Majuha mengine haya hapa, ndiyo maana tunaibiwa

Majuha mengine haya hapa, ndiyo maana tunaibiwa

Retired

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2016
Posts
44,629
Reaction score
83,056
sikiliza hii



===

Wakati mamlaka nchini Kenya zikiendelea kutambua makaburi waliozikwa waumini wa Mchungaji, Paul Mackenzie, Mkuu wa Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, Paulo Chacha ameibaini kuwepo kwa kanisa linaloendesha ibada tata.

Chacha amebaini kuwepo kanisa hilo juzi Juni 8, 2023 katika Kijiji cha Nyamayinza Kata ya Gulumungu wilayani humo ambapo amesema kanisa hilo linamilikiwa na William Masuma na mkewe, Kabula Lushika ambao wanawatoza wagonjwa Sh30, 000 kabla ya kuwafanyia maombi hayo.

Amesema wamebaini kuwepo wagonjwa zaidi ya 200 waliolazwa huku zaidi ya 50 walio taabani wakiendelea kupatiwa matibabu katika mazingira duni huku akiagiza Jeshi la Polisi kufanya chunguzi ili kubaini iwapo kuna wagonjwa waliofariki na kuzikwa eneo hilo kinyemela sambamba na kusitisha huduma za kanisa hilo.

Hata hivyo akizungumza chini ya ulinzi wa Polisi, Mhubiri Masuma amesema pamoia na kuwa na kibali cha kutoa huduma ya Tiba Asili, katika eneo hilo anatoa huduma ya maombezi kwa wagonjwa pekee huku akisisitiza kuwa hakuna mgoniwa ambaye amezuiwa kwenda hospitalini.

Chanzo: Mwananchi
 
sikiliza hii

View attachment 2651592

===

Wakati mamlaka nchini Kenya zikiendelea kutambua makaburi waliozikwa waumini wa Mchungaji, Paul Mackenzie, Mkuu wa Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, Paulo Chacha ameibaini kuwepo kwa kanisa linaloendesha ibada tata.

Chacha amebaini kuwepo kanisa hilo juzi Juni 8, 2023 katika Kijiji cha Nyamayinza Kata ya Gulumungu wilayani humo ambapo amesema kanisa hilo linamilikiwa na William Masuma na mkewe, Kabula Lushika ambao wanawatoza wagonjwa Sh30, 000 kabla ya kuwafanyia maombi hayo.

Amesema wamebaini kuwepo wagonjwa zaidi ya 200 waliolazwa huku zaidi ya 50 walio taabani wakiendelea kupatiwa matibabu katika mazingira duni huku akiagiza Jeshi la Polisi kufanya chunguzi ili kubaini iwapo kuna wagonjwa waliofariki na kuzikwa eneo hilo kinyemela sambamba na kusitisha huduma za kanisa hilo.

Hata hivyo akizungumza chini ya ulinzi wa Polisi, Mhubiri Masuma amesema pamoia na kuwa na kibali cha kutoa huduma ya Tiba Asili, katika eneo hilo anatoa huduma ya maombezi kwa wagonjwa pekee huku akisisitiza kuwa hakuna mgoniwa ambaye amezuiwa kwenda hospitalini.

Chanzo: Mwananchi
Makanisa yote mbona yanafanya hivyo kuanzia yule wa kawe hadi sijui nani. Ndio maana nasemaga zumaridi walwonea maana hana tofauti na wengine
 
Back
Top Bottom