Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,761
- 216,011
Miaka ile ilikua ni habari za mdomo tu, unafahamishwa wafanya biashara wenye huduma ya kutuma pesa. Wengi walikua Kariakoo. Walifanya huduma hii katika mikoa yenye biashara zao.
Ukifika pale unatoa maelekezo ya ndugu yako aliye Arusha, jina lake na namba yake ya simu. Wanaandika katika daftari. Unaacha pesa unayotaka einde Arusha. Kwa kila transaction walichukua kama 2,000 ya vocha ya simu.
Kule Arusha utampigia ndugu yako simu, anakwenda dukani, au atapiga simu kwanza na kuwataarifu kuwa anakwenda. Akifika wanampa pesa ana saini daftari na kuondoka.
Ilijenga undugu na kuaminiana. Mara nyingi ukifika kama wamekuzoea utafanya na shopping ya mahitaji yako baada ya kukabishiwa mzigo wako. Wakijua unakaa mbali watakupa na chakula kabla hijaondoka. Na mkizoeana sana wanaweza kukupa pesa na ndugu yako akituma mnalipana.
Hii iliwasaidia wao kutokuzunguka na pesa ya biashara. Akifuata mahitaji ya duka Dar hela zinakua zipo Dar.
Baada ya miamala kuanza undugu na urafiki huu ulikufa. Ninadhani sasa ni wakati wa kufufuka upya.
Ukifika pale unatoa maelekezo ya ndugu yako aliye Arusha, jina lake na namba yake ya simu. Wanaandika katika daftari. Unaacha pesa unayotaka einde Arusha. Kwa kila transaction walichukua kama 2,000 ya vocha ya simu.
Kule Arusha utampigia ndugu yako simu, anakwenda dukani, au atapiga simu kwanza na kuwataarifu kuwa anakwenda. Akifika wanampa pesa ana saini daftari na kuondoka.
Ilijenga undugu na kuaminiana. Mara nyingi ukifika kama wamekuzoea utafanya na shopping ya mahitaji yako baada ya kukabishiwa mzigo wako. Wakijua unakaa mbali watakupa na chakula kabla hijaondoka. Na mkizoeana sana wanaweza kukupa pesa na ndugu yako akituma mnalipana.
Hii iliwasaidia wao kutokuzunguka na pesa ya biashara. Akifuata mahitaji ya duka Dar hela zinakua zipo Dar.
Baada ya miamala kuanza undugu na urafiki huu ulikufa. Ninadhani sasa ni wakati wa kufufuka upya.