Makosa na katiba mpya

Makosa na katiba mpya

mzenjiboy

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2010
Posts
907
Reaction score
385
Nadhani kabla ya kutengeneza rasimu ya kwanza na ya pili na hatimae kupatikanwa kwa katiba mpya, kwanza kabisa kulikuwa na haja ya kupiga kura ya maoni juu ya muungano kama raia wa pande mbili wanautaka au hawautaki. Endapo kungepatikana majority kura ya NDIO hapo ndio pangelifanyika mchakato wa kupata katiba mpya. Na kungepatikana kura nyingi za HAPANA hapo tena kungelikuwa na maneno mengine. Ama kuweka kura ya maoni mwisho na ikiwa walio wengi wakikataa muungano ina maana mambo yote yaliokwisha kutekelezwa itakuwa ni bure pamoja tukizingatia na gharama zake. Kwa maoni yangu kilichotendeka ni makosa lakini ndio twendeni nalo.
 
Hii nchi ilishauzwa ndugu bado kuhama tu!!!
 
......uko sahihi kabisa kiongozi: kitendo cha watu wachache kujifanya wanajua kila kitu na kudharau mawazo ya wengi ndicho kinapelekea haya yote kutokea: Tuombe Mungu tupate Katiba ambayo itaonyesha taswira yenye mujumuhisho wa mawazo ya wengi kwakweli.
 
Bhana ninyi mtapiga kelele za bure tu!
Hivi mnadhani hawakuliona hilo?
Muungano hauvunjwi hata watu wakiuana!
Chezea siasa za Afrika nyie!!!
 
Back
Top Bottom