Majibu: Rais yupo sahihi anaposema kuna watu wameficha pesa ndani kuihujumu serikali

Mkuu naona sasa umeanza kutangaza dini! Suala la ugonjwa ni suala la nafsi, na siyo suala la kimfumo.! Uchumi ni mfumo! Hata mimi nimeshuhudia nyumba ambayo ingeweza kuuzwa kwa milioni 30 ikiuzwa milioni 10. Sababu ya bei hiyo sitaitaja. Unajua siyo kila bidhaa itaingia sokoni ifikie kununuliwa. Mfano nyumba. Kwa hiyo kama unatafuta pesa ya matibabu utauza kwa bei yoyote.! Kuhusu Ben Saanane. Namheshimu sana japo sijawahi kumuona. Naomba nikwambie kwamba maarifa hayaanzii kwa Ben Saanane. Yapo miaka mingi kabla ya wewe na hiyo ID yako na Ben Saanane hamjazaliwa. Kubwa kuliko yote, maarifa yote yanaletwa na watu. Kwa hiyo mimi kujifunza kwa Ben Saanane wewe kwako ni ajabu.! Kitu kimoja ambacho ni hasara kwa taifa ni wanafunzi kutosoma vitabu, badala yake wanashinda na kukesha wakisoma past papers. Taratibu tu mwishowe utaelewa.
Ny
Yha,msichanganye mambo vijana.

Wewe jiulize tu mama yako mgonjwa anahitaji kutibiwa umehanganika k
 
Tofautisha kuhifadhi ndani na benki,wale waliohifadhi uswiss wanapata faida ya riba kule ila mtu akihifadhi ndani huku anapata faida gan?
 
Na pesa zilizopo Kwa mobile money agents au wanaotumia simu pesa nazo zimefika?
 
Nafikiri twende kwenye hoja ya msingi,eleza huu mfumuko wa bei ambao kwa uelewa wako umedai ndio chanzo cha ugumu wa maisha kwa sasa.Ufafanue hili kulingana na mazingira ya sasa ni imani yangu jibu litapatikana
 
Tofautisha kuhifadhi ndani na benki,wale waliohifadhi uswiss wanapata faida ya riba kule ila mtu akihifadhi ndani huku anapata faida gan?
Mkuu kuhifadhi mamilioni kwasababu yakupata riba wewe unaona ndio lengo lao?Wewe una milioni 100,000,000 unaambiwa weka fixed account halafu mwisho wa mwaka upate interest ya 10% utaziweka ama utafanya biashara?Wale zile pesa wamezificha kule lengo ni kuhofia kwakua ni nyingi lazima wanaweza wakaulizwa wamezipataje na ndio maana wakaziondoa lakini hawakufuata hizo interest huko.Na ndio maana tunasema hawa walioficha hizi pesa lengo lao kubwa ni ku haribu uchumi kuikomoa serikali
 
Uchumi ni taaluma kama kila mtu alivyo na ya kwake.
Ukiingia anga za watu bila hodi ndo kauli kama hizi.
 
