Uchaguzi 2020 Majaliwa: Tutazipeleka Koroboi na Vibatali makumbusho ya Taifa

Uchaguzi 2020 Majaliwa: Tutazipeleka Koroboi na Vibatali makumbusho ya Taifa

eddy

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2007
Posts
16,054
Reaction score
11,568
Leo Waziri Mkuu alivyokuwa Lamadi akielekea Bunda ameongea maneno mazito sana kuwa Serikali ya JPM imenuia kuhakikisha kila kaya ina umeme

Iwe ya nyasi tembe mbavu za mbwa zote zitawekewa umeme na kama nguzo hazifiki mfano visiwani watafungiwa sola hukohuko, hakuna kutumia kibatali wala koroboi wala chemli wala karabai hizi zote zitakuwa zana za kale zitapelekwa makumbusho ya taifa kama kumbukumbu.

Kaka Kasim kaagiza nguzo zigawiwe bure, tena zigawiwe ka njugu, hata kama uko nyuma ya mlima nguzo itakufuata hukohuko,

Kwa wapenzi wa kufugafuga kuku bata si ndio neema hii kule shambani kwangu nitaweka na mabanda ya kuku kabisa umeme upo.

JPM hapa masikini katukomboa kwelikweli, namie najitolea laki wahitaji watano wawekewe umeme nao.

Ndio maana alisisitiza bwawa la nyerere lijengwe haraka kumbe tusijekosa umeme maana mambo ya mgao hataki kabisa kusikia.
 
Haya maneno hata kwenye kanga yapo, nenda Tanesco leo kama utapewa hata waya bure
 
Kama ni hivyo kwanini juzi Tanesco juzi wamenunua majeneretor kwa ajili ya matumizi ya ofisi zao ?
 
Kama ni hivyo kwanini juzi Tanesco juzi wamenunua majeneretor kwa ajili ya matumizi ya ofisi zao ?
Bwawa bado linajengwa; hata hivyo mimi kijijini kwetu siku hazi hatutumia chemli wala vibatali tena. Imetusaidia sana kwani hata maji sasa tunavuta chini kwa submersible pump tu; niliwapa jamaa wakaja na drill yao kuchimba kisima kwa milioni mbili na nusu- najua walinigonga ila nilikuwa na haraka kabla ya kurudi kazini, sasa hivi maji hayo yanatumika mtaa wote bure tu na wala bili ya umeme vijini siyo kubwa kama mijini. Sijui rationale yake economically, ila ndugu zangu siku hizi wanaula sana
 
Back
Top Bottom