Makongoro aibuka na kudai mafisadi wako 4 ndani ya CCM

Lunyungu,

Huyu jamaa ni mjinga kupindukia yaani siamini haya aliyoyasema!

Wana tapatapa sasa hivi hamna hata mmoja mwenye usafi sasa kila mtu sasa hivi anaangalia wapi atashika ili iwe njia yake ya kuwarubini wananchi,hawajui kwamba sasa hivi tumestuki hata wenye PhD ambao tunadhani wapo makini na maslahi ya taifa kumbe wameoza woteeee
 

Ndio wabunge vijana hao ambao tunajipa moyo kuwa watabadili CCM. Mbaya zaidi wapo wengi wengine waja na angalao hawa wamesaliti mafunzo ya Mwalimu, miiko na hata fkira za utanzania. wanaokuja 2010 hawajui Fikira, Miiko wala Dira, kwao wao ni UHESHIMIWA (POWER) MBELE KWA MBELE...

omarilyas
 
wenzetu wa ukonga ndivyo mlivyomtuma mbunge wenu?
 
ila huwa anajitahidi sana kutetea mafisadi, nasikia alikuwa ktk kikao cha EL pale dodoma kupanga mikakati ya kumsafisha

H O N G E R A S A A N A
 
Kishoka umesahau kuwa Makongoro ana PHD fafa so na huo ni upeo wake ktk huo ufafa wake.
 
Wana jf, mesahau sera za CCM? nikuangalia maslai ya chama kwanza sio maslai ya taifa. wanaendelea kulindana.
 
Humu jamiiforum tuwe wa kwanza kutowapa hawa jamaa title feki. Huyu ni MR. MAKONGORO MAHANGA sio DR!! Au ndio maana wanatumia initials DK sio DR?
Kwanza bidi tuwaweke wote kwenye list halafu admin aifanye sticky pale juu ili tuwe na reference!!!
 

Hili suala si la chama, kama anajiamini anatetea maslahi ya Taifa awataje publicly. Huko ndani ya chama chao wanajua huo uozo. Kumbuka vile vikao vya Butiama Mkuu, ni upuuzi mtupu.
 
Makongoro Ni mbunge wangu wa jimbo la Ukonga, huyu bwana vikao vyake vya mikakati alikua anavifanyia pale banana, kuna bar moja maarufu inaitwa ANGELS BAR, au Tarime bar almaarufu kwa Chota, hapa ndipo alipokua anaanzishia mashambulizi na alipata msaada mkubwa wa Wakurya na wajaluo wanaoishi kipunguni.....bado mbinu zake tunazifatilia, ila naamini uchaguzi mkuu ujao atadondoka kama wapinzani wake ndani ya chama watajipanga vizuri, au kama mission ya wapinzani kuchukua majimbo yote ya Dar es salaam itaungwa mkono na umma,

Kifupi hupaswi kumshangaa Mahanga ila tushangae sisi wana Ukonga tuliemweka madarakani,


Elimu na madarasa yake aliohudhuria hayakutosha kumfuta ujinga, bado ana kiwi cha macho machoni.
 
Yeye ndo fisadi ndo maana anawatetea. Watu kama hawa hawatakiwi ktk zama hizi. Anajikomba kwa wakubwa zake mnafiki mkubwa huyu. hovyooo!
 
Huyu Makongoro naona anatafuta jina tu katika siasa za Tanzania, yeye anasema hao mafisadi mbona hawatajwi wakati yeye mwenyewe anashindwa hata kutaja hao wanne anaowasema, nafikiri sitakosea nikimuita huyu jamaa mjinga kwani naona anachoongea hapa ni pumba tu, if you get nothing to talk about just shut up and enjoy your bonuses from CCM and Bunge....huyu ni mnafiki na mzandiki mkubwa.
 

Mkuu FP, saafi sana strong analysis.

Respect.

FMEs!
 

- Duh! Papa Sam babu kubwa kumbe na wewe ni wa home saafi sana tupo pamoja, kumbe na wewe unawashitukia wale watu wakurya wa Kipunguni yaani familia ya Mahende waliofilisi ule mradi wa wananchi wa-Denmark wa vifaranga vya kuku pale kona ya Air Aviation, na kuanzisha mashirika ya malori na mabasi, sasa wanaamua nani awe mbunge na nani asiwe! Unajua hawa jamaa ndio waliompa ubunge Chale Kajege kule Mwibara, sasa tizama yaani kwa hela zetu wenyewe wananchi wa Tanzania, that is incredible!

- Mahanga alimshinda Rupia, another joker aliyeahidi kuleta maji pale jimboni kwetu lakini alipochaguliwa hakurudi tena mpaka uchaguzi ulipofikia ndio akajitokeza tena, halafu Mahanga kumbuka alikuwa na support ya Mkapa baada ya kumkarabatia nyumba yake bure pale Sea View na alikuwa kiungo muhimu sana kwa Mtandao.

Otherwise, strong analysis na keep it up unajua umegusa home kabisaa yaani County ya Segerea, inayoundwa na kata za Kinyerezi, Majumba Sita, na Sitaki shari, Kipunguni, Vidunda, na Airwing.

Respect.

FMEs!
 
yeyote anayemtetea mwizi ni mwizi pia, yeyote anayemtetea kibaka ni kibaka pia, na yeyote anayemtetea fisadi ni fisadi pia... kila mwamba ngoma, ngozi huvutia kwake na samaki mmoja akioza wote wameoza hivyo ccm wote ni mafisadi na wote wameoza maana wamewakumbatia, wanawatetea na kuwalinda mafisadi...

ingekuwa awamu ya mzee kifimbo... ile tu ukikisiwa na shombo ya ufisadi au kutotimiza wajibu ipasanyo ungekaa chonjo na kuwekwa kando... ccm ya leo au ccm ya wana mtandao hii ni ndoto za kimweli na hadithi za alinacha... ccm imekuwa sikio la kufa...
sijui ni lini manjonjo na malimbwata ya kifimbo cheza na kalingu yeye yataiamsha ccm usingizini ili ianze kuweka kando mafisadi badala ya kufungua matawi mpaka maka!
 
ingekuwa awamu ya mzee kifimbo... ile tu ukikisiwa na shombo ya ufisadi au kutotimiza wajibu ipasanyo ungekaa chonjo na kuwekwa kando... ccm ya leo au ccm ya wana mtandao hii ni ndoto za kimweli na hadithi za alinacha... ccm imekuwa sikio la kufa...

- Mkuu haya maneno mngekua mnayaacha jamani, hawa mafisadi hawakuzaliwa after 1985.

Respect.


FMEs!
 


Lawam,a ziende kwa wakurya wa Gongo la Mboto walio ikumbatia CCM .Mambo yafanyike kama Tarime
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…