Gwappo Mwakatobe
JF-Expert Member
- Nov 22, 2019
- 1,730
- 2,230
Wakati Rais Samia Suluhu Hassan, anatimiza siku 100 akiwa madarakani, ni wazi Watanzania bado wana kiu ya kupata Katiba Mpya.
Na wengi hususan wanasiasa, wamekuwa wakiidai kwa nguvu zote.
Hata hivyo, itakumbukwa wakati Samia anaapishwa kuwa Rais, alisema anajua kuwa miongoni mwa mahitaji ya Watanzania ni Katiba mpya, “lakini wasubiri kwanza.”
Pamoja na kauli njema hiyo ya mama, ni vyema tukatafakari kidogo. Maana kuna watu wana mawazo kwamba tunaweza kutengeneza Katiba vijiweni!
Pia kuna mawazo potofu yanayoendelea kwamba kila mtu ni mtaalamu wa kutengeneza Katiba.
Wengine wanafikiri Katiba ni kama Mahakama na wengine wanafikiri Katiba ndiyo jibu la kila kitu.
Jibu la Rais Samia kuwa tusubiri kwanza, lina maana kubwa na Watanzania wanapaswa kulitafakari kwa kina.
Vinginevyo tutachanganyikiwa hata kabla ya kumaliza kazi yenyewe ya kutengeneza Katiba hiyo.
Na swali la kujiuliza jingine ni je, tunaitaka Katiba ya vivuli au Katiba ya vitu halisi?
Tujiulize, tunaitaka Katiba ya kuwalinda watu fulani, au kukipendelea chama fulani cha siasa au kuipendelea dini fulani?
Ni wazi majibu yatakuwa hapana, bali tunataka Katiba ya wananchi.
Inawezekana leo ninaelekea kujadili mada inayochanganya kidogo, wakati Mama yetu ndiyo kwanza ana miezi mitatu tu na siku 10 madarakani.
Lakini ili kuijadili vizuri mada hii, nitamtumia mwanafalsafa Plato, aliyeona kwa mara ya kwanza ukweli juu ya vivuli na vitu halisi.
Plato ndiye mwanafalsafa aliyeanzisha Astria ya Pango. Asria hii ndiyo iliyoendelea hadi kuonyesha ukweli kwamba kuna vitu vinavyodumu na vile vinavyopita. Kwamba vingine ni vivuli na vingine ni vitu halisi, ukweli na vitu visivyobadilika milele yote. Mfano, upendo ni kitu kinachodumu milele yote.
Watu wanaopendana wanakuja na kupita, lakini upendo upo palepale. Au ubaya. Watu wanatenda ubaya na kushiriki ubaya wanakuja na kupita, lakini ubaya unabaki palepale. Hata kama tungefanikiwa kuwamaliza wabaya wote, ubaya utabaki katika wazo la ubaya, na endapo atachipuka tena mtu mbaya, atashiriki ubaya katika wazo la ubaya!
Hii astaria ya pango ilimfikisha Plato, katika hatua ya nadharia ya mawazo. Hii inajulikana kama nadharia ya Plato ya Mawazo.
Kwa ujumla, nadharia ya mawazo ni ule ukweli ambao haubadiliki au una hali ya umilele na haina hali ya umaada ambapo vitu vyote vijavyo kwetu katika hali ya umaada huja kama vivuli vyake.
Kulingana na Plato, ni elimu pekee yake ambayo inaweza kuwatoa hawa watu kutoka kwenye maisha ya kivuli kwenda kwenye ulimwengu wa mwanga.
Elimu kadiri ya Plato si tu jambo la kusoma vitabu mbalimbali na kupata shahada, bali ni hali ile inayomfanya mtu awe na uwezo wa kujua ukweli kama ulivyo na kuishi kadiri ya misingi ya hiyo elimu. Kwa kadiri ya Plato, elimu ni lazima imfanye mtu abadilike kutoka kwenye ulimwengu wa kivuli na kwenda kwenye ulimwengu wa mwanga. Na kwamba mtu akishapata mwanga, atakuwa hajapata elimu ya kweli kama hatachukua jukumu la kuwafundisha wengine.
