Majina ya Wachezaji Hawa Ni Burudani Tosha


Mkuu kulikuwa na Asanga Aswile, Sekilojo Chambua, lipuli iringa kulikuwa na daudi kufakunoga.
 
Naikumbuka Yanga ya miaka ya mwanzo ya themanini, kulikuwa na akina hamis kinye, alan shomari, ahmed amasha, fred felix minziro, lawrence mwalusako, charles boniface mkwasa, isihaka hassan chukwu,idd chama, omary hussein homa ya jiji, abeid mziba miaka ya kati ya themanini wakaja akina aboubakar salum sure boy! Hayo majina kwa kweli yalikuwa yakitajwa rtd mpaka raha. Ila nakumbuka Gor mahia walitutesa miaka ile ya mwanzo kila tukikipiga nao wanatuchapa. Kuna mbongo akiitwa abbas hamis magongo, na lile beki lao bora bob ogora mwee walitutesa
 

yanga hii ilkuwa ni kali, ila wakati naanza kushabikia yanga list ilikuwa ni:
1.Hamis Kinye
2.Yussuf Ismail Bana
3.Ahmed Amasha
4.Athuman Juma chama jogoo
5.Allan Shomari
6.Charles Boniface mkwasa
7.Hussein Idd/Juma kampala
8.Juma Mkambi "jenerali"
9.Makumbi Juma "Bongabonga"
10.Abeid Mziba
11. Omar Hussein "keegan/ saleh Hijja
baadae ndo kikaja kikosi cha mkuu mkirua hapo juu.
Hata hivyo siwezi wasahau kina muhidin cheupe, celestine sikinde mbunga, fred felix minziro, sahau kambi n.k
 
Hivi huyo Morris Nyuchi, alikuwa binadamu gani mwenye nyeti nyingi kihivyo bila kufika Guiness Book of records? Alikuwa anaweza kucheza kweli? Pia umemsahau Malota Soma na mimi Mkereketwa Huyu.
 
majimaji wana lizombe enzi za akina isihaka majaliwa golini, baadaye akaja steven nemes akitokea cda ya dodoma, samli ayoub beki mstaarab, mhando mdeve, peter mhina, octavian mrope(sijaona mido ya aina yake) hamis fande, madaraka selemani, peter tino, ahmed kampira, celestin sikinde mbunga, wakati wa hiki kikosi ni timu mbili tu nilishuhudia zikishinda pale majimaji stadium, simba na pamba. Simba sababu wale wafadhiri wa majimaji akina ahmed bora walikuwa simba damu, ila pamba walikuwa wapo juu kwa kiwango enzi za kina joram mwakatita, fumo felician, na jezi zao nyeupee zimeandikwa pamba kwa thiodan!
 



Shikamoo tena kwa sana tu. Enzi hizi ndiyo tulikuwa na kitu kinaitwa mpira hapa Tanzania. Ila ilipofikia katikati ya miaka ya 90 yaani kile kizazi cha kina Lunyamila na hiki cha bongo fleva ndiyo mpira wetu ukaisha baada ya kuingiliwa na wachezaji wachawi na wababaishaji. Wanaroga wenye vipaji wasicheze ili wapangwe wao na kuhaibisha soka na taifa letu wakituwakilisha popote pale si mchangani au kimataifa. Nasema, wapandishwe kwenye break down na kutumbikizwa bahari ya Hindi wachezaji wote wachawi.
 
Kichochi Lemba,Mnenge Suluja Mnenge,Kaingilila maufi,Bahatisha Ndulute,Daudi Kufakunoga,Kaunda Mwakitope,Moses Mkandawile,Chachage Mluge,Vitus Kimbwilambwiza
 
kenneth Malitoli alikuwa ni mchezaji wa Zambia na mdogo wake Mordon Malitoli. Labda ulikuwa unamaanisha Kenneth Mkapa leftback na team captain wa Yanga kipindi hicho.
Hapana mkuu....Yuko sahihi kabisa.....Kuna kikosi cha Malindi cha mwaka 1994/1995 ambacho kilikuwa kinafadhiliwa na NAUSHAD MOHAMMED....Kikosi hiki kilisajili wachezaji nyota wa nje kama Mordon Malitoli na Alfred Mapataki (Zambia), Julian Albertov (Bulgaria), Edibily Lunyamila, Victor John Bambo, Nico Bambaga, Athanas Michael, Juma Bakari Kidishi , Innocent Haule na wengine.....Malindi ilitisha sana kwenye Kombe la ligi ya Muungano ya mwaka 1995...Hakukuwa na cha Yanga wala Simba, kila timu ilipokea kichapo tu....Kikosi kilikuwa chini ya Super Coach wa Zanzibar enzi hizo Abdulghan Msoma

Timu ilianza kutetereka baada ya NAUSHAD MOHAMED kuitosa
 
ni kweli bwana, nilishasahau kama hawa wazambia walikuja kupiga soka la kulipwa hapa bongo!
 
kenneth Malitoli alikuwa ni mchezaji wa Zambia na mdogo wake Mordon Malitoli. Labda ulikuwa unamaanisha Kenneth Mkapa leftback na team captain wa Yanga kipindi hicho.

Nilikua namaanisha Keneth Malitoli....kuna wakati alichezea Malindi ya Zenji mwaka ule Malindi wamefika semis za Kombe la CAF
 

mimi nachangia majina haya,
mohammed mkandinga,
mohd 'bob' choppa,
faustine kibingwa,
justine simfumkwe,
roster ndunguru,
frank kassanga'bwalya'
ezekiel grayson'jujuman'
john bosco,
mhando mdeve
yassin abu naphiri,
akida makunda na mlage kabange.
 

wengine ni Idd Nassoro "Cheche", Mchunga Bakari "Mandela", Victor Mkanwa, Hanzuruni Hamis, Ladislaus Shawa, Ally Shah, Godes Mjungu na Juma Burhani ( Mkali wa African Sports "wana kimanumanu")
 
Cheche Kaigile. Reli kigoma
Venance Moto. Majimaji songea
Daud Kufakunoga
Kainglila Maufi
Mohamed Digalu. Bandari mtwara
 

Mkuu Balantanda nakukubali. Ila ungetuwekea vilabu vyao hao wachezaji ungebora kumbu kumbu zetu marra dufu!

 
Last edited by a moderator:
Mkuu Balantanda nakukubali. Ila ungetuwekea vilabu vyao hao wachezaji ungebora kumbu kumbu zetu marra dufu!


Ngoja nojaribu mkuu wangu....Kama nimekosea nitarekebishwa na wadau

 
Sidhani ila wanaokumbuka zaidi wanaweza kutujuza manake nakumbuka huyu alikuwa kipa wa pamba ya mwanza enzi hizo....Yawezekana unamchanganya na Lubigisa Lubigisa....

Mkirua nadhani wewe ndiye umewachanganya hawa baba na mwana.
Baba ndiye alikuwa golikipa wa Pamba ya Mwanza na jina lake ni Madata Lubigisa. Mtoto wa Madata Lubigisa aliyechezea Simba alikuwa akiitwa Lubigisa Madata Lubigiss (Lubigisa Lubigisa).

Chilambo Domick alifariki aidha mwishoni mwa miaka ya 80s ama mwanzoni mwa 90s. Nakumbuka Chilambo Domick amefariki wakati Pamba bado iko ligi kuu tena inatisha sana kipindi hicho ndani na nje ya Tanzania.

copy watu8
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…