Makapuku Forum

Nimewamic humu ndanii.
DA shuu na DA makiiii.
[emoji8][emoji8][emoji182][emoji182][emoji182]
 
Mamlaka za maafa nchini zimeshauriwa kuendelea kuratibu utekelezaji wa mipango itakayosaidia kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua za masika.

Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imetoa tahadhari ikieleza vipindi vya mvua kubwa vinaweza kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi, hivyo kusababisha uharibifu wa miundombinu, mazingira, upotevu wa mali na maisha.

Kaimu Mkurugenzi wa TMA, Dk Ladislaus Chang’a amesema hayo leo Februari 22, 2024 alipotoa taarifa ya uchambuzi wa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na mwelekeo wa msimu wa mvua za Masika katika kipindi cha Machi hadi Mei, 2024.

TMA imesema kutakuwa na mvua za wastani hadi juu ya wastani kwa msimu wa masika, 2024 katika maeneo mengi ya nchi yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka.

Ongezeko la mvua linatarajiwa Machi.

Dk Chang’a amesema mvua za masika zinatarajiwa kuanza wiki ya nne ya Februari katika maeneo mengi na zinatarajiwa kuisha wiki ya tatu na ya nne ya Mei, 2024 katika maeneo mengi.
 
Meli ya Kampuni binafsi ya Flying Horse imezima ghafla ikiwa safarini kutoka Pemba kwenda Unguja na kusababisha taharuki kwa abiria.

Tukio hilo limetokea leo Fabruari 22, 2024 baada ya Injini moja ya kushoto kupata hitilafu muda mfupi kuanza safari yake

Akizungumza na Mwananchi Digital, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Baharini (ZMA), Sheikha Ahmed Mohamed amesema hitilafu hiyo imetokea dakika chache baada ya kutoka bandari ya Pemba.

“Kwahiyo ilikuwa haijatembea umbali mrefu na kilikuwa na meli zingine tulichofanya Serikali iliamrisha meli hizo ziivute kuirudisha bandarini Pemba bila kuleta madhara yoyote,” amesema

Mkurugenzi huyo, amesema abiria waliokuwa kwenye meli hiyo bila kutaja idadi yao, walihamishiwa kwenye meli nyinginezo zilizokuwa zinakwenda Unguja, Hivyo abiria walifika Salama na kuendelea na shughuli zao

Mmoja wa abiria aliyekuwamo kwenye meli hiyo, Makame Haji amesema meli hiyo ilikuwa haijatumia hata dakika tano, imetoka bandarini na ghafla walisikia ikibadilisha mgurumo na kupunguza mwendo

“Kilichosaidia bado tulikuwa karibu, watu wamepata hofu lakini haikuwa kubwa tulikuwa bado karibu na bandari,”
Ilikuja meli nyingie ikaivuta na kuirudisha kwenye gati tukashuka na kuhamishiwa kwenye meli nyingine tukaanza safari ya kuja Unguja,”

 
OGOPA
.
10 —Mabao ya Mo Salah (19), Diogo Jota (14), Darwin Núñez (13), Cody Gakpo (11) na Luis Díaz (10), yanaifanya LIVERPOOL kuwa timu ya kwanza katika ligi tano bora Ulaya kuwa na wachezaji watano waliofikisha mabao 10 na zaidi katika michuano yote msimu huu.
 
Refa Boubou Traore (34) kutoka Mali [emoji1159] ndiye amepagwa na CAF kushika kipyenga katika mechi ya Yanga na CR Belouizdad ya Algeria zitakapokutana Jumamosi kuanzia Saa 1:00 usiku kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.
.
Traore amechezesha mechi mbili za Belouizdad ambazo ya kwanza ni ile waliyocheza Februari 28, 2021 na Mamelodi Sundowns kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa ambayo timu hiyo kutoka Algeria ilichapwa mabao 5-1.
.
Februari 24, 2023, CR Belouizdad ilipoteza kwa bao 1-0 mbele ya Al Merrikh ya Sudan, huku refa wa mchezo akiwa ni Boubou Traore.

…………..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…