Maisha yangu ni mazuri kuliko walezi wangu kwa kipindi chao. Je, nipo kwenye uelekeo wa kutusua au zama tu zimebadilika?

Maisha yangu ni mazuri kuliko walezi wangu kwa kipindi chao. Je, nipo kwenye uelekeo wa kutusua au zama tu zimebadilika?

Ncha Kali

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2019
Posts
15,335
Reaction score
29,114
Umuofia kwenu ndugu zangu

Kwanza ieleweke kuwa sipo hapa kujigamba wala kujipigia mstari, ni swali la kawaida tu nimelenga kuwashirikisha na kujifunza kwenu.

Ni kijana japo umri umesonga lakini sio kivile, elimu ya hapa na pale japo sioni kama naitumia moja kwa moja ila inaninufaisha na imesaidia kunichorea ramani ya maisha yangu.

Nilizaliwa na kukulia vijijini ndani ndani huko, ila baada ya kuonekana mwenye uwezo darasani na tabia njema, ikamshawishi ndugu mmoja kunivuta ili nikaishi na kusomea kwake.

Huyu ndugu ni babangu mkubwa ambaye alikuwa akiishi ‘mjini’ ukilinganisha na kwetu, ni mtumishi wa umma hivyo hata hali ya yake ilionekana ni maisha fulani ya kishua.

Kupitia baba huyu nikapata kuosha macho [exposure] na kujua upande mwingine wa dunia, mjini, na hivyo kujionea na kujifunza na kufurahia maisha mapya.

Hoja yangu iko hapa:

Pamoja na kile nilichokiona kuwa maisha mazuri na ya kisasa, lakini babangu huyu hakuwa na simu, nyumbani hakukuwa na TV japo ya chogo.

Makochi ya mbao na mito yalipamba sebule yakifunikwa vema na vitambaa, nyumba kubwa lakini madirisha hakuna nondo wala aluminiamu.

Hapo ni familia yenye kuheshimika baba na mama wote ni watumishi na mishahara inaingia, umri wao kipindi hicho ni kwenye miaka 45 hivi, kiufupi maisha yalikuwa mazuri kabisa.

Na hata ukiacha hapo, majirani pia na watumishi wengine sio kwamba walikuwa na maisha mazuri kuzidi... la hasha kote ilikuwa kama sawa tu na hata waliokuwa na TV basi ni chogo.

Sasa leo hii mimi katika miaka yangu 30 hii, japo sijajenga ila nalipa kodi nyumba ambayo ni bora kabisa, kodi ambayo siwezi kuwatajia wazee wangu hawa wataona nafuja pesa japo kwangu naona ni hadhi yangu.

Nimeweza kumiliki vitu vya thamani kiasi chake, hapa siongelei maTV makubwa na simu kali ila gari naogopa kurogwa [emoji16][emoji16][emoji16]

Na hapo sioni kama nimefika ila si haba kushukuru, yes naishi vema, maisha fulani ambayo wakinitembelea hawa wazee wangu ambao kwa sasa ni wastaafu wanahisi kupumzika.

Nina familia yangu, ndugu na wategemezi tumaini lao ni kwangu. Sijajenga wala sina gari lakini ramani yote ipo sawa ni suala la utekelezaji tu, InshaAllah.

Sasa nilichojiuliza ni kama hivi, ni nyakati tu zimebadilika na imekuwa kawaida kumiliki hivi vitu, au ni kweli nipo kwenye ‘raiti traki’ kuyaelekea mafanikio?

Wazee wetu walioishi na kusota hadi hadi kustaafu ndo wanajenga, ni kwa sababu ya nyakati au ni kweli maisha yalikuwa magumu.?

Sijui kama nimeeleweka, nitarudi, acha nijifukize kwanza.
 
sio hawakutaka hivyo vitu vizuri ila ni kipaumbele waliona bora mtoto wa ndugu yao asome kuliko kuwa na tv nzuri....
 
Mimi nakupongeza ila naomba tushirikishe bussiness inayokuweka mjini. nlijichanga sana mpaka kufikia milion kadhaa lakn mwishon mwa mwaka jana cjui nilikosea nn nkazizika rasmi kwny biashara flan hv ambayo haikunpa hata mia.
 
nafatilia sana uzi wako, nadhani tupo njia moja mimi na wewe mkuu
 
Yaani umepanga alafu unaona wanaoishi kwao umewazidi?

Ingekua kujenga na kununua gari ni kuchora ramani nafikiri yangekua mengi kuzidi majani huko mtaani.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hujaelewa vizuri mkuu mfano wangu unahusisha nyakati tofauti na wala sio kama nawazidi, nimelinganisha ubora wa maisha niliyopitia mimi na hatua walizopiga ambao nilijifunza kwao.

Bila shaka hata kwenu unaona wazee wanaojenga au kununua nyumba wakistaafu, hata kama walijenga zamani ila zinakuwa ‘zimepitwa na wakati’.

Bado kuishi vema sio lazima ujenge mkuu, wewe jenga nitakuja kupanga hapo nikulipe.
 
mm nakupongeza ila naomba tushirikishe bussiness inayokuweka mjini. nlijichanga sana mpaka kufikia milion kadhaa lakn mwishon mwa mwaka jana cjui nilikosea nn nkazizika rasmi kwny biashara flan hv ambayo haikunpa hata mia.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sina maajabu kivile, huenda tu matarajio yangu kwenye maisha sio makubwa ndiyo maana naona kuridhika mapema.... usikate tamaa.
 
zama zimebadilika zamani kushona ndala ilikua kawaida ila siku hizi no,hata hivyo vitu tv,sabufa zamani havikupatikana kirahisi ila siku hizi kila mtaa una duka la Tv,kwahiyo wewe kazana ni zama si mafanikio kiviile japo wengne hawana
 
Sasa tutapimaje hayo mafanikio yako mpwa? Nyumba huna, tutajie basi account yako bank inasomaje, unatuambia umepanga nyumba kiasi usemi, unaweza kuona kwako ni kikubwa kumbe ni katone tu,

Katika hili ni wewe tu na huyo na huyo babako ndio mnaweza kupimana. I am Sorry for being harsh.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni mambo ya nyakati kubadilika, ni sawa na maendeleo kitaifa leo tunajenga barabara mpya na kuzibomoa za zamani.

Wakati huo hizi tunazibomoa leo walijivunia watangulizi wetu, na kwao waliona wamepiga hatua.

Kwa upande wako vipaumbele vilikuwa tofauti, na hata upatikanaji vya hivyo vitu baadhi ya maeneo vilichelewa kwa sababu ya ujamaa.

Pengine maendeleo mfano magari ilichukuliwa kama anasa, pengine hofu ya kurogana kama kwetu kule.

Mambo kama simu na TV kali hazikuwepo, fanicha sio kwa mitindo ya kisasa ila kwa nyakati zao zilikuwa fasheni na ishara ya maisha bora.
 
Sasa tutapimaje hayo mafanikio yako mpwa? Nyumba huna, tutajie basi account yako bank inasomaje, unatuambia umepanga nyumba kiasi usemi, unaweza kuona kwako ni kikubwa kumbe ni katone tu,

Katika hili ni wewe tu na huyo na huyo babako ndio mnaweza kupimana. I am Sorry for being harsh.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa mfano rahisi ankali, wewe umekulia nyumba ya vioo (aluminum)? wazazi wako waliweza lini kumiliki simu? Pengine hata nyumba ya umeme?

Ni vitu vichache kama hivyo unaweza kutumia kupima, jibu litakujia kuwa ni nyakati tofauti.
 
Back
Top Bottom