Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wanaweza kumwambia Rais ukweli pale anapotoa maamuzi yasiyo sahihi?

Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wanaweza kumwambia Rais ukweli pale anapotoa maamuzi yasiyo sahihi?

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Rais Samia alikuwa Makamu wa Rais na Majaliwa alikuwa Waziri Mkuu chini ya utawala wa Hayati Magufuli. Wakati huo mengi yalifanyika na hakuna siku wawili hawa waliwahi kupinga.

Baada ya Rais Samia kuingia amepingana kwa kiasi kikubwa na mtangulizi wake. Amepingana naye kuhusu uwepo wa mikutano ya adhara, amewarejesha kazini wale waliotumbuliwa kwa Kashafa nzito, amekiri uwepo wa COVID miaka ya nyuma nk.

Haya yote aliyofanya hakuna siku wakati wa Utawala wa Magufuli tuliwahi kusikia amepinga na hivyo kupelekea Magufuli kutenda kinyume na washauri wake.

Nikalinganisha JPM na Samia naamini wasaidizi wa Samia wamekaa kimya wakisubiri atoke madarakani wamkosoe. Matokeo yake badala ya kuendelea pale mtangulizi alipofika tunatumia muda mwingi kurekebisha mapungufu yake.

Je, kama Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wanashindwa kushauri vizuri kwanini wapo? Kama Rais ndiye kila kitu kwanini tunatumia gharama kubwa kumwekea Makamu na Waziri Mkuu?

Je, Rais Samia kuendelea na wasaidizi wanaosema yes kwenye kila jambo kuna afya kwa Taifa? Kuwa na wasaidizi ambao moyoni wanawaza tofauti na wanavyokushauri kuna tija?

Nadhani kama kuna Sehemu Rais Samia anakosea wasaidizi wake wamweleze sasa siyo kusubiri astaafu waanze kumkosoa kivitendo. Viongozi wakiwa wakweli na kukubali hata kujiuzulu pale ushauri wao unapokataliwa tutalisaidia sana Taifa letu.

Tumemwingiza chaka mama kwenye kikokotoo, mikopo ya asilimia 10, tumemshauri vibaya akawatumbua wasio na hatia tukijua , tumemshauri na kumpa taarifa za uongo kuhusu tozo, tumemdanganya kuhusu umuhimu wa Chawa kwenye maendeleo nk

Je, tunasubiri lini tumshauri ipasavyo? Tufanye sasa na Mwenyenzi Mungu atatubariki kwa vingi zaidi. Mama ni msikivu atatusikiliza tusiwe Chawa.
 
Kumwambia bosi ukweli au kumshauri haina maana kwamba anakubaliana nawe na kwamba atafuata ushauri wako.
 
Katiba (kakitabu tu) imempa nguvu kubwa sana Rais, anaweza kupokea ushauri kutoka kwa washauri wake ila ana hiyari ya kupokea au kutupilia mbali ushauri anaopewa. Sasa jiulize kwani yeye hana akili hadi akubali kupokea ushauri wa ovyo?
 
Upinzani bungeni husaidia kushape Serikali, sasa hamna upinzani.
 
Serikali ya CCM sio kama CHADEMA ambao wanapingana mitandaoni na kutukanana wenyewe. Viongozi hushauriana na kukosoana kwenye vikao rasmi na sio hadharani. Wakitoka nje ya kikao mbele ya wananchi huwa kitu kimoja.
 
Serikali ya CCM sio kama CHADEMA ambao wanapingana mitandaoni na kutukanana wenyewe. Viongozi hushauriana na kukosoana kwenye vikao rasmi na sio hadharani. Wakitoka nje ya kikao mbele ya wananchi huwa kitu kimoja.
Si Kweli,

Wangekuwa wanashauriana na Kuambiana Kweli,

Wangeacha kuiba kura.
 
Serikali ya CCM sio kama CHADEMA ambao wanapingana mitandaoni na kutukanana wenyewe. Viongozi hushauriana na kukosoana kwenye vikao rasmi na sio hadharani. Wakitoka nje ya kikao mbele ya wananchi huwa kitu kimoja.
Madam habari
 
Majibu haya tunayapata hapa kwaa ndugu Pascal Mayalla karibu tafadhali
Asante sana kuni tag.
Rais Samia alikuwa Makamu wa Rais na Majaliwa alikuwa Waziri Mkuu chini ya utawala wa Hayati Magufuli. Wakati huo mengi yalifanyika na hakuna siku wawili hawa waliwahi kupinga.

Baada ya Rais Samia kuingia amepingana kwa kiasi kikubwa na mtangulizi wake. Amepingana naye kuhusu uwepo wa mikutano ya adhara, amewarejesha kazini wale waliotumbuliwa kwa Kashafa nzito, amekiri uwepo wa COVID miaka ya nyuma nk.

Je, kama Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wanashindwa kushauri vizuri kwanini wapo? Kama Rais ndiye kila kitu kwanini tunatumia gharama kubwa kumwekea Makamu na Waziri Mkuu?

Nadhani kama kuna Sehemu Rais Samia anakosea wasaidizi wake wamweleze sasa siyo kusubiri astaafu waanze kumkosoa kivitendo. Viongozi wakiwa wakweli na kukubali hata kujiuzulu pale ushauri wao unapokataliwa tutalisaidia sana Taifa letu.