RAiSI KUBADILI NOTI SIO SUlUHU
Mnamo hapo jana MH.JP Magufuli alitishia
kubadili noti ili kuwakomesha wale waliozificha
lengo ni kuwataka waweke fedha benki ili ziingie
kwenye mzunguko. Kisiasa ni rahisi sana kufanya
hivyo ila ni kiuchumi ni vigumu sana kufanya
hivyo.
Kumbukumbu zinaonyesha ili fedha ipotee
kwenye mzunguko inachukua zaidi ya miaka
mitano na kuendelea which means hata Noti
zikibadilishwa leo bado wale waliozificha
wataendelea kuzitumia mpaka Mwaka 2021 kwa
mantiki hiyo tatizo la upotevu wa fedha kwenye
Taasisi mbalimbali za kifedha halitatatuliwa
kirahisi.
Fedha kwenye mashirika ya fedha ipotelea wapi?
Mojawapo ya maswali magumu ambayo
watanzania wengi wameshindwa kuyaelewa kwa
kina ni wapi fedha imepotelea.
1.Ongezeko la kodi kwenye miamala ya fedha
(increase in transaction cost). Serikali
ilipotangaza ongezeko la kodi ya ongezeko la
thamani (VAT) iliwaathiri moja kwa moja
watumiaji wa sarafu ya shilingi. Mfano rahisi
Asilimia 18 ilioongezwa kwenye bei ya kufanyia
miamala ilipunguza kwa kiasi kikubwa Bank
deposits za watu kitu kilichopelekea pesa nyingi
kurudi mikononi mwa watu na benki nyingi
kukosa pesa kwa ajili ya kufanya shughuli za
kifedha nchini. Hapo utaona aienufaika ni TRA
kwani mapato yameongezeka kwa asilimia 18 ya
kila muamala anaofanya mtu mmoja.
2.Ongezeko la bei za vitu muhimu kama sukari.
Ugumu mwingine uliosababisha fedha ipungue
benki na kurudi mikononi mwa watu imechangiwa
kwa kiasi kikubwa na kuongezeka kiholela kwa
bei ya sukari which means sukari iliokua inauzwa
sh.2000 ilipanda hadi Zaidi ya shilingi
2700,matokeo yake kiuchumi Ilipunguza kwa kiasi
kikubwa pesa mikononi mwa watu kwa zaidi ya
asilimia 40 na kupelekea pesa benki kupungua
kwa asilimia zaidi ya 40 kwa kila kilo ya sukari
ilionunuliwa.
3. Serikali kubana matumizi(Reduction in
government expenditure). Hapa napo tulifeli kwa
kiwango kikubwa serikali ilibana matumizi
yaliosadikiwa sio ya lazimaa,hapa napo pesa
badala ya kwenda kwenye mikono ya watu wengi
iliishia kwenye mkono mmoja wa serikali hivyo
kupunguza kiwango kikubwa cha pesa kwenye
mzunguko
4.Kodi kubwa na mizigo kwenye sekta ya utalii
na bandarini. Mwezi uliopita iliripotiwa kua
Magari kwenye bandari ya Dar es salaam
yamepungua kutoka magari 3000 hadi magari
1500 kwa siku moja,na hii ilisababishwa kwa
kiasi kubwa na ongezeko la kodi huku serikali
ikidhamiria kukusanya mapato mengi ndani ya
muda mfupi.Hapo tulifeli kwa kiasi kikubwa kwani
tunazungukwa na nchi washindani wenye bandari
kubwa kuliko yetu kwa Mfano Msumbiji na
kenya.Wafanya biashara wengi wamekimbilia
huko kwa hofu ya kupata hasara,madhara yake ni
watu wengi kukosa ajira na hivyo kupelekea
kukosekana kwa ujira ambao ungeweza kuongeza
pesa kwenye mzunguko.
Nini kifanyike sasa?
Ni dhambi kubwa kuwakomoa watu waliojiwekea
fedha walizotafuta kwa jasho lao wenyewe na
hata sarafu ikibadilika bado hawataweza
kuathirika moja kwa moja. Serikali ingejitahidi
kuongeza idadi ya pesa nyingi kwenye mzunguko
kwa kutumia benki kuu ya Tanzania. Hapa Benki
kuu inatakiwa kununua bonds kutoka kwa watu
binafsi na mashirika ya watu binafsi ili ku
dispense more amount kwenye mzunguko, pili
kodi zisizo za msingi zipunguzwe ili
kuwashawishi watu waendelee kutumia mashirika
ya kifedha. Benki ni kama mfanyabiashara tu
ambae yupo pale kwa ajiri ya kujipatia faida sasa
ukiongeza kodi ina maanisha mtu wa mwisho au
benki yenyew inaweza kubeba mzigo mzito
ambao ni vigumu kuutua na utaangukia uchumi
wa nchi nzima (Macroeconomics)
Owen j chimela
 
Hivi kinachofubaza akili yenu ni nini??
Ata uwe layman wa uchumi vitu vidogo kama hivi lazima uvijue tu, sasa rais anasema watu wameficha pesa ajichunguze aone serikali imetangaza tenda ngapi za miradi mikubwa, na mingapi inafanya kazi?

