Uchaguzi 2020 Majimbo waliyopitisha wabunge kibabe kwa kuengua Wapinzani yatapiga kura za hasira dhidi ya Magufuli

Uchaguzi 2020 Majimbo waliyopitisha wabunge kibabe kwa kuengua Wapinzani yatapiga kura za hasira dhidi ya Magufuli

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Wanamikakati ya CCM hawafikirii vizuri. Kitendo cha wao kusuka njama ili kuwaengua wapinzani kwenye majimbo ya ubunge na udiwani ni kitendo kitakochokwenda kumgharimu Magufuli kura za urais.

Wananchi wanatafsiri kuwa kuwanyima choice kwenye ubunge na udiwani kwa kuwalazimishia watu kushinda bila kupingwa ni dharau kwao, ni dhulma dhidi yao na ni kitendo cha kuwanyima haki ya kuchagua na kuchaguliwa kwa mujibu wa katiba yetu ya nchi. Hasira hizi za wananchi zinakwenda kuelekezwa kwa raisi Magufuli kwa kumnyima kura, kwa mujibu wa falsafa ya kama unaninyima mboga basi na mimi Ugali sitoi!

Hii mbinu ya kuengua wapinzani ingewafaa CCM kama kungekuwa na mgombea dhaifu wa Upinzani au kama Upinzani ungekuwa dhaifu. Lakini Lissu ameamsha ari za wananchi, anawapa elimu ya uraia, anawapa hasira wananchi kwenye mikoa ambayo wagombea wengine wa ubunge na madiwani wameenguliwa, kwa hiyo wananchi wanatafsiri kuwa uonevu huu unasababishwa na Magufuli na kwa hiyo watapiga kura za kumkataa.

CCM kama wako Smart, wangeachana na hii biashara ya kukimbilia ushindi wa mezani kwenye ubunge maana itawagharimu sana kura za uraisi.

Logic iko Simple tu, Ukininyima kumchagua mbunge nimtakaye, au na madiwani ninaowataka basi hata huyo rais mnayeomba nimchague naye nitamkataa!.

Lissu ameamsha ari na hasira ya wananchi hasa kule kwenye majimbo ambayo wagombea wa upinzani wameenguliwa kibabe!
 
Mkuu, la msingi ni kuweka mawakala wa uchaguzi wenye kuaminika nchi nzima. Kumbuka NEC wanayo orodha yao ya wapigakura waliojiandikisha zaidi ya 29Mn.

Hapo ni "timing" tu ya kukata kichwa cha kobe endapo atatoa kichwa chake ndani ya gamba lake. Upinzani ni lazima uwe na vituo vingi vya majumuisho ya matokeo ya upigaji kura kutoka kila kituo cha kura kilichopo nchi nzima.

NEC na ZEC ndizo silaha pekee zilizobakia ktk kuchakata na kutoa matokeo ya uongo kwa nafasi za urais. Wanajificha ktk sheria ya matokeo haya kutokutakiwa kuhojiwa kisheria.

Vyama vya ushindani ni lazima vije na Mpango Be (Plan B) na vijiandae kuja na kanuni muhimu ya kuheshimiana, yaani kama mbwai na iwe mbwai.
 
Back
Top Bottom