SI KWELI Makomando wa Mbowe wakamatwa sakata la mauaji na Utekaji nchini

SI KWELI Makomando wa Mbowe wakamatwa sakata la mauaji na Utekaji nchini

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
JAMII CHECK_SIKWELI_3.jpg
 
Tunachokijua
Freeman Aikaeli Mbowe ni Mwenyekiti Taifa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), amewahi kuwa mbunge wa Hai na mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Desemba 1, 2024 Abdul Nondo alitekwa na watu ambao hawajafahamika katika kituo cha mabasi Magufuli jijini Dar es salaam majira ya saa 11 alfajiri alipokuwa akitokea Kigoma. Taarifa zake zilitolewa na chama chake lakini pia kupitia kwa aliyewahi kuwa kiongozi wa chama hicho Zitto Kabwe na baadaye kutoka kwa taarifa rasmi ya jeshi la polisi.

Usiku wa Desemba 1, 2024 Nondo alipatikana akiwa ametupwa katika ufukwe wa bahari ya hindi maarufu kama Coco beach (kisa kuzima Cha kutekwa na kupatikana kisome hapa)

Tangu kupatikana kwa Nondo Polisi wamesema wanaendelea na Uchunguzi Ili kubaini watu waliohusika na Tukio hilo (Soma hapa).

Leo Desemba 4, 2024 imeibuka Taarifa kwenye Mtandao wa X (Zamani Twitter) yenye nembo ya Millard Ayo ikidai Jeshi la Polisi limewakamata Makomado wa Freeman Mbowe kwa kuhusika katika kumteka Abdul Nondo, taarifa hizo zimechapishwa hapa na hapa.


Ni upi uhalisia wa Taarifa hiyo?

Ufuatiliaji wa Kimtandao uliofanywa na JamiiCheck umebaini kuwa taarifa hiyo haina ukweli na post hiyo haijawahi kuchapishwa na akaunti rasmi ya Millard Ayo kama inavyoonekana.

Uchambuzi wa Posti husika
Picha iliyotumika kutengeneza chapisho hilo imetolewa katika Taarifa ya Jeshi la Polisi iliyokuwa inaripoti kuwakamata Watu Waliojaribu kumteka mfanyabiashara Deogratius Tarimo na haielezi chochote kuhusu watu hao kuhusika na Freeman Mbowe kama ambavyo Posti hiyo inadai.
1733383419536-png.3169365

Picha ya Wahalifu iliyochapishwa kwenye Ukurasa rasmi ya Millard Ayo

Zaidi ya hayo, Taarifa maalumu ya Polisi inayoeleza kupatikana kwa Abdul Nondo kwenye fukwe za Coco Beach zinaeleza kuwa Uchunguzi wa Tukio hilo bado unaendelea (Soma hapa), mpaka leo Desemba 5, 2024 hakuna Taarifa nyingine iliyoeleza muendelezo wa tukio hilo

Uchambuzi wa JamiiCheck umebaini aina ya Mwandiko (font type) iliyotumika katika post hiyo haufanani na font anayoitimia Milard Ayo katika kuchapisha Taarifa zake nyingine.​
Back
Top Bottom