Awali nilileta lalamiko la kutokuwepo huduma ya maji kwa muda mrefu bila sababu yoyote huku magari ya kuuza maji yakiwa yanaranda mitaani kuuzia watu maji kwa gharama kubwa.
Baada ya lalamiko hilo huduma hiyo imeanza kutolewa japo sio kila siku ila angalau mara moja kwa wiki maji yanatoka kwa masaa kadhaa angalau yamepunguza adha ya ununuaji wa maji kwa bei juu kwani watu hukinga na kuyahifadhi.
Your browser is not able to display this video.
Pamoja na kurejea, maji kutoka kwa wiki bado hayajfikia hitaji letu, tunahitaji jitihada zifanyike zaidi maji yawe yanatoka kila wakati bila kukatika kwani ni hitaji, na haki yetu kupata huduma hii muhimu na ya msingi kila wakati pasi na kupewa kwa siku na siku.
Sambamba na hilo asante sana JamiiForums Shukrani zangu za dhati kwenu kwa kupaza sauti zilozofika kwa walengwa ambapo awali walitolea ufafanuzi na kisha kuanza utekelezaji mara moja na kisha huduma kuletwa, mbarikiwe sana.
Awali nilileta lalamiko la kutokuwepo huduma ya maji kwa muda mrefu bila sababu yoyote huku magari ya kuuza maji yakiwa yanaranda mitaani kuuzia watu maji kwa gharama kubwa.
Baada ya lalamiko hilo huduma hiyo imeanza kutolewa japo sio kila siku ila angalau mara moja kwa wiki maji yanatoka kwa masaa kadhaa angalau yamepunguza adha ya ununuaji wa maji kwa bei juu kwani watu hukinga na kuyahifadhi.
Pamoja na kurejea kwa kuyoka kwa wiki bado tunahitaji jitihada zifanyike maji yawe yanatoka kila wakati bila kukatika kwani ni hitaji, haki yetu kupata huduma hii muhimu na ya msingi kila wakati pasi na kupewa kwa siku na siku.
Sambamba na hilo asante sana JamiiForums Shukrani zangu za dhati kwenu kwa kuoaza sauti zilozofika kwa walengwa ambapo awali walitolea ufafanuzi na kisha kuazna utekelezaji mara moja na kisha huduma kuletwa, mbarikiwe sana.