[emoji187] Kwa sass tunakabiliwa na kazi kubwa ya kumfunga Mcongo halafu Zambia na Morocco watoke sare au Zambia wafungwe. Ni kazi ngumu. Ulazima wa kumfunga Congo ni moja kati ya kazi ngumu katika soka. Wanatuzidi mambo mengi kuanzia uwezo na hadhi ya mchezaji mmoja mmoja hadi kucheza kitimu. Wana timu haswa.
.
Walituonyesha tofauti yao na sisi kwa namna walivyokabiliana na Morocco. Wakati sisi tulikuwa wanyonge wao walionyesha ubora wao. Walichomoa bao na wakataka la ushindi. Na ni mechi ambayo inatia shaka kufikiria namna ambavyo pambano letu na Congo linavyoweza kwenda. Kama Fiston Mayele anaanzia benchi unaweza kufikiria ubora wa timu yao.
.
Vyovyote ilivyo tuanze kufikiria namna ya kushindana katika michuano ijayo. Hadi sasa inaonekana imeanza kuwa rahisi kuja katika michuano hii lakini bado tupo katika uwezo wa ushiriki tu na si ushindani. Tunahitaji kufanya uwekezaji wa kisasa katika soka.“ — Edo Kumwembe.
View attachment 2880502