Makapuku Forum

Kisiwa cha Nyasahungu kilichopo ndani ya Ziwa Victoria wilayani Musoma, Mkoa wa Mara kimezama baada ya maji kuongezeka ndani ya ziwa hilo.

Kisiwa hicho kimezama kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha, ingawa hadi sasa hakuna madhara kwa binadamu zaidi ya nyumba za makazi kuzama ziwani.

Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dk Halfan Haule ameyasema hayo leo Jumanne Mei 7, 2024 alipozungumza na Mwananchi Digital kwa simu.

Amesema kaya zaidi ya 20 zimeathiriwa na hali hiyo. Hata hivyo, amesema tayari Serikali imewahamaisha wakazi wa kisiwa hicho ambao shughuli yao kuu ni uvuvi, imewapeleka katika kisiwa kingine cha Kagongo na wanaendelea na shughuli zao.

 
Good morning cute

Please nifungulie pm
 
Wasifanye upendeleo ili kila muhusika anufaike
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…