Makapuku Forum

Hapo ni Korea Kusini mzazi akitoka hospitali haendi kwa bibi..anakwenda wapi unajua...anakwenda kwenye vituo maalum kwa ajili ya kujiuguza.

Wenyewe wanaviita Joriwons..huko mama anakaa siku 21...anapewa huduma zote kama yuko hotelini vile..huko mama atafanyiwa facial, masaji na madarasa ya elimu ya ulezi...watoto wanakuwa nursery chini uangalizi wauguzi, mama anamuona mtoto wake wakati wa kunyonyesha na kama mama hajisikii kumuona mtoto wake basi atamchukua siku anaruhusiwa...

Kwa sasa katika kila wanawake 10 wanaojifungua wanawake 8 huwa wanakwenda kwenye vituo vya namna hiyo....licha ya anasa zote hizo bado wanawake huko Korea hawataki kabisa kuzaa...

Picha ni kwenye mojawapo ya vituo vinavyotoa uangalizi kwa wazazi huko Korea kwenye jiji la Seoul!
 
Musk apandikiza chip kwenye ubongo wa binadamu

Kampuni ya Neuralink inayomilikiwa na tajiri Elon Musk imefanikiwa kupandikiza kwa mara ya kwanza chip kwenye ubongo wa binadamu.

Mwezi wa 5 mwaka jana, Elon Musk alipata kibali kutoka FDA ya Marekani kuanza majaribio ya kifaa hicho kwa binadamu.

Majaribio hayo kwa binadamu yatadumu kwa miaka 6 kabla ya kuidhinishwa kutumika rasmi kwa binadamu iwapo kifaa hicho kinaonyesha mafanikio na kitakuwa salama.

Kampuni ya Neurolink imesema mgonjwa wa kwanza aliyepandikiziwa kifaa hicho kwenye ubongo anaendelea vizuri na chip hiyo imefanya kazi.

Wakati wa upandikizaji wa kifaa hicho Roboti zitakuwa zinatumika kupandikiza nyaya nyembamba kuliko nywele za binadamu kwenye ubongo wa binadamu.

Elon Musk anasema kifaa hicho ni kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa fahamu ikiwemo wagonjwa wenye stroke ambao sasa watakuwa wanaweza kuongea kupitia computer au simu.

Kwa sasa utafiti huo unafanyika kwa watu ambao wamekatika miguu na mikono..!
 
Sasa angalia kwenye kitako cha chupa za maji ya kunywa au juice...kama chombo kina alama hii hicho chombo kinatumika mara moja tu...

Ukiimaliza tupa usikutumie tena kwa kujaza maji au kuweka mafuta ya kula...pia chupa yenye alama hiyo isiwekwe nje kwenye jua au karibu na moto na kama ulikuwa umeyaacha maji yake kwenye gari ni bora kutupa..

Plastiki yenye alama hiyo ikitumika mara kwa mara au kukaa kwenye joto mfano nje kwenye jua au ndani ya gari kemikali za Antimony na Phthalates huwa zinayeyuka na kuingia kwenye maji.

Kemikali zinaweza kusababisha madhara kwa mtumiaji ikiwemo kuvuruga homoni za uzazi...halafu ukienda dukani usichukue maji ambayo yamepigwa na jua....haya share au mtag umpendae na yeye ajifunze na kama una makopo ya hivyo kwenye friji tupa kuanzia leo....!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…