Kwa maneno mengine, mtu mwenye elimu ya kweli ni yule anayeipata elimu akatoa elimu. Mtu anayeipata elimu akabaki nayo anakuwa bado yuko gizani, pangoni!
Mtu, aliyeelimika ni yule anayeshughulika na vitu visivyopita. Ni mtu yule anayeshughulikia heshima, kuliko kushughulikia watu wanaoheshimiana, ni mtu anayeshughulikia upendo kuliko wapendanao, na ni yule anayeshughulikia Utanzania kuliko kuwashughulikia Watanzania!
Si kwamba anawapuuza Watanzania, hapana, ila kwake kitu cha msingi ni Utanzania. Mtu anayetanguliza Utanzania, atawahudumia Watanzania wote bila kuangalia kabila, sura, cheo au hali ya mtu.
Mtu, anayetanguliza Utanzania, atatenda haki wakati wote, atawapenda Watanzania wote na atawahudumia wote. Sote tukishughulika na Utanzania, Tanzania yenye neema inawezekana leo, kesho na keshokutwa. Tanzania yenye neema kwa vizazi vijavyo inawezekana pia! Hivyo ni muhimu kwetu sote kukazana kuisaka elimu, elimu ya kweli ya kutuletea mwanga na kututoa gizani.
Hoja pana ni kwamba, kama tunatengeneza Katiba ya vivuli itadumu muda mfupi na kutokomea kusikojulikana. Lakini kama tunatengeneza Katiba ya vitu halisi; mfano Katiba ya upendo badala ya wapendanao; Katiba ya heshima badala ya wanaoheshimiana; itadumu vizazi na vizazi.
Nina imani Rais Samia anapoendelea na majukumu yake, ataendelea kufikiria namna njema ya kuufufua na kuuendeleza mchakato wa kutafuta Katiba Mpya uliokwama, ili kukata kiu ya Watanzania.
Ni vyema kuwashirikisha watu wote juu ya Katiba. Ni vyema kwamba makundi mbalimbali yakatoa maoni juu ya Katiba. Lakini ni lazima tufike mahali tukubali kwamba si kila mtu anaweza kutengeneza Katiba.
Privatus Karugendo
Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
Na wengi hususan wanasiasa, wamekuwa wakiidai kwa nguvu zote.
Hata hivyo, itakumbukwa wakati Samia anaapishwa kuwa Rais, alisema anajua kuwa miongoni mwa mahitaji ya Watanzania ni Katiba mpya, “lakini wasubiri kwanza.”
Pamoja na kauli njema hiyo ya mama, ni vyema tukatafakari kidogo. Maana kuna watu wana mawazo kwamba tunaweza kutengeneza Katiba vijiweni!
Pia kuna mawazo potofu yanayoendelea kwamba kila mtu ni mtaalamu wa kutengeneza Katiba.
Wengine wanafikiri Katiba ni kama Mahakama na wengine wanafikiri Katiba ndiyo jibu la kila kitu.
Jibu la Rais Samia kuwa tusubiri kwanza, lina maana kubwa na Watanzania wanapaswa kulitafakari kwa kina.
Vinginevyo tutachanganyikiwa hata kabla ya kumaliza kazi yenyewe ya kutengeneza Katiba hiyo.
Na swali la kujiuliza jingine ni je, tunaitaka Katiba ya vivuli au Katiba ya vitu halisi?
Tujiulize, tunaitaka Katiba ya kuwalinda watu fulani, au kukipendelea chama fulani cha siasa au kuipendelea dini fulani?
Ni wazi majibu yatakuwa hapana, bali tunataka Katiba ya wananchi.
Inawezekana leo ninaelekea kujadili mada inayochanganya kidogo, wakati Mama yetu ndiyo kwanza ana miezi mitatu tu na siku 10 madarakani.
Lakini ili kuijadili vizuri mada hii, nitamtumia mwanafalsafa Plato, aliyeona kwa mara ya kwanza ukweli juu ya vivuli na vitu halisi.
