Makadirio ya Kodi TRA kwa biashara zaidi ya moja yakoje?

Nyamtukila

Member
Joined
Dec 9, 2017
Posts
29
Reaction score
5
Mfano, Mtu akiwa na duka la mangi, salon, na mgahawa maeneo tofauti, anapokadiriwa kodi yanaangaliwa mauzo katika biashara zote au kila biashara inakadiriwa kodi kivyake?
 
ukiwa na watoto watatu wanasoma shule tofauti utawalipia ada kwenye shule moja au utaenda kulipa ada kwenye shule zote tatu?acha ujinga jiongeze
 
ukiwa na watoto watatu wanasoma shule tofauti utawalipia ada kwenye shule moja au utaenda kulipa ada kwenye shule zote tatu?acha ujinga jiongeze
Kuuliza sio ujinga, ungemjibu kistaarabu ingekuwa bora zaidi...
 
Kila biashara inakadiriwa kiasi inachoingiza kwa mwaka ila mwisho wa siku inajumuishwa yote na wanakutolea kodi yote unayopaswa kulipa kwa pamoja
 
Unawez kukadiriwa kwa biashara zote minimekadiriwa hivo ili mradi uwe unajua kila biashara yako kwa mwez unapata net profit ya shingap ili unapokadiriwa ujipime mwenyewe kinastahili hicho kiasi au umelaliwa hapo ndo mnaaza malumbano kidgo namaafisa kuwa nikod kubwa bana sina hiyo hela then mpaka mnafikia kias cha kodi ambacho ni nafuu kwako kulingana na profit unayoipata
 
Ukiingia ktk website ya TRA utakuta makadirio kabisa yapo kulingana turnover yako kwa mwaka na vilevile kila mwaka wanatoa TAX TABLE ya namna gani utakadiwa kodi kulingana napato lako unalopata kuanzia shingi 1 mpaka bilioni
 
Ukiwa na turnover ya zaida ya 20m kwa mwaka.unatakiwa uandae hesabu zako mizania financial statement ili uwe unakadiriwa kodi kulingana na net profit uliyoipata ktk mwaka mzima wote uliopita wa biashara baada yakulipa kodi ile net profit ulioipata
 
Ila kama ndo unaanza biashara watakukadiria kodi kulingana na mtaji wako uliowaambia labda nna mtaji wa 4milioni watakuuliza kwa siku utategemea kuuza shingap ukawaambia labda ntauza 15000 wanakuja sasa ktk mwaka unasiku ngap mwaka unasiku365 wao sasa kwasababu hutofanya biashara mwaka mzima kuna siku zingne utapumzika au utakua unamwa au hutokua nawateja ndo wanakisia labda utafanya biashara yaan utauza iyo 15000 kwa siku 310 ndo wanakuja kukokotoa 15000×310=4650000 wakishapata hiyo wanarud sasa ktk muongozo wao wamakadirio mwenye mauzo ya 4600000 anatakiwa alipe kodi kias gani utakiwango pale nakiwango ni 150000 kwaiyo kodi yako utakayoilipa kwa mwaka ni hiyo 150000 na utailipa kwa installment4 yaani 150000÷4=37500 kwaiyo kila installment moja utalipa 37500 napindi utakapo pitisha tarehe ya installemt kulipa utapigwa faini na installament ziko hivi unatakiwa ulipie kabla ya tarehe za mwisho kuisha installent na ziko hivi unatakiwa ulipe ya hizi nistallment 1.istallment pay before 31/3/18.second installment before 30/6/2018 third pay before 30/9/2014 and lastinstallment pay before 31/12/2018 waaasalam watongezea wadau wengne
 
Kwa mantiki hii inabidi kuanza biashara kabla ya kwenda TRA ili ujue halo halisi ya biashara husika.
 
Inakuaje Kama bado hujaanza iyo biashara na hujui utauza sh ngapi kwa siku ?
 
ukiwa na watoto watatu wanasoma shule tofauti utawalipia ada kwenye shule moja au utaenda kulipa ada kwenye shule zote tatu?acha ujinga jiongeze
Majibu kama haya huwa yanatolewa na wafu.Mjibu mwenzio vizuri kwa ustaarabu.Unadhani kama wewe unajua ni wote wanajua? ACHA HIZO.
 
Asante sana mkuu, kwa mchango wako mzuri .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…