Majibu ya hata Ulaya; USA wanafanya ni kupotoka (Statistics are like bikinis. What they reveal is suggestive, but what they conceal is vital.')

Majibu ya hata Ulaya; USA wanafanya ni kupotoka (Statistics are like bikinis. What they reveal is suggestive, but what they conceal is vital.')

Logikos

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
15,460
Reaction score
24,233
Tuliambiwa hata United Kingdom Bandari wamewapa watu.., ni kweli UK hata uzalishaji siku hizi hawafanyi kama zamani magari yao yote ni mali za wengine..., UK baada ya ukoloni kuisha ilijikita kwenye Service industry (pamoja na kuuzia watu silaha); ila muhimu kabisa walijikita kwenye Service ya kutakatisha Pesa za walamba asali duniani kutokea Middle East mpaka Wafanyabiashara, na viongozi wa nchi nyingi duniani ikiwemo Africa... Yaani waliamua London iwe a Financial Center ya Dunia..... (Je na sisi tukiwaiga walichofanya kwa kuachia kila rasilimali (Commanding Heights) na sisi Dar ni Financial Center..., Ila huenda hata wao walichofanya sio kwamba wamefanikiwa.... arguably naweza kusema wanajuta....

Tunaambiwa kwamba USA wanamikopo zaidi kuliko nchi nyingine yaani bajeti yao ina deficit kubwa (yaani matumizi yao ni makubwa kuliko makusanyo) hilo ni kweli ila tunasahau kwamba hio pesa tunayoitafuta ili tununulie vitu kuanzia madawa mpaka bidhaa zingine ni pesa yao (Dollar) hivyo hata wakiya print ya kutosha bado mtayakusanya na mwisho wa siku kuyarudisha kwao....

Angalizo;
Tubapojibu Hoja tuseme ni nini na kipi kifanyike na kitatufaa vipi sisi kwa mazingira yetu na sio hata fulani anafanya.....
 
Back
Top Bottom