Makubaliano ya vikao vya ukoo kisheria kwenye mirathi (Msaada please)

Miniti za kikao cha ukoo mnazo? Ambazo kila aliyehudhuria alisaini?

Kikao hicho kiliteua msimamizi wa Mirathi?
Msimamizi huyo, kama aliteuliwa, alithibitishwa na Mahakama?

Kama yote ni NDIO, Msimamizi wa mirathi aende Ofisi ya aridhi akaweke tahadhari inayoitwa CAVEAT.

Nashauri zaidi kuwa nenda kwa wakili utamueleza kwa utulivu na atakagua docs ulizo nazo kwa ajili ya hatua sahihi.

Kumbuka masuala ya kisheria huhitaji umakini kwa kila hatua.
 
Nashukuru kwa majibu yako kaka. Kwenye kikao nilikuwa mdogo sana ila ninapo wauliza walio kuwepo wanasema kulikuwa na karatasi yenye maelezo ya kikao kizima ila sasa kwenye minute kuwa kila mtu asign ndio sikumbuki.
 
Naahidi kulifuatilia hili .. maana ni muda wa 16 years umepita wale wazee wakubwa walio kuwa kwenye hicho kikao wameshafariki karibia wa4 .. sasa dah.. Itakuwaje kama hakukuwa na sign za wana ndugu? Je kwa sasa naweza kuanza vip afresh?
 
Labda kukusaidia. Utaratibu wa mirathi ni kwa kufungua mirathi mahakamani. Mahakama ndiyo inamteua msimamizi wa mirathi baada ya kikao cha familia kukaa na kupendekeza.

Pia mtu yeyote mwenye interest na mali za marehemu anaweza kuomba kuteuliwa na mahakama kuwa msimamizi wa mirathi.

Hivyo basi, kama kweli hiyo nyumba ni ya marehemu baba yenu, na kama aliipata ndani ya ndoa, basi lazima kwanza mali hiyo itengwe kiasi anachostahili kupata mjane na kinachobaki kinakuwa ni sehemu ya mali ya marehemu ambayo inastahili kurithiwa na warithi.

Hujachelewa, unaweza kuchukua hatua!
 
Poleni sana... Inasikitisha sana...

Ngoja waje kukupa muongozo...


Cc: mahondaw
 
Ni matatizo ambayo wazee wengi wamefanya na kusababisha hasara kwa familia zao.
Ila naamini sisi tuliobaki na tunaenda kuwa wazee wa kesho tumeanza kuchukua hatua za kuandika wosia. naamini watanzania wengi vijana wanaanza kuelemika na kuzingatia haja ya kuandika wosia. labda kama mtu huna mali.
 
urithi sio lazima uwe nyumba au kiwanja kitu chochote.Kuna baba yangu alifariki aliniambia mama yake alivyofariki alirithi godoro na kitanda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…