Makapuku Forum

Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imesema katika mwendelezo wa ukarabati na maboresho ya uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es salaam tayari vimefungwa vifaa vya huduma za mtandao wa kasi wa internet (Free WiFi) ambapo kwa sasa hakutokuwa tena na stress za matatizo ya mtandao ukiwa katika uwanja huo na Mashabiki watapata huduma hiyo bure .
 
Serikali ya Senegal mapema wiki hii imekataa kuondoa marufuku iliyoweka kwa mtandao wa kijamii wa TikTok huku wakiitaka kampuni hiyo itie sahihi makubaliano ambayo yataruhusu kuundwa kwa utaratibu wa Serikali kuondoa akaunti mbalimbali ambazo zitakiuka taratibu za Nchi hiyo.

Waziri wa Mawasilino Moussa Bocar amesema wamejadiliana na TikTok na kwa sasa zuio la mtandao huo litaendelea hadi makubaliano ya kina waliyoyafanya yakamilike.

Senegal ilizuia kupatikana kwa TikTok nchini humo August mwaka huu kufuatia kukamatwa kwa Kiongozi wa Upinzani, Ousmane Sonko akisema mtandao huo utakuwa unatumiwa kusambaza ujumbe wa chuki na upotoshaji ambao ulikuwa unatishia usalama wa Nchi.

Mgogoro wa kuwania madaraka kati ya Sonko, Kiongozi wa Chama cha Pastef, na Rais Macky Sall ulisababisha maandamano ya vurugu mwezi June 2023 na kuharibu sifa ya Senegal kama nchini yenye demokrasia thabiti zaidi Afrika Magharibi.

Wakati wa majadiliano yake na TikTok, Serikali imeiomba udhibiti bora wa mtandao huo na kuuliza maswali kuhusu utendaji kazi wa muundo wake na ulinzi wa taarifa pia imeomba malipo ya haki kwa Watengeneza maudhui ambayo yatawawezesha Vijana kujikimu kimaisha kupitia mitandao ya kijamii.
 
Kijana William Bahati (20) Mkazi wa Kijiji cha Kashero Wilayani Mbogwe Mkoani Geita amefariki Dunia kwa kujinyonga na kamba ya kufungia mbuzi huku sababu zikitajwa kuwa ni kukosekana kwa nauli ya kwenda ukweni kumzika Baba Mkwe wake.

Akiongea kuhusu tukio hilo Mke wa Marehemu, Grace Jeremiah Mkazi wa Kijijini hapo amesema sababu za Mumewe kujinyonga zimetokana na kushindwa kupata nauli ya kwenda ukweni ambako kulikuwa na Msiba wa Mkwewe .

"Mume amejinyonga baada ya kukosa nauli ya kwenda msibani nyumbani kwetu, tulikuwa ndani mida ya saa 11 akawa anasikitika kuwa anaumia kukosa nauli ya kusafiri yeye na Mimi kwenda kumzika Baba, sasa aliamka kitandani akavaa nguo akatoka akasema ngoja niende shambani ndio tukamkuta sasa ameshajinyonga”

Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kashero Alfred Msukuzi amesema tukio hilo limetokea October 2 mwaka huu ambapo amekiri kuwa Kijana huyo amejinyonga kwa kukosa pesa ya kwenda ukweni.
 
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa @innocentbash , amesema Serikali imesikia kilio cha Watumiaji wa barabara kuu ya TANZAM kutokea Ruaha Mbuyuni hususan eneo la Mlima Kitonga lenye urefu wa kilometa 7.6 na inakwenda kutoa suluhisho, ambapo tayari Wataalamu wamewasilisha mapendekezo ya muda mfupi na muda mrefu ambayo yatafanyiwa kazi na Serikali.

Eneo hilo la Mlima Kitonga ambalo limekuwa kero kubwa kwa Watumiaji wa barabara kutokana na kuwepo kwa Mlima mkali na kusababisha foleni kwa muda mrefu pamoja na ajali za magari sasa Serikali inakwenda kuipanua kwa gharama ya Tsh. bilioni 6.478 ikiwa ni makadirio ya utekelezaji wake katika mpango wa muda mfupi.

