Makonda ameagiza kuhamishwa kwa Wakuu wa Idara mbalimbali za Mkoa wa Arusha ambao wamehudumu kwenye Mkoa huo kwa zaidi ya miaka mitano

Makonda ameagiza kuhamishwa kwa Wakuu wa Idara mbalimbali za Mkoa wa Arusha ambao wamehudumu kwenye Mkoa huo kwa zaidi ya miaka mitano

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda ameagiza kuhamishwa kwa Wakuu wa Idara mbalimbali za Mkoa wa Arusha ambao wamehudumu kwenye Mkoa huo kwa zaidi ya miaka mitano.

Waliohamisha kwa maelekezo ya Mkuu wa Mkoa ni pamoja na James Labikoki ambaye ni Afisa usafirishaji na taka ngumu, Theresia Maro ambaye ni Afisa TEHAMA, Mfaume Mfaume Afisa Utumishi na Dkt. Onesmo Mandike ambaye alikuwa Afisa Kilimo na Mifugo.

Mkuu wa Mkoa pia ametoa maagizo kwa Katibu tawala wa Mkoa Mussa Missaile kuwashusha vyeo Yusuph Mange aliyekuwa Afisa Elimu Sekondari na Hussein Bakari Afisa Elimu Msingi ambao wanadaiwa kushindwa kutimiza majukumu yao kikamilfu na hivyo kuathiri usimamizi wa miradi ya elimu.

Mkuu wa Mkoa amefikia hatua hiyo mara baada ya kumtaka Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Injinia Juma Hamsin kumueleza kuhusu wanaokwamisha mambo ya Halmashauri kusonga mbele ambapo katika maelezo yake alimuomba Mkuu wa Mkoa kuwahamisha Watumishi waliofanya kazi kwa zaidi ya miaka mitano kwenye kituo hicho kimoja cha kazi.
 
Jerry Slaa hakika majibu kwa anayoibua yanapatikana! Huyu mwingine mhhhhhhhh kama sioni kitu kwa kweli - hivi ni kweli wale watumishi wote watahamishwa? Mhhh ngoja tuone! - yetu macho na masikio. mwisho wake mtamuuuuuuuu!
 
Erhics za Hr,reshuffling ni afya kwa mfanyakaz.huwez kukaaa kituo kimoja miaka 10.utakuwa tu umeishiwa na innovation. Ndio mana miaka 5 unakua eligible kabisa kuhama
 
Jerry Slaa hakika majibu kwa anayoibua yanapatikana! Huyu mwingine mhhhhhhhh kama sioni kitu kwa kweli - hivi ni kweli wale watumishi wote watahamishwa? Mhhh ngoja tuone yetu macho na masikio. mwisho wake mtamuuuuuuuu!
Hata wasioohamishwa si wameshushwa vyeo na imekwisha hiyo
 
Maafisa elimu ni wateule wa katibu mkuu tamisemi, RAS ni msimamizi.

Wakuwahamusha nje ya mkoa hao wakuu wa idara ni km tamisemi.


RAS atawaroteti ndani ya mkoa na kuwalipa posho zao. Ijumaa wanakuwa pamoja jijini.
 
Ifike mahala hata hizo kazi za Serikali ziwe za contract za miaka mitatu mitatu, baada ya hapo mkataba wako unakuwa reviewed based on performance. Performance iangalie na uaminifu wa mtu, kuwe Kuna police clearance na takukuru clearance.
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda ameagiza kuhamishwa kwa Wakuu wa Idara mbalimbali za Mkoa wa Arusha ambao wamehudumu kwenye Mkoa huo kwa zaidi ya miaka mitano.
ambapo katika maelezo yake alimuomba Mkuu wa Mkoa kuwahamisha Watumishi waliofanya kazi kwa zaidi ya miaka mitano kwenye kituo hicho kimoja cha kazi.
Watumishi wanataka sana uhamisho lakini hukataliwa kwa madai ya hakuna fedha za kugharamia hamisho zao.

Nami ningekuwa Arusha ningemwambia amuru na Mimi nihamishwe nilipwe mapesa ya uhamisho..

Ila upande mwingine kuhamishwa toka Jiji la Arusha "Geneva ya East Africa" upelekwe let say Namtumbo - Lindi au Kasulu - Kigoma obviously ni kama kumtoa samaki kwenye maji na kumtupa nchi kavu au kwenye tope!!
 
