Akiwa humo humo gerezani, Dillinger anakutana na wahuni wengine kama Harry "Pete" Pierpont, Charles Makley, Russell Clark, na Homer Van Meter, ambao wote hao kwa pamoja wanapanga tukio jingine la uhalifu wa kuivamia benki fulani, endapo kama watafanikiwa kutoka gerezani humo.
********** END OF PART 1 **********