KERO Malalamiko kuhusu ucheleweshaji wa malipo ya faida ya uzazi (Maternity Benefits) na NSSF

KERO Malalamiko kuhusu ucheleweshaji wa malipo ya faida ya uzazi (Maternity Benefits) na NSSF

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Winnerstz

Member
Joined
Nov 25, 2023
Posts
10
Reaction score
7
Maelezo ya Malalamiko:

Naandika malalamiko haya kwa niaba ya ndugu yangu ambaye ni mwanachama wa NSSF na alifuata taratibu zote zinazohitajika ili kudai faida za uzazi (maternity benefits). Nyaraka zote muhimu ziliwasilishwa kwa wakati, ikiwa ni pamoja na cheti cha daktari na fomu za madai.

Hata hivyo, licha ya ahadi ya kulipa ndani ya kipindi cha miezi miwili, hadi sasa malipo hayo bado hayajafanyika, na hakuna mawasiliano kuhusu ucheleweshaji huu. Hali hii imeleta changamoto kubwa, hasa kwa kuwa fedha hizo zinahitajika kwa maandalizi ya haraka ya kujifungua na mahitaji ya mtoto.

Tunaomba yafuatayo:
  1. NSSF ihakikishe kuwa malipo yote ya faida za uzazi yanashughulikiwa kwa haraka ili kusaidia wanachama walioko katika hali nyeti kama wajawazito.
  2. Kuwe na uwazi na mawasiliano bora kuhusu ucheleweshaji wa malipo kwa wanachama wanaosubiri.
  3. Kuboresha mifumo ya ndani ili kuhakikisha madai yote yanashughulikiwa kwa ufanisi na kwa wakati unaofaa.
Malalamiko haya ni kwa nia ya kujenga, ili kuhakikisha kuwa wanachama wa NSSF wanahudumiwa kwa haki na ufanisi.
 
Maelezo ya Malalamiko:

Naandika malalamiko haya kwa niaba ya ndugu yangu ambaye ni mwanachama wa NSSF na alifuata taratibu zote zinazohitajika ili kudai faida za uzazi (maternity benefits). Nyaraka zote muhimu ziliwasilishwa kwa wakati, ikