SEHEMU YA KWANZA.
Kwa wapenda filamu wengi Africa na duniani kote jina la Rambo ni jina maarufu mkombozi wa wanyonge dhidi ya tawala za kibabe za Vietcong ndani ya Vietnam na hata kule Cambodia.
John Rambo ni Askari asie mzaha na mswalie mtume dhidi ya adui zake. Huwasambaratisha adui zake kwa silaha nzito na ndogondogo na Mara nyingine akiteka silaha kutoka kwa maadui zake na kuzitumia hizohizo kuwashambulia na kuwamaliza kikatili.
Haya sasa nimeanza kukumbuka hili la John Rambo nikitumia kama mfano tu wa hadithi ya kweli ninayotaka kukuhadithia kuhusu Rambo halisi wa Ki- Syria kwa jina Meja jenerali Suheil Al Hassan.
Tuendelee.
*******
Wakati wa anguko kuu la serikali ya Syria likiwa wazi katika mwaka 2011 Ni wakati huu ambapo nchi zingine za kiarabu hasa Anti US zilikuwa Tayari zimeangushwa na maandamano makubwa ya kimapinduzi kuanzia kule Libya, Tunisia, Misri, na Yemen.
Syria ya miaka ile ilishachafuka kwa maandamano ya kutisha. Waandamanaji wakidai rushwa imetawala, umaskini umetamalaki na pia swala la kukosekana kwa demokrasia na vifungo juu ya vyombo vya habari na wanahabari . Kwa sababu hizo chache kati ya nyingi miongoni mwa waandamanaji wakaanzisha uasi.
Wakaanza kuiba, kuvunja magereza na kuwatoa wafungwa. Isitoshe wananchi hawa wenye hasira kali wakaanza kuua polisi na wanajeshi watiifu wa rais Dr Bashar Al Assad wakishinikiza Rais Assad atoke madarakani kwa kujiuzulu.
Na kwa kuhofia anguko kama la Ghadafi na Mubarak Dr Assad akaanzisha mashambulizi dhidi ya raia akiwaua kwa silaha za kivita Kama ndegevita na magari yasiyopitisha risasi. Hapo wakauawa makumi na pengine mamia ya waandamanaji. Jambo Hili lilikua ni kosa kuu! Assad alikuwa ameshindwa kujifunza kutokana na makosa ya wenzake akina Ghadafi.
Walichokitaka wamagharibi kilikua kinaelekea kutimia. Mwali wao yaani Assad aliingia tayari kwenye kilengeo cha NATO. Bila kujua alishajichanganya. Lakini pengine si kujichanganya tu kimahesabu lakini ulikuwa tayari ni mkakati wa NATO wa namna ya kumuondoa Rais Assad madarakani. Matumizi makubwa ya nguvu dhidi ya raia yakawa ni kisingizio kipya cha NATO kujiingiza katika Syria kwa namna ya ufadhili wa silaha na fedha kwa vikundi vya kijihadi ili kupambana na Assad.
Humo ndimo yalimoanza kuzaliwa makundi ya kigaidi na kiasi kama FSA ( Free Syrian Army) Alqaida ( Alnusra) na baadae IS na vingine vingi.
Mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2011 Syria yote ilikuwa imekamatwa na waasi na magaidi kasoro vitongoji kadhaa tu jijini Damascus.
Syria Sasa ilikuwa imengia katika full scale war. Vita dhidi ya Waasi na magaidi wanaofadhiliwa na Wamagharibi. Makambi ya kijeshi yalikuwa tayari yameangukia chini ya vikundi vya waasi. Kwa Vita ya ghafla Kama hii dhidi ya wananchi wenye silaha nzito na fedha jeshi la Syria likafeli vibaya kuzuia upinzani huu licha ya kuwa pengine na silaha bora kuliko Waasi. Jeshi liliingia katika mparaganyiko mkubwa yaani hapakuwa na connection nzuri ya utoaji wa amri kijeshi katika kamandi zote za jeshi la Syria yaani ardhini, makini na angani. Walikuwa hawajajiandaa dhidi ya uasi mkubwa hivi.
Syria ikachafuka zaidi mapambano yakapamba Moto huko Allepo,Afrin na kwingineko. Kama ujuavyo waasi na magaidi wapiganapo huja mstari wa mbele kwa morali kali. Hata wakidondoka wenzao mamia kikubwa hua ni kutimiza lengo .
Hapa Askari wenye mioyo laini nao wakaasi wakaamua kulipwa na Marekani. Nani afe kizembe? Wakati ili usiuawe ni vyema kujiunga na waasi?
Sasa basi kwa hofu na spidi kubwa makamanda wa jeshi la Assad wakaasi wakaanza kupigana dhidi ya Assad na serikali yake. Mfano wa kambi za jimbo la mpakani na Uturuki yaani Afrin ziliasi na kuwa kambi kuu za uasi na pia zikipata msaada wa hali na mali kutoka Uturuki. Wakapata anti- tank rocket, wakapata vyakula na hata inteligensia.
Pigo lililoje kwa Assad na serikali yake? Makamanda walioapa kuilinda Syria na Rais Assad wamemsaliti? Askari watiifu wakauawa kikatili kwa mamia ya makundi kwa risasi za waasi. Katika siku fulani mwishoni mwa mwaka 2011 askarijeshi watiifu kwa Assad wapatao 250 walipigwa risasi hadharani mjini Allepo na waasi waungwao mkono na Uturuki. Happ Allepo ndipo palipokua ngome kuu ya waasi na uasi dhidi ya Assad. Hilo la mauaji lilifanywa kwa makusudi kama kitisho kumuonesha Assad na jeshi lake kwamba wakijitia uhayawani kupigana watakwisha.
Kwa hali ile nani angebaki mtiifu kwa serikali iliyoitwa ya kidikteta? Hakuna! Hata hivyo Askari wengine walishaiva vilivyo. Syria ilikuwa na itakuwa kwao daima. Wakaamua kupigana kiume na kufia huko! Miongoni mwao askari hawa kulikua na mwamba mmoja mfupi si mfupi mrefu si mrefu wa saizi ya kati. Alipenda kujiita na hupenda kuitwa " "Al Nimri" ama kwa kipare "Tiger". Huyo jina lake kabisa aliitwa Colonel Suheil Salman Al Hassan. Ni nani huyu Suheil Al Hassan kivita. Ukurasa ujao tutamchimba kiundani zaidi.
ITAENDELEA...
Kwa wapenda filamu wengi Africa na duniani kote jina la Rambo ni jina maarufu mkombozi wa wanyonge dhidi ya tawala za kibabe za Vietcong ndani ya Vietnam na hata kule Cambodia.
John Rambo ni Askari asie mzaha na mswalie mtume dhidi ya adui zake. Huwasambaratisha adui zake kwa silaha nzito na ndogondogo na Mara nyingine akiteka silaha kutoka kwa maadui zake na kuzitumia hizohizo kuwashambulia na kuwamaliza kikatili.
Haya sasa nimeanza kukumbuka hili la John Rambo nikitumia kama mfano tu wa hadithi ya kweli ninayotaka kukuhadithia kuhusu Rambo halisi wa Ki- Syria kwa jina Meja jenerali Suheil Al Hassan.
Tuendelee.
*******
Wakati wa anguko kuu la serikali ya Syria likiwa wazi katika mwaka 2011 Ni wakati huu ambapo nchi zingine za kiarabu hasa Anti US zilikuwa Tayari zimeangushwa na maandamano makubwa ya kimapinduzi kuanzia kule Libya, Tunisia, Misri, na Yemen.
Syria ya miaka ile ilishachafuka kwa maandamano ya kutisha. Waandamanaji wakidai rushwa imetawala, umaskini umetamalaki na pia swala la kukosekana kwa demokrasia na vifungo juu ya vyombo vya habari na wanahabari . Kwa sababu hizo chache kati ya nyingi miongoni mwa waandamanaji wakaanzisha uasi.
Wakaanza kuiba, kuvunja magereza na kuwatoa wafungwa. Isitoshe wananchi hawa wenye hasira kali wakaanza kuua polisi na wanajeshi watiifu wa rais Dr Bashar Al Assad wakishinikiza Rais Assad atoke madarakani kwa kujiuzulu.
Na kwa kuhofia anguko kama la Ghadafi na Mubarak Dr Assad akaanzisha mashambulizi dhidi ya raia akiwaua kwa silaha za kivita Kama ndegevita na magari yasiyopitisha risasi. Hapo wakauawa makumi na pengine mamia ya waandamanaji. Jambo Hili lilikua ni kosa kuu! Assad alikuwa ameshindwa kujifunza kutokana na makosa ya wenzake akina Ghadafi.