Je, tunasubiri lini tumshauri ipasavyo? Tufanye sasa na Mwenyenzi Mungu atatubariki kwa vingi zaidi. Mama ni msikivu atatusikiliza tusiwe Chawa.
Kwa mujibu wa katiba yetu, rais wa JMT anaruhusiwa kushauriwa na yoyote wakiwemo wasaidizi wake, lakini kwenye kufikia maamuzi, anafikia maamuzi yeye kama yeye, hawajibiki kufuata ushauri wa yeyote!.

Na kufuatia kanuni ya a collective responsibility, ukimshauri chochote rais, huruhusiwi kusema umemshauri nini, ulichomshauri akifuata, credits ni kwa rais, akikataa, ni unanyamaza, kama hukubaliani na ushauri wako, unaachia ngazi.
Hili niliwahi kulizungumza humu, Naamini Rais Magufuli ana washauri wazuri na anashauriwa vizuri tuu! , Ila...

Watu ambao wanaweza kumshauri rais na kusema wamemshauri nini ni wananchi na sisi media, ambao ni mhimili wa nne usio rasmi, na ukimshauri jambo, asipofuata ushauri huo, liitokea la kutokea ni unamtundika msalabani!, kama ilivyofanyika nchini Marekani kwenye kashfa ya Watergate, gazeti la Washington Post, lilimshauri kitu rais wa Marekani, akagoma, likamtundika msalabani, Ikulu pakawa pachungu, akabwaga manyanga na kutoka baru!.

Sisi media tumewashauri sana viongozi wetu Wasaidizi wa Rais, Please Msaidieni Rais Wetu Kwenye Public . Msimuachie Kila Kitu Peke Yake! .
P
 
Asante sana kuni tag.

Kwa mujibu wa katiba yetu, rais wa JMT anaruhusiwa kushauriwa na yoyote wakiwemo wasaidizi wake, lakini kwenye kufikia maamuzi, anafikia maamuzi yeye kama yeye, hawajibiki kufuata ushauri wa yeyote!.

Na kufuatia kanuni ya a collective responsibility, ukimshauri chochote rais, huruhusiwi kusema umemshauri nini, ulichomshauri akifuata, credits ni kwa rais, akikataa, ni unanyamaza, kama hukubaliani na ushauri wako, unaachia ngazi.
Hili niliwahi kulizungumza humu, Naamini Rais Magufuli ana washauri wazuri na anashauriwa vizuri tuu! , Ila...

Watu ambao wanaweza kumshauri rais na kusema wamemshauri nini ni wananchi na sisi media, ambao ni mhimili wa nne usio rasmi, na ukimshauri jambo, asipofuata ushauri huo, liitokea la kutokea ni unamtundika msalabani!, kama ilivyofanyika nchini Marekani kwenye kashfa ya Watergate, gazeti la Washington Post, lilimshauri kitu rais wa Marekani, akagoma, likamtundika msalabani, Ikulu pakawa pachungu, akabwaga manyanga na kutoka baru!.

Sisi media tumewashauri sana viongozi wetu Wasaidizi wa Rais, Please Msaidieni Rais Wetu Kwenye Public . Msimuachie Kila Kitu Peke Yake! .
P
Unataka kutuambia tunafeli kwa sababu Marais wanashupaza shingo kupokea ushauri au tunafeli kwa sababu Marais wetu wanapenda kufanya kazi na watu wasioweza kuwashauri sahihi?

Kwanini tunaamini Rais anakataa ushauri na tusiamini kwamba waliopewa dhamana ndio wanaoshindwa kutimiza wajibu?


Tunatokaje hapa? Kwamba kumshauri akakataa basi ujiweke pembeni kuliko kuendelea kutembea na msafara wa magari ukijua ofisini hakuna mchango wako unaopokelewa
 
Je, kama Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wanashindwa kushauri vizuri kwanini wapo? Kama Rais ndiye kila kitu kwanini tunatumia gharama kubwa kumwekea Makamu na Waziri Mkuu?

Je, Rais Samia kuendelea na wasaidizi wanaosema yes kwenye kila jambo kuna afya kwa Taifa? Kuwa na wasaidizi ambao moyoni wanawaza tofauti na wanavyokushauri kuna tija?
Unajua maana ya ushauri? Maana yake ni pendekezo, na ushauri unaweza kukubaliwa au kukataliwa. Walimshauri asimfanye Makonda Katibu Mwenezi wa CCM, kwani alikubali? Aliwakatalia.

Na ukimshauri mtu mara tatu, akakataa au kupuuza ushauri wako, siku nyingine kubaliana tu na kile anachotaka kufanya hata akikuomba ushauri - mwambie wewe huoni tatizo yeye kufanya anachotaka kufanya - hasa kama unaipenda kazi yako. Mara nyingi watu wanaokataa au kupuuza ushauri, mambo yakiharibika wanakuwa na hasira na wale waliowashauri, kwa sababu wanajiona wamefedheheshwa na kuwa exposed kwamba wana tatizo la kufanya maamuzi sahihi.

Kwa hiyo mara nyingine unaweza kutoa ushauri, ushauri wako ukakataliwa au kupuuzwa. Basi unakaa kando unasubiri mwana kuyatafuta mwana kuyapata.

Philosophy hii ina-apply hata kwa Raisi Samia.
 
Back
Top Bottom