Pre GE2025 Makamu Mwenyekiti CHADEMA Zanzibar atangaza msimamo wa chama kuelekea Uchaguzi Mkuu

Pre GE2025 Makamu Mwenyekiti CHADEMA Zanzibar atangaza msimamo wa chama kuelekea Uchaguzi Mkuu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar kimesema bila mabadiliko ya sheria na mifumo ya uchaguzi nchini, hakutakuwa na Uchaguzi Mkuu mwaka huu.

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar, Said Mzee Miraji amesema hawatakubali kuwa na sheria mbovu za uchaguzi na haiwezekani wakurugenzi wa halmashauri ambao ni wateule wa rais kuwa ni sehemu ya maofisa wa Tume ya Uchaguzi.

Alisema hayo visiwani Zanzibar jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za chama hicho huko Rahaleo, mjini Zanzibar.

Makamu Mwenyekiti huyo alisema wanapozungumzia mabadiliko ya sheria ili kuwapo wagombea huru kwa nafasi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na wabunge si jambo linalowanufaisha CHADEMA tu bali ni jambo litakalowanufaisha watanzania wote na wapenda demokrasia, hivyo wataendelea kusimamia hoja hiyo.

"Tunataka mgombea wa urais angalau apate asilimia 50 ya kura ndipo atangazwe kuwa mshindi. Haiwezekani mtu anapata chini ya kura ya asilimia 50 anatangazwa kuwa ndiye mshindi. Hii si haki, tunasema mtu huyo hajachaguliwa," alisema.

Miraji alisema wanataka mfumo wa uchaguzi uwezeshe watu wawili walioongoza kupata kura nyingi, uchaguzi urudiwe ili kupata mshindi stahiki.

Alisema wako tayari Uchaguzi Mkuu usogezwe mbele ili sheria ya uchaguzi ifanyiwe marekebisho na kuwa na uchaguzi huru na haki.

1738316104536.png

 
Nyumbu kweli ni zero brain, hakutakuwa na uchaguzi? Chadema hawajitambui, waseme hawatashiriki hawawezi kuzuia uchaguzi kufanyika. Ni aibu mtu mzima anatoa hoja km mtoto mdogo
 
Nyumbu kweli ni zero brain, hakutakuwa na uchaguzi? Chadema hawajitambui, waseme hawatashiriki hawawezi kuzuia uchaguzi kufanyika. Ni aibu mtu mzima anatoa hoja km mtoto mdogo
Umemwelewa mtoa maada au umekurupuka tu mkuu! Uchaguzi gani unaouzungumzia kwa katiba hii au nyingine kama katiba yenyewe ndo hii huo uchaguzi ni wengi tu hatuutaki maana hakuna maana ya uchaguzi ikiwa wagombea hao hao wasimamizi wa uchaguzi! Ni kuwafanya watanzania wajinga! Hiyo sio ajenda ya chadema ni ajenda ya watanzania wote ilikuwa tu imekosa kiongozi! Usilete uchawa kwenye mambo ya msingi
 
Umemwelewa mtoa maada au umekurupuka tu mkuu! Uchaguzi gani unaouzungumzia kwa katiba hii au nyingine kama katiba yenyewe ndo hii huo uchaguzi ni wengi tu hatuutaki maana hakuna maana ya uchaguzi ikiwa wagombea hao hao wasimamizi wa uchaguzi! Ni kuwafanya watanzania wajinga! Hiyo sio ajenda ya chadema ni ajenda ya watanzania wote ilikuwa tu imekosa kiongozi! Usilete uchawa kwenye mambo ya msingi
Umemwelewa mtoa maada au umekurupuka tu mkuu! Uchaguzi gani unaouzungumzia kwa katiba hii au nyingine kama katiba yenyewe ndo hii huo uchaguzi ni wengi tu hatuutaki maana hakuna maana ya uchaguzi ikiwa wagombea hao hao wasimamizi wa uchaguzi! Ni kuwafanya watanzania wajinga! Hiyo sio ajenda ya chadema ni ajenda ya watanzania wote ilikuwa tu imekosa kiongozi! Usilete uchawa kwenye mambo ya msingi
Huyo ni UWT anawaza viti maalumu pekee
 
Umemwelewa mtoa maada au umekurupuka tu mkuu! Uchaguzi gani unaouzungumzia kwa katiba hii au nyingine kama katiba yenyewe ndo hii huo uchaguzi ni wengi tu hatuutaki maana hakuna maana ya uchaguzi ikiwa wagombea hao hao wasimamizi wa uchaguzi! Ni kuwafanya watanzania wajinga! Hiyo sio ajenda ya chadema ni ajenda ya watanzania wote ilikuwa tu imekosa kiongozi! Usilete uchawa kwenye mambo ya msingi
SEMA WEWE PEKEYAKO NDIYO HUUTAKI UNAZUNGUMZIA WENGI NA NANI? MIMI MBONA NAUTAKA? USITUSEMEE SEMA WEWE PEKEYAKO
 
Back
Top Bottom