Makanisa yafunguliwa DRC baada ya miezi mitano

Makanisa yafunguliwa DRC baada ya miezi mitano

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Huduma za ibada katika makanisa ya nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), zimerejea baada ya takribani miezi mitano iliyopita.
Makanisa hayo yalifungwa kutokana na mlipuko wa virusi vya corona.

Jumapili hii, mamia ya Wakristo nchini humo wamejumuika kwa pamoja katika sala wakiwa na shangwe kubwa.
Makanisa yakiwa na vifaa vya kunawia mikono na vipima joto huku kila mkristo akivalia barakoa.

Huku polisi wakiwa na mavazi ya kiraia wakiwepo katika makanisani kuhakikisha kuwa muongozo wa kujikinga dhidi ya corona unafuatwa.
Aidha ibada hizo zimewagawa waumini kuingia kwa awamu katika ibada ili kupunguza msongamano.

Lakini hatua hii imekuja wakati ambao baadhi ya waangalizi wakihofia kuongezeka zaidi kwa visa vya maambukizi ya corona.
Hata hivyo kwa sasa DRC, imefungua mipaka yake na usafiri wa ndege na gari unaruhusiwa kutoka jimbo moja kwenda jimbo lingine.
 
Tata Nzambe yoka losambo ya Bana Congo tozali na mosala na biso
 
Back
Top Bottom