DOKEZO Majembe Auction Mart waiba madirisha Majohe

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Wakati mwingine huwa sielewi
Hao watu wanakuwaga wapi mpaka watu wanajenga kunahamiwa halafu baadae wanasema maeneo ni yakwao??
Why wasijitokeze awali kabisa wanapoona watu wanaanza kupaendeleza??
Yaani watu wajenge wahamie pageuke mji halafu unakuja kusema ni eneo lako unakuwa wapi muda wote huo hayo yakifanyika.
 
Haya mambo ya ardhi ni mtihani Sana

Nakumbuka huko maeneo ya kerege bagamoyo,wananchi WA pale walivamia maeneo ya watu,tukapewa taarifa maeneo yanauzwa,Mimi na mke wangu na baadhi ya wadau tukajichanganya tukanunua, nakumbuka tulinunua viwanja viwili na wife kama 2,000,000/=

Daah baadae mwenyewe karudi,ikajulikana wananchi wamevamia eti kisa mwenyewe hakuwepo Muda mrefu,hakukuwa na namna zaidi ya kupoteza hela.

Tukafungua kesi dhidi ya waliotuuzia tukaenda nayo,si unajua danadana za mahakama tena,mara jaji kaenda likizo mara kurushwa tarehe,tukaona isiwe tabu tutakuja kulipana katika mahamaka ya Allah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…