Plato ndiye mwanafalsafa aliyeanzisha Astria ya Pango. Asria hii ndiyo iliyoendelea hadi kuonyesha ukweli kwamba kuna vitu vinavyodumu na vile vinavyopita. Kwamba vingine ni vivuli na vingine ni vitu halisi, ukweli na vitu visivyobadilika milele yote. Mfano, upendo ni kitu kinachodumu milele yote.
Watu wanaopendana wanakuja na kupita, lakini upendo upo palepale. Au ubaya. Watu wanatenda ubaya na kushiriki ubaya wanakuja na kupita, lakini ubaya unabaki palepale. Hata kama tungefanikiwa kuwamaliza wabaya wote, ubaya utabaki katika wazo la ubaya, na endapo atachipuka tena mtu mbaya, atashiriki ubaya katika wazo la ubaya!
Hii astaria ya pango ilimfikisha Plato, katika hatua ya nadharia ya mawazo. Hii inajulikana kama nadharia ya Plato ya Mawazo.
Kwa ujumla, nadharia ya mawazo ni ule ukweli ambao haubadiliki au una hali ya umilele na haina hali ya umaada ambapo vitu vyote vijavyo kwetu katika hali ya umaada huja kama vivuli vyake.
Kulingana na Plato, ni elimu pekee yake ambayo inaweza kuwatoa hawa watu kutoka kwenye maisha ya kivuli kwenda kwenye ulimwengu wa mwanga.
Elimu kadiri ya Plato si tu jambo la kusoma vitabu mbalimbali na kupata shahada, bali ni hali ile inayomfanya mtu awe na uwezo wa kujua ukweli kama ulivyo na kuishi kadiri ya misingi ya hiyo elimu. Kwa kadiri ya Plato, elimu ni lazima imfanye mtu abadilike kutoka kwenye ulimwengu wa kivuli na kwenda kwenye ulimwengu wa mwanga. Na kwamba mtu akishapata mwanga, atakuwa hajapata elimu ya kweli kama hatachukua jukumu la kuwafundisha wengine.
Kwa maneno mengine, mtu mwenye elimu ya kweli ni yule anayeipata elimu akatoa elimu. Mtu anayeipata elimu akabaki nayo anakuwa bado yuko gizani, pangoni!
Mtu, aliyeelimika ni yule anayeshughulika na vitu visivyopita. Ni mtu yule anayeshughulikia heshima, kuliko kushughulikia watu wanaoheshimiana, ni mtu anayeshughulikia upendo kuliko wapendanao, na ni yule anayeshughulikia Utanzania kuliko kuwashughulikia Watanzania!
Si kwamba anawapuuza Watanzania, hapana, ila kwake kitu cha msingi ni Utanzania. Mtu anayetanguliza Utanzania, atawahudumia Watanzania wote bila kuangalia kabila, sura, cheo au hali ya mtu.
Mtu, anayetanguliza Utanzania, atatenda haki wakati wote, atawapenda Watanzania wote na atawahudumia wote. Sote tukishughulika na Utanzania, Tanzania yenye neema inawezekana leo, kesho na keshokutwa. Tanzania yenye neema kwa vizazi vijavyo inawezekana pia! Hivyo ni muhimu kwetu sote kukazana kuisaka elimu, elimu ya kweli ya kutuletea mwanga na kututoa gizani.
Hoja pana ni kwamba, kama tunatengeneza Katiba ya vivuli itadumu muda mfupi na kutokomea kusikojulikana. Lakini kama tunatengeneza Katiba ya vitu halisi; mfano Katiba ya upendo badala ya wapendanao; Katiba ya heshima badala ya wanaoheshimiana; itadumu vizazi na vizazi.
Nina imani Rais Samia anapoendelea na majukumu yake, ataendelea kufikiria namna njema ya kuufufua na kuuendeleza mchakato wa kutafuta Katiba Mpya uliokwama, ili kukata kiu ya Watanzania.
Ni vyema kuwashirikisha watu wote juu ya Katiba. Ni vyema kwamba makundi mbalimbali yakatoa maoni juu ya Katiba. Lakini ni lazima tufike mahali tukubali kwamba si kila mtu anaweza kutengeneza Katiba.
Privatus Karugendo
Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app