Majibu ya TRA: Nitadaiwa hadi mwisho wa dahari

MfalmewaKiha

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2017
Posts
1,191
Reaction score
1,240
Ndugu zanguni
Salam sio pesa kwamba nisipo kupa hutaishi

Mwaka 2009 Mungu alinipa chombo cha moto, yani pikipiki,, (mtumba) Lakini kwa bahati mbaya Pikipiki hiyo mwishoni mwa mwaka 2011 ikawa na matatizo ya hapa na pale, nikajaribu kutengeneza ila bado ikawa inasumbua,
Mwisho kabisa nikaacha kuitumia iko Store tu.

Kuna msamalia mwema akanishauri niende TRA kuweka zuio la mapato kwa ajili ya manufaa ya baadae.

Nimefika TRA nikawaeleza kwamba Pikipiki kwa sasa haitumiki kwa miaka kadhaa, yani ni km Skrepa tu.

Nikawaomba waiondoe kwenye System ya kulipia. Afisa wa TRA anayehusika amenipa jibu moja, na ktk majibu hayo kuna neno sikulielewa ameniambia hivi ITADAIWA MPAKA MWISHO WA DAHARI. Hivyo akaniomba nilipe tu kwani haina namna.
 
yap kulipa ni lazima kaka ndio sheria Tanzania tulikua tunafanya issue zetu kiholela sana
 
Mbona pikipiki unalipia fire tu kwa sasa, tra hakuna tena makato
 
POLE SANA KWA HILO!LAKINI ILITAKIWA MARA TU BAADA YA KUTOKA BARABARANI BAADA YA BODABODA YAKO KUFA UENDE TRA UKIWA UMEANDIKA BARUA KUMJULISHA MENEJA KUWA KAZI HIYO YA BODABODA IMEKUFA!
 
Mifumo yetu ya kutathimini kodi bado haipo sawa.
 
Jamaa wa TRA Wana Majibu ya shombo kama wazaramo wa pwani.
Yaani jibu unalopewa unajiuliza, Huyu mtu kaokotwa mtaani au alisoma shule??
Mtu kufanya kazi tra anahisi Kama anaishi Humo.
Wanasahau kuwa mtaani tunaishi wote
 
halafu wengine watakuja kusema nanilii ameleta heshima nchini!
 
Wadau kwanza nianze kwa kusikitika.... hii issue ya vyombo vya moto kudaiwa imekuwa inaonekana kama tatizo ambalo linaletwa na uelewa mdogo wa taratibu za namna kumiliki vyombo hvyo: TRA wanajaribu kuandaa vipindi kuhusu hili nami nimejifunza yafuatayo:-
1. Kushindwa kubadilisha umiliki wa vyombo vya moto pindi linapouzwa au kugawiwa kwa mtu mwingine: katika hili sheria inamtaka mnunuzi au muuzaji kubadilisha umiliki ndani ya siku 26.. hili uwe na viambatanisho muhimu kama nakala halisi ya kadi ya gari, copy ya kitambulisho cha muuzaji, mkataba wa mauziano ambao umegongwa muhuli wa mwana sheria, kama ilikuwa gari ya biashara basi awe na statement tokea TRA ambayo itaonesha kulipwa kwa deni la kodi ya mapato.
2. Kama gari ambayo imepatwa na ajali au mbovu haiwezi kutembea tena unapaswa kuwa na taarifa ya polisi kwamba gari hyo haitaingia tena barabarani.. utaandika barua iliyoambatana na taarifa za gari na ukiambatanisha na vehicle inspection report tokea polisi.. utapaswa kulipulia madeni ya kodi yote ya nyuma. Then utaomba gari au pkpk au trailer kuondolewa kwenye mifumo ya TRA.
3. Gari kama imeibiwa utatoa taarifa polisi ukiwa na RB utaandika barua ili gari hyo waiBLOCK kwenye mifumo ya TRA ili kuepusha gari hyo kufanyiwa mabadiliko yoyote kwa upande wa TRA.

MUHIMU: LIPA KODI YAKO KWA WAKATI ILI KUEPUSHA USUMBUFU KAMA HUU... pia toa taarifa kwenue vyombo husika kama chombo chako cha moto kinaleta shida....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…