Pia azingatie hakuna mtu anafanya biashara isiyo na faida watu wamewithdraw pesa kwenye mzunguko labda hawapati faida kwenye biashara win to win situation possibly hakuna uwezi kufanya biashara alafu faida yote unalipa kodi. Kwa hali kama hii lazima watu watafute shadow environment aidha kwa kuhamisha miradi au kuset new businesses.

Hapa kuna principal za uchumi zinatumika kujibu maswali magumu haya.
 
Mkuu acha kuchanganya mambo.
Wewe unasema kuongezeka kwa tozo kwenye miamala ya kibenki kumepelekea watu kubaki na pesa mifukoni sasa kwanini hao waliobaki na pesa mifukoni wanalalamika hawana pesa?
Unasema BOT wanunue bond kwa watu binafsi ili kuongeza pesa kwenye mzunguko ki vipii wakati unaona taasisi zinafilisika kwakukosa pesa?
Unatoa takwimu za mapato yatokanayo na kodi kushuka bandarini kwani mizigo imepungua wakati bandari pamoja na makusanyo ya nchi yanaonesha kuongezeka kila siku,unatumia data zipi?
Kupanda kwa Sukari imepunguza 60% ya pesa mikononi mwa watu,are serious?
 
Sio kila kitu mnakosoa na elimu zenu za ukawa. Mleta hoja yuko sahihi. As an individual and a country at large we are facing high deflation rather than inflation. There is no enough money in the circulation that money has become scarce while it's devaluating
 
Kama mzunguko wa fedha hauna msaada kwa wafanya biashara kwanin wasiache
 
Bado nasubiri jibu la mwisho na sahihi kwa janga hili.......
 
Ila kiukweli ela utafute wewe jasho lako mwenyewe...Sasa hii ishu ya kupangiwa pa kuiweka inanichanganyaπŸ™πŸ™πŸ™
*Anyway nipeni pesa bure bila kutafuta na kutoa jasho langu*
 
Yaani mtu akubali kuhifadhi fedha bila kuitumia wala kuizalisha, pesa yenyewe inashuka thamani kila siku kwa lengo tu la kumkomoa Magufuli?
majasusi wanaweza hiyo kazi,wanaingiza hata dola bilion 3 tu,wanatumia kupata madafu na kuyapiga moto,
nyie mtabaki mnatafuna humu ndani
 
uko sahihi saana,umeniwakilisha[emoji119] [emoji119] [emoji119] [emoji119] [emoji119] [emoji119]
 
wanauchumi wamekaa wakatafakari wakaandika, purchasing power ikipungua lazima bei itashuka, sasa unachokataa ni nini kuwa kama pesa haipo means purchasing power itapungua na ivyo kitasababisha bei ishuke regardness kwa sababu za cost
 
Hapa ndipo unagundua elimu yetu haitusaidii kitu ni mwendo wa kucrem tu, kama mtu unashindwa kuelewa tofauti ya deflation na inflation in application,
Inapoongelewa pesa iliyofichwa hawazungumzii pesa zilizoifadhiwa bank za ndani na za nje , sababu pesa yoyote inayowekwa bank haikai uko inarudishwa in circulation, na zile zinazoifadhiwa bank za nje kule hupeleki TSH unadeposit Dollar, ko bado hiyo haiaffect lolote sababu bado pesa itakuwa in circulation. Kama ingekuwa watu wanhifadhi pesa zao benk kwa kuogopa basi isingeaffect lolote
Kwa namna yoyote hali ya kuotokuwepo pesa mikononi mwa watu inamaanisha pesa zimeshikiliwa mikononi na hapo inamaanisha pesa in circulation imeondolewa
Na hii itasababisha watu kupungua uwezo wa kupurchase, purchase power ikipungua itapelekea delfation na sio inflatio.
Watanzania tuache kuwaza kisiasa wa upande flani katika mambo yasiyohitaji siasa hasa uchumi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…