Bashungwa amesema hayo Mkoani Iringa wakati alipofika eneo hilo na kupata taarifa ya Wataalamu kutoka Wakala wa Barabara (TANROADS) baada ya kukamilisha usanifu wa upanuzi wa Mlima Kitonga ili kuimarisha usalama kwa Watumiaji wa barabara hiyo “ Mh. Rais ni Mtu wa vitendo na tayari utekelezaji wa upanuzi utaaanza hivi karibuni”

"Moja ya maagizo aliyonipatia Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni pamoja na kushughulikia kero ya eneo hili la Mlima Kitonga ambalo limekuwa likipoteza ndugu zetu pamoja na mali na ameniagiza kwanza tutafute suluhisho la muda mfupi na nimpelekee suluhisho la muda mrefu"

Kwa upande wake, Meneja wa TANROADS, Mkoa wa Iringa, Yudas Msangi amesema mita 1600 za Mlima Kitonga zitatanuliwa ili kupunguza ajali na foleni katika eneo la Mlima Kitonga barabaea kuu ya TANZAM ikiwa ni suluhisho la muda mfupi na maeneo mengine yatafungwa vioo maalum kwenye maeneo yenye kona kali ili kuwasaidia Madereva kuona magari mengine na kuongeza usalama zaidi.
 
Raia tisa wa Marekani wameripotiwa kuuawa katika vita vinavyoendelea Israel, huku idadi ya vifo ikiripotiwa kuvuka 1,300.

Israel ilishambulia ukanda wa Gaza kwa mashambulizi ya anga leo Jumatatu, wakati ikiendelea kujibu mashambulizi ya kushtukiza ya kundi la wanamgambo wa Palestina Hamas yaliyoanza Jumamosi asubuhi.

Mawaziri wa Israel wameamuru kuzingirwa kabisa kwa Ukanda wa Gaza ambao tayari umezingirwa na kukata usambazaji wa chakula, maji na umeme kwa wakazi wake takriban milioni mbili.

Shambulio la Hamas, ambalo halijawahi kushuhudiwa, ni shambulio kubwa kuwahi kushuhudiwa na Israel katika kipindi cha miaka 50.

Zaidi ya Waisraeli 700 wameuawa katika kile Hamas inachokiita Operesheni ya Mafuriko ya Al Aqsa, huku Wapalestina wasiopungua 560 wakiuawa katika mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Israel kwenye Ukanda wa Gaza.

Zaidi ya raia 100 wa Israel, wanajeshi na raia wa kigeni pia wamechukuliwa mateka na Hamas, jambo ambalo limemfanya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu kutangaza kuwa nchi yake iko vitani.

 
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amewaagiza Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) kutompa kazi nyingine Mkandarasi ambaye hajafikisha asilimia 60 ya kazi za awali ili kuondokana na hali ya kumrundikia kazi za ujenzi Mkandarasi mmoja.

Amesema hayo leo October 09, 2023 wakati akiongea na Wananchi wa Kijini cha Isenyi Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara wakati wa ziara ya ukaguzi, utekelezaji wa miradi inayotekelezwa mkoani Mara.

"Nawaagiza TANROADS, Kama kuna Makandarasi wanaotekeleza Barabara au kazi nyingine ya ujenzi na wako chini ya asilimia 60 ya utekelezaji, msiwape miradi mingine mipya”

Bashungwa @innocentbash amesema hajaridhishwa na utekelezaji wa Barabara ya Sanzate - Nata unaotekelezwa na Kampuni ya China Railway Seven Group wenye urefu wa kilometa 40 ambapo utekelezaji huo unasuasua kwa miaka mitatu kwa sababu ya kurundikiwa kazi nyingi za ujenzi.
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan wa Tanzania na Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi, wamekubaliana kuongeza matumizi ya fedha za Nchi (Shilingi na Rupia) badala ya fedha za kigeni kwenye biashara kati ya Tanzania na India.

Hatua hiyo itapunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya dola za Marekani kwenye Nchi hizo kwasababu kwa sasa (kwa takwimu za India 2022/23) thamani ya biashara ya India na Tanzania imefika dola bilioni 6.7 (zaidi ya shilingi trilioni 14) - ongezeko kubwa kutoka dola bilioni 3.2 mwaka 2021/22 (takwimu za Tanzania).

Waziri Mkuu Modi amesema lengo la hatua hiyo ni kuongeza biashara na kupunguza gharama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…