Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,336
- 4,731
Waliohamisha kwa maelekezo ya Mkuu wa Mkoa ni pamoja na James Labikoki ambaye ni Afisa usafirishaji na taka ngumu, Theresia Maro ambaye ni Afisa TEHAMA, Mfaume Mfaume Afisa Utumishi na Dkt. Onesmo Mandike ambaye alikuwa Afisa Kilimo na Mifugo.
Mkuu wa Mkoa pia ametoa maagizo kwa Katibu tawala wa Mkoa Mussa Missaile kuwashusha vyeo Yusuph Mange aliyekuwa Afisa Elimu Sekondari na Hussein Bakari Afisa Elimu Msingi ambao wanadaiwa kushindwa kutimiza majukumu yao kikamilfu na hivyo kuathiri usimamizi wa miradi ya elimu.
Mkuu wa Mkoa amefikia hatua hiyo mara baada ya kumtaka Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Injinia Juma Hamsin kumueleza kuhusu wanaokwamisha mambo ya Halmashauri kusonga mbele ambapo katika maelezo yake alimuomba Mkuu wa Mkoa kuwahamisha Watumishi waliofanya kazi kwa zaidi ya miaka mitano kwenye kituo hicho kimoja cha kazi.