Walichokitaka wamagharibi kilikua kinaelekea kutimia. Mwali wao yaani Assad aliingia tayari kwenye kilengeo cha NATO. Bila kujua alishajichanganya. Lakini pengine si kujichanganya tu kimahesabu lakini ulikuwa tayari ni mkakati wa NATO wa namna ya kumuondoa Rais Assad madarakani. Matumizi makubwa ya nguvu dhidi ya raia yakawa ni kisingizio kipya cha NATO kujiingiza katika Syria kwa namna ya ufadhili wa silaha na fedha kwa vikundi vya kijihadi ili kupambana na Assad.
Humo ndimo yalimoanza kuzaliwa makundi ya kigaidi na kiasi kama FSA ( Free Syrian Army) Alqaida ( Alnusra) na baadae IS na vingine vingi.
Mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2011 Syria yote ilikuwa imekamatwa na waasi na magaidi kasoro vitongoji kadhaa tu jijini Damascus.
Syria Sasa ilikuwa imengia katika full scale war. Vita dhidi ya Waasi na magaidi wanaofadhiliwa na Wamagharibi. Makambi ya kijeshi yalikuwa tayari yameangukia chini ya vikundi vya waasi. Kwa Vita ya ghafla Kama hii dhidi ya wananchi wenye silaha nzito na fedha jeshi la Syria likafeli vibaya kuzuia upinzani huu licha ya kuwa pengine na silaha bora kuliko Waasi. Jeshi liliingia katika mparaganyiko mkubwa yaani hapakuwa na connection nzuri ya utoaji wa amri kijeshi katika kamandi zote za jeshi la Syria yaani ardhini, makini na angani. Walikuwa hawajajiandaa dhidi ya uasi mkubwa hivi.
Syria ikachafuka zaidi mapambano yakapamba Moto huko Allepo,Afrin na kwingineko. Kama ujuavyo waasi na magaidi wapiganapo huja mstari wa mbele kwa morali kali. Hata wakidondoka wenzao mamia kikubwa hua ni kutimiza lengo .
Hapa Askari wenye mioyo laini nao wakaasi wakaamua kulipwa na Marekani. Nani afe kizembe? Wakati ili usiuawe ni vyema kujiunga na waasi?
Sasa basi kwa hofu na spidi kubwa makamanda wa jeshi la Assad wakaasi wakaanza kupigana dhidi ya Assad na serikali yake. Mfano wa kambi za jimbo la mpakani na Uturuki yaani Afrin ziliasi na kuwa kambi kuu za uasi na pia zikipata msaada wa hali na mali kutoka Uturuki. Wakapata anti- tank rocket, wakapata vyakula na hata inteligensia.
Pigo lililoje kwa Assad na serikali yake? Makamanda walioapa kuilinda Syria na Rais Assad wamemsaliti? Askari watiifu wakauawa kikatili kwa mamia ya makundi kwa risasi za waasi. Katika siku fulani mwishoni mwa mwaka 2011 askarijeshi watiifu kwa Assad wapatao 250 walipigwa risasi hadharani mjini Allepo na waasi waungwao mkono na Uturuki. Happ Allepo ndipo palipokua ngome kuu ya waasi na uasi dhidi ya Assad. Hilo la mauaji lilifanywa kwa makusudi kama kitisho kumuonesha Assad na jeshi lake kwamba wakijitia uhayawani kupigana watakwisha.
Kwa hali ile nani angebaki mtiifu kwa serikali iliyoitwa ya kidikteta? Hakuna! Hata hivyo Askari wengine walishaiva vilivyo. Syria ilikuwa na itakuwa kwao daima. Wakaamua kupigana kiume na kufia huko! Miongoni mwao askari hawa kulikua na mwamba mmoja mfupi si mfupi mrefu si mrefu wa saizi ya kati. Alipenda kujiita na hupenda kuitwa " "Al Nimri" ama kwa kipare "Tiger". Huyo jina lake kabisa aliitwa Colonel Suheil Salman Al Hassan. Ni nani huyu Suheil Al Hassan kivita. Ukurasa ujao tutamchimba kiundani zaidi.
ITAENDELEA...