Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,509
- 3,756
MAREKANI: Makamu Rais wa zamani wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Dunia(FIFA), Juan Angel Napout amehukumiwa kifungo cha miaka 9 jela baada ya kukutwa na hatia ya kosa la kupokea rushwa
Katika uchunguzi uliofanywa ndani ya chombo hicho kikubwa cha soka duniani, Juan alipatikana na hatia ya kuchukua mamilioni ya dola kwa njia ya rushwa
Hatua hii inakuja siku chache baada ya kifungo cha miaka minne alichopewa Mkuu wa zamani wa soka Brazil, Jose Maria Marin ambaye pia alihusishwa kwenye tuhuma hizo hizo
Wote kwa pamoja walikutwa na hatia ya kupokea rushwa kutoka kwa Kampuni kubwa ambazo zilikuwa zikijitangaza kupitia FIFA
Sent using Jamii Forums mobile app
Katika uchunguzi uliofanywa ndani ya chombo hicho kikubwa cha soka duniani, Juan alipatikana na hatia ya kuchukua mamilioni ya dola kwa njia ya rushwa
Hatua hii inakuja siku chache baada ya kifungo cha miaka minne alichopewa Mkuu wa zamani wa soka Brazil, Jose Maria Marin ambaye pia alihusishwa kwenye tuhuma hizo hizo
Wote kwa pamoja walikutwa na hatia ya kupokea rushwa kutoka kwa Kampuni kubwa ambazo zilikuwa zikijitangaza kupitia FIFA
Sent using Jamii Forums mobile app