Makundi ya pro-Russia jukwaani na mitaani baada ya uvamizi huko Ukraine

Makundi ya pro-Russia jukwaani na mitaani baada ya uvamizi huko Ukraine

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Tangu uvamizi wa Russia nchi Ukraine uanze Pro-Putin/Russia naweza kuwagawanya katika makundi matano

1. Wanaozungumzia huu uvamazi wa Urusi kwa upande wa Historia ila bahati mbaya historia imewapitia kushoto au ni ile historia waliyoisikia vijiweni tu kwa watu ambao hawajakanyaga hata darasa moja la Historia. Hapo utasikia NATO ilikuwa na makubaliano na Russia isijitanue kuelekea Urusi ikayakiuka, au kuna makubaliano/mkataba wa Russia na Ukraine isijiunge NATO . Hawa wanajitahidi ila Historia waliyo nayo ni uongo na hawana ushahidi wowote wa kihistoria.

2. Wanaozungumzia huu mgogoro kwa nadharia njama "conspiracy theories". Hawa wataongolea biolabs, ushoga, Covid, monkeypox, NWO na ujinga mwingine mwingi. Hawa ni wa kupuuzwa tu.

3. Wanaozungumzia huu uvamizi kama ushabiki wa Simba na Yanga tu. Hawa utasikia wanasema Ukraine sio Zimbabwe, NATO amezidiwa kila kitu na Russia, NATO kama mwanaume aingie vitani kupigana, dunia haiwezi kuwa na mbabe mmoja tu, Chechens wamekiwasha. Hawa wengi wao nafikiri ni watoto wa 2000 na hawajui hata maana ya vita nini.

4. Wanaompenda Putin na kushangilia uvamizi wake kwa sababu eti hata US au NATO huwa anavamia nchi nyingine na kwasababu hiyo taifa lingine lenye nguvu linaweza kufanya hivyo pia. Hawa ukianza kuwachumbulia case moja moja hoja yao inayeyuka kama povu

5. Wanaoamini NATO hasa US wame stage huu mgogoro kwa maslahi yao binafsi hasa ya kuuza silaha au wengine wanasema kuimuza Russia. Hapa utawakuta baadhi ya wasomi.
 
6. Wanaoshangilia hii vita kwa kuchukua upande wa urusi au ukraine kwa kigezo cha dini

Muislamu atamshangilia Mrusi kwasababu Marekani anayemsaport ukraine amekuwa na migogoro na nchi za kiislamu

Mkristo anaisaport Ukraine kwakua Marekani kuna implication ya imani ya kikristo
 
Hawa watakuwa vilaza wa kutupwa. Mbona Marekani ni Mshirika mkubwa wa Saudi Arabia ulipozaliwa Uislamu! Pia ni mshirika wa mataifa mengi sana ya Kiislamu. Halafu mbona watu wengi wanaotoka mataifa ya Kiarabu wanakimbilia US na sio Russia?

6. Wanaoshangilia hii vita kwa kuchukua upande wa urusi au ukraine kwa kigezo cha dini

Muislamu atamshangilia Mrusi kwasababu Marekani anayemsaport ukraine amekuwa na migogoro na nchi za kiislamu

Mkristo anaisaport Ukraine kwakua Marekani kuna implication ya imani ya kikristo
 
Mimi nimeongelea upande wa uongo na ujinga, ukigeuza upande wa pili wa shillingi utaujua ukweli.
Lengo la mada hii ni kitu gani? Maana kama hao wote ni waongo au hawajui kitu. Sasa ukweli ni upi? Tulinganishe hayo uliyosem tujue anaeufahamu chanzo cha mgogoro ni nini. Otherwise hutakuwa na tofauti nao
 
Ndiyo maana unajikojoleaga kitandani kizembe ,je sisi tunao jua umuhimu wa balance ya dunia katika nguvu.

Wewe unaoshabikia nato na usa [emoji631] nisawasawa na watu mnaopinga mfumo wa vyama vingi na kutaka chama kimoja, sisi tunao shabikia urusi tunataka mgawanyo wa nguvu za kidunia wenye balance.
 
Hawa watakuwa vilaza wa kutupwa. Mbona Marekani ni Mshirika mkubwa wa Saudi Arabia ulipozaliwa Uislamu! Pia ni mshirika wa mataifa mengi sana ya Kiislamu. Halafu mbona watu wengi wanaotoka mataifa ya Kiarabu wanakimbilia US na sio Russia??
Uislamu haukuzaliwa Saudia Arabia kama umesoma biblia,,,chanzo cha huu mgogoro wa Urusi ungekijua ungekua upande wa Urusi.
 
