Makaburi ya Kisutu yamebeba kumbukumbu kubwa ya wapigania uhuru wa Tanganyika

Makaburi ya Kisutu yamebeba kumbukumbu kubwa ya wapigania uhuru wa Tanganyika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Leo asubuhi katika matembezi yangu Maktaba nimekuta picha ya kaburi la Sheikh Haydar Mwinyimvua (1905 - 1987) ambae mwanae Sheikh Ahmed Haydar tumemzika siku chache zilizopita.

Picha hii nilipiga mwaka wa 2017 siku ya maziko ya Kleist Abdul Sykes (1950 - 2017).

Tulikuwa tumemaliza kuzika na watu wachache tukabakia nyuma kufanya dua za ziada na nakumbuka aliyetuongoza kwenye dua ile alikuwa Sheikh Abdallah Awadh.

Tulipomaliza kusoma Adam Haydar mdogo wake Sheikh Ahmed Haydar akanivuta akanambia, ''Mohamed njoo tumsomee dua Mzee Haydar huyu hapa.''

Nyuma tu ya kaburi la Kleist ambae alikuwa kazikwa jirani na baba yake, lilikuwa kaburi la Sheikh Haydar Mwinyimvua.

Marehemu hawa wote wawili wawili walipigania uhuru wa Tanganyika na wameacha historia kubwa.
 
Angalia picha:
Screenshot_20210124-221038.jpg
Screenshot_20210124-221109.jpg
 
Mohammed mbali na hekima ninayoiona kwenye majibu yako hata kama swali lilikuwa la kipuuzi tu,wewe hadi hapa tulipo wewe ni kiongozi tena cha mwalimu.
 
Nnangale,
Ahsante.
Mzee Mohamed nilisoma UDsm pale kuna walimu wachache sana nikiwapenda miongoni Mwao ni
Shvji
Chachage
Haroub othmani
Kutaka wachache.
Nilisoma gazeti la rai miaka ile kule tulikutana na wandishi wengi ambao kimsingi nawaita walimu wangu nje ya kuta za madarasa. Hao ni kina
Ulimwengu.
Mihangwa
Karugendo
Hilali swed
Kutaja wachache.
Kwa muktadha huu nawe nakuongeza .
Kwako najifunza mengi sana
Allah akuongezee uhai nizidi kuchota maarifa toka kwako
 
Mzee Mohamed nilisoma UDsm pale kuna walimu wachache sana nikiwapenda miongoni Mwao ni
Shvji
Chachage
Haroub othmani
Kutaka wachache.
Nilisoma gazeti la rai miaka ile kule tulikutana na wandishi wengi ambao kimsingi nawaita walimu wangu nje ya kuta za madarasa. Hao ni kina
Ulimwengu.
Mihangwa
Karugendo
Hilali swed
Kutaja wachache.
Kwa muktadha huu nawe nakuongeza .
Kwako najifunza mengi sana
Allah akuongezee uhai nizidi kuchota maarifa toka kwako
Kinoa...
Ahsante sana.
 
Mzee Mohamed; dini hairuhusu haya mambo. Kiufasaha zaidi, dini hairuhusu labelling ya makaburi basi tunakosea tu. Tunakumbushana tu.
 
Na Makaburi ya Wangazija pale bibi titi Mohamed opposite naTaasisi ya Elimu ya Watu wazima yamebeba history kubwa pia
 
Dudus,
Sina ujuzi wa hayo kwa hiyo sitasema kitu.
Muft Said,mnara wa saa mbele kwenye eneo LA waz au tuite bustan pembezon mwa samora rodi kuna kabur pale limejengewa marumaru nyeupe ambalo halina maelezo yoyote naomba unijuze tafadhal km unafaham chochote kuhusu hilo.
 
Tuletee history ya HAMZA MWAPACHU nae naskia alipigania uhuru wa Tanganyika na alikuwa msomi mzuri kipindi hicho
 
Leo asubuhi katika matembezi yangu Maktaba nimekuta picha ya kaburi la Sheikh Haydar Mwinyimvua (1905 - 1987) ambae mwanae Sheikh Ahmed Haydar tumemzika siku chache zilizopita.

Picha hii nilipiga mwaka wa 2017 siku ya maziko ya Kleist Abdul Sykes (1950 - 2017).

Tulikuwa tumemaliza kuzika na watu wachache tukabakia nyuma kufanya dua za ziada na nakumbuka aliyetuongoza kwenye dua ile alikuwa Sheikh Abdallah Awadh.

Tulipomaliza kusoma Adam Haydar mdogo wake Sheikh Ahmed Haydar akanivuta akanambia, ''Mohamed njoo tumsomee dua Mzee Haydar huyu hapa.''

Nyuma tu ya kaburi la Kleist ambae alikuwa kazikwa jirani na baba yake, lilikuwa kaburi la Sheikh Haydar Mwinyimvua.

Marehemu hawa wote wawili wawili walipigania uhuru wa Tanganyika na wameacha historia kubwa.
Makaburi tangu hatujapata uhuru wa nchi yetu, mpaka leo bado yana nafasi ya kuzika wafu kweli au kuna mchezo wa kuzika juu ya kabauri la zamani ⁉️
 
Back
Top Bottom