Maafisa elimu ni wateule wa katibu mkuu tamisemi, RAS ni msimamizi.

Wakuwahamusha nje ya mkoa hao wakuu wa idara ni km tamisemi.


RAS atawaroteti ndani ya mkoa na kuwalipa posho zao. Ijumaa wanakuwa pamoja jijini.
Nadhani RC kafanya kazi yake.

Kama mamlaka ya kuthibitisha hayo maamuzi ni TAMISEMI kupitia kwa Katibu Mkuu wake, basi anapaswa kufanya hivyo.

Otherwise "mamlaka ya kimkoa" on the other hand ndiyo TAMISEMI yenyewe hiyo. Kwa hiyo hakuna mgogoro hapo!
 
Kitu kizuri nikuchunguza performance zao na record zao kuanzia takukuru na police, wale wenye record mbaya unastaafisha kwa manufaa ya umma na wale wasio na shida unahamisha vituo vya kazi.
 
Erhics za Hr,reshuffling ni afya kwa mfanyakaz.huwez kukaaa kituo kimoja miaka 10.utakuwa tu umeishiwa na innovation. Ndio mana miaka 5 unakua eligible kabisa kuhama
Swali je HR hawajui hilo,je Tamisemi wahusika hawana hizo records? Mbona walimu wanafundisha shule moja hadi wana staafu hapo hapo? Kwenye utendaji muajiri lazima utengeneze KPI tatizo hata huyu mkuu wa mkoa hana KPI ndio mana inakua ngumu kupima ufanisi,kufanya nyongeza, kupandisha vyeo kwakua kigezo sio ufanisi ni kua katika ajira kwa muda mrefu,ila uhalisia unaweza kua na muda mchache ukawa more productive nakuleta matokeo kuliko waliokaa muda mrefu ndio mana sector binafsi zinafanikiwa,hivyo alichofanya ni muendelezo wa sanaa
 
Matumizi mabaya ya hela za serikali, labda wajihamishe wenyewe
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda ameagiza kuhamishwa kwa Wakuu wa Idara mbalimbali za Mkoa wa Arusha ambao wamehudumu kwenye Mkoa huo kwa zaidi ya miaka mitano.

Waliohamisha kwa maelekezo ya Mkuu wa Mkoa ni pamoja na James Labikoki ambaye ni Afisa usafirishaji na taka ngumu, Theresia Maro ambaye ni Afisa TEHAMA, Mfaume Mfaume Afisa Utumishi na Dkt. Onesmo Mandike ambaye alikuwa Afisa Kilimo na Mifugo.

Mkuu wa Mkoa pia ametoa maagizo kwa Katibu tawala wa Mkoa Mussa Missaile kuwashusha vyeo Yusuph Mange aliyekuwa Afisa Elimu Sekondari na Hussein Bakari Afisa Elimu Msingi ambao wanadaiwa kushindwa kutimiza majukumu yao kikamilfu na hivyo kuathiri usimamizi wa miradi ya elimu.

Mkuu wa Mkoa amefikia hatua hiyo mara baada ya kumtaka Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Injinia Juma Hamsin kumueleza kuhusu wanaokwamisha mambo ya Halmashauri kusonga mbele ambapo katika maelezo yake alimuomba Mkuu wa Mkoa kuwahamisha Watumishi waliofanya kazi kwa zaidi ya miaka mitano kwenye kituo hicho kimoja cha kazi.
 
Ifike mahala hata hizo kazi za Serikali ziwe za contract za miaka mitatu mitatu, baada ya hapo mkataba wako unakuwa reviewed based on performance. Performance iangalie na uaminifu wa mtu, kuwe Kuna police clearance na takukuru clearance.
Nani wa ku-review na kupima hizo performance? Usinielewe vibaya, wazo lako ni zuri sana lakini nataka ujue kuwa huko juu kwa kina mama Abdul, ambako ndiko wenye huo wajibu, kumeoza kuliko huku chini. Nakuhakikishia kwa asilimia zote kuwa nchi kama viongozi wake wa juu ni waadilifu basi walio chini ni lazima watakuwa waadilifu. Huwezi kuwa na rais, mawaziri, wakuu vya vyombo vya dola etc ambao ni wezi halafu utagemee makatibu kata na tarafa wawe waadilifu.
 
Back
Top Bottom