Uvamizi wa Putin ni haramu na hauna justification yoyote.
Nendeni mkampige sasa kama mlivyofanya Iraq Libya, Vietnam na kwingineko. Msimuachie Ukraine peke yake na akimalize pale Poland is next Lithuania.
Anamega Ukraine na kuifanya Russia na hammufanyi chochote zaidi ya kubweka kwenye mitandao.
Na mkinifanya wabishi anakata gesi kipindi cha baridi ili akili iwakae sawa.
 
Acheni mvua iendelee kunyesha tuone panapovuja.

Wa afrika wenzenu kila siku wanauawa kwenye uwanja wa mapigano huko DRC, Somalia, Sudan, Ethiopia na n.k lakini mmekaa kimya tu wala hampigi kelele mkekaa kimya as if wanaokufa huku siyo watu ni nguruwe ila Ukraine na ulaya ndo watu si ndiyo?
Wa afrika wengi wamejaa unafiki sana na wengi ni bendera fuata upepo, jitu lipo tayari kukaa hapa kutwa nzima kuwatetea watu wa ulaya kuliko kulaani angalau hata kwa dakika chache tu, mauaji ya wakongo wanaokatwa vichwa kila kukicha.

Acha ulaya nao walionje joto la jua ili wajaribu kuishi maisha ambayo ndo yamekuwa maisha ya wenzao huku afrika na bara la asia kwa miaka mingi sasa.

Nachukia sana kuona Mtu mweusi kutoka Afrika anaejikuta anatetea migogoro ya ulaya nakukaa kimya kinachoendelea ndani ya bara lake na kwa majirani zake.

Shame on you poor Africans [emoji17]
 
Ungekuja na hitimisho lanini kifanywe dhidi ya RUSSIA ili kuumaliza huu mgogoro alouanzisha ungeeleweka
Mana VIKWAZO naona vimepiga U TURN vilipotokea
Naona jamaa bado wananunua mafuta kama awali tena kwa wingi na tena kwapesa ya baniani mbaya hapa wazi EU wanachangia kwazaidi ya 50% kwa PUT IN na KREMLIN kuendelea na OP yao walio ianza nabila yashaka yaenda vyema
Naona ngano bado inauzwa kama kawaida na tumeona UKRAINE ndio anateseka na NGANO yake hapa nisuala la muda tuu kabla ya EU na DUNIA haijalubaliana na masharti ya PUT IN na MOSCOW juu ya NGANO na VIKWAZO kama alivyotaka kwa NISHATI na RUBO
Hoja yako na 3 kuhusiana na NATO tunataka NATO waingilie sababu wamejipambanua kua wao ndio watetezi wa wanyonge kama walipofanya utetezi wao kwa raia wa LIBYA nawanachama wao walipofanya hayo AFGHANISTAN nawanachama wao walivyofanya hayo YUGOSLAVIA KUWAIT SYRIA nk kwanini huko walienda kusaidia ila wanaiacha UKRAINE inateketea!!?
Kiufupi umeandika maneno mengi bila ya hitimisho lakwamba kipi kifanyike dhidi ya RUSSIA ili aondoke UKRAINE mana kama vikwazo usitegemee kama RUSSIA ataacha kuichapa UKRAINE sababu ya vikwazo nandio maana hua tunawaambieni RUSSIA sio ZIMBABWE sababu kwavikwazo walivyomuekea ingekua RUSSIA kama ZIMBABWE ingekua ishasimamisha OP yake
Mwisho kabisa :-OP yaendelea vyema sana namalengo lazima yatafikiwa kama yalivyopangwa kama mnataka yasifikiwe museme RUSSIA ifanywe nini maana kwavikwazo musahau kama RUSSIA itaiacha UKRAINE ndio kwaanza wanazidi imegega kila leo ndio maana tunaitaka NATO ikaisaidie UKRAINE sababu tunahisi pengine ndio kidooogo wanaweza kumfikirisha RUSSIA kwaanacho kifanya lasivyo hizi thread zenu zakulalama hazitasaidia
NATO wakamsaidie UKRAINE acheni kuwatetea huku mkilalama lalama EU kupitia vikwazo tayar ishachemka nawewe na Pro wenzio wote mnalijua hili
RUSSIA sio ZIMBABWE

Sent using Jamii Forums mobile app
 
6. Wanaoshangilia hii vita kwa kuchukua upande wa urusi au ukraine kwa kigezo cha dini

Muislamu atamshangilia Mrusi kwasababu Marekani anayemsaport ukraine amekuwa na migogoro na nchi za kiislamu

Mkristo anaisaport Ukraine kwakua Marekani kuna implication ya imani ya kikristo
Hapa ungeandika kwa kubold na kwa herufi kubwa. Mwanzo mimi sikujua hili, ila mbeleni ndo nikajua kumbe wanaoshabikia Urusi kuna itikadi za udini ndani yake.
 
Back
Top Bottom