Makamba: Mjadala wa EPA ufungwe

Hofstede

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2007
Posts
3,577
Reaction score
1,109
Katibu mkuu wa CCM bwana Yusuph Makamba amedai Mjadala wa EPA ufungwe kwa kuwa watuhumiwa wote wameshafikishwa mahakamani. Je ni kweli watuhumiwa wa EPA wote wameisha fikishwa mahakamani?

 
Acha baadhi ya Wabunge wa CCM watake huyu jamaa aondolewe kwenye nafasi hiyo. Anaropoka kila kukicha vitu visivyokuwa na kichwa wala miguu. JK inabidi amtafute mtu mwingine katika nafasi hiyo maana kuwepo kwake kunazidi kuiharibia CCM.
 
Huyu Makamba aache kamba zake hapa. Unajua wazee kama hawa upumbavu na ujinga unazidi uwezo wao wa kufikiri. Halafu mtu kama huyu ndio unaambiwa ni mtendaji mkuu wa chama oops! nilisahau kumbe ni mtendaji mkuu wa Chama Cha Majambazi.
 
..wazee kama hawa ndio sababu kubwa nchi haina maendeleo!
 
Makamba akili yake kubwa ni kwa wahindi kuomba pesa za kuendeshea chama na zingine anaweka mfukoni .So msameheni hajui yuko wapi sasa .
 
Tuetegemee kusikia nini kutoka kwa fisadi anayekosa usingizi kwa ndoto kuwa huenda yeye nae ataburuzwa mahakamani kwa tuhuma za EPA?
 
Anataka watu waamini kuwa kuna kitu anaficha, kuna mijitu mijinga kuliko nilivyofikiri.
 
atakuwa amebanwa na haja kubwa.. its one thing that makes people want to hurry things up.. iliwawahi idara husika.. Huyu mzee sijui alisoma wapi.. He's a wasteman.. And the damage that CCM inasuffer by not having a strong CEO itakuwa irreversible.
 
Ushauri kwa wana CCM - kama hakuna mwanaccm mwingine wa kuweza kuwa katibu mkuu basi afadhali kiti kiwe vacant kuliko kuwa na mtu kama huyu!!
 
Hana aibu kuzungumza jambo kama hilo hapo Karatu, Jimbo la Uchaguzi la
Dr. Wilbrod Slaa aliyeibua jambo. Haraka angerekebisha usemi wake.

___________________________________
If the blind lead the blind, both shall fall into the ditch. Matthew 15:14:
 
Swala la Kagoda si linahusiana na CCM wao wenyewe?
Anaomba mjadala ufungwe ili kagoda tusahau lakini wapi mzee utakwenda na maji na wewe.
 
Anataka watu waamini kuwa kuna kitu anaficha, kuna mijitu mijinga kuliko nilivyofikiri.

Kuna watu wengine ukisoma kauli zao au kuwasikiliza, unapata maswali mengi kuliko majibu. Hivi Makamba alifikaje alipofika?

Nina hasira na huyu babu...ngoja niishie hapa...!!! Damn!!!!!
 
I heard he is having a thinking sickness so he fails to think clearly-its crap!!; Amekariri vifungu vya biblia na quran na ndivyo vimemfikisha hapo otherwise its real a crap; sijui kwa nini JK anamshikilia lakini kwa majambaza anafaa sana
 
Mabaka oh sorry Makambakamba ni kikaragosi katumwa na mganga wake aropoke na tusishangae kusikia mengi atakayoendelea kuzungumza. Sasa hoja za CCM hapa ni zipi? Akisema Operesheni Sangara haiendi mbali - hoja yake ni ipi kama kada? Hana kitu ndio maan anarudia ya wenzake. Akapimwe upstairs!!!!!!
 
wana sababu zao za kuwapa watu vilaza madaraka kama hayo.
Hawajiamini kwa sababu ya mapungufu yao,wanajua nini kitatokea kipindi cha uchanguzi
itakapotokea wamemweka mtu strong katika nafasi nyeti halafu baadaye
naye akataka kushindana nao.
 
CCM chini ya Makamba kama katibu mkuu ina kazi nzito 2010. Serikali ya CCM chini ya mawaziri waliopo sasa wanaofanya mikutano ya siri kutumia kodi ya watanzania ili kupanga njama za kihalifu kumuhujumu raia kibiashara kutetea matumbo yao ina ngoma zito machoni mwa wananchi. Kiini cha yote haya ni Rais Bomu. Makamba mpumbavu na mawaziri wasiobebeka, wote ni wateule wa kikwete!!! Jahazi linazama.
 
huyu mzee msimlaumu sana ni kuchanganyikiwa kwani wahusika ndio wanaomhonga lela za kuendeshea hicho chama chake cha majambawazi sasa unafikiri tuhuma zikiwafika atakula wapi si atakufa na njaa lakini sisi twasema tumechoka iliobaki Mgosi wa kaya mbwai ni mbwai tu hapa hakuna cha osie wala nini hatupo lushoto hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…