Makamu wa Rais Shirikisho la Soka Afrika(CAF), afungiwa Maisha kujihusiha na Soka

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Shirikisho la soka duniani(FIFA) limempa kifungo hicho Makamu wa Rais wa Kwanza wa CAF, Kwesi Nyantakyi ambaye pia ni Rais wa zamani wa Shirikisho la Soka nchini Ghana

Ni baada ya kubainika kupokea rushwa ya Dola za Kimarekani 65,000(Tsh. Milioni 148.85) kutoka kwa Mwanahabari aliyekuwa anafanya uchunguzi kuhusu ufisadi katika mchezo wa soka

Mbali na adhabu hiyo kali pia ametozwa faini ya Franc za Uswisi 500,000(takribani Tsh. Bilioni 1.135)

Nyantakyi, alijiuzulu mwezi Juni baada ya kuonekana kwenye ripoti ya uchunguzi iliyotolewa na Mwanahabari Anas Aremeyaw Anas, akipokea rushwa

Hata hivyo madai hayo aliyakanusha na kufuatia adhabu ya FIFA, haijafahamika iwapo atakata rufaa
 
Siasa za mpira noma sana,ukiwa unaingilia mishe za watu wanakutoa kwenye system faster
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…