ni muhimu tuyajua majina. Sababu ya kuyajua na kuyatangaza hadharani ni kutaka kutoa adhabu stahiki. baadhi ya Mhe..R..Mtaafu na heshima kibao, ulinzi na bado kodi zetu zinawalipa pensheni kumbe mijizi kama mingine. Binafsi nina imani watajulika mchan kweupe.
wengine wanafanya money loundering kwa NGOs zao kwa kutuzuga. Adhabu ipatikane hapa hapa duniani
Vilevile juhudi za pamoja( public effort) zifanyike ili pesa zirejeshwe.
Tafadhali usipotosdhe watu, Mh Membe alichosema ni kuwa atawataja wezi wa fedha za radar, siyo hawa wa fedha za miradi ya gas na mafuta zilizoko Uswisi. Kaenda zaidi kwa kusema majina yao yako kwenye public domain, mtu katunga kitabu na kawaweka orodha ya wala rushwa mbali mbali, wakiwemo wa TZ wa radar.
Yaani namsifu aliyeiroga nchi hii tupo anxious kujua majina then tuwachague kuwa wenyeviti wa kamati mbalimbali za bunge kama ilivyo kwa Chenge na wengineo wengi tu mungu atusaidie
Ngoja nijiendee zangu Kifungiro Lushoto,nikichoka huko nitaenda pale Maisara Zenj,hata pale Kenya,Uganda na kwa Kagame napo wapo waliojiwekea vijisenti vyao Uswiswi,sio siri mbona wanajulikana hata mimi nimeweka huko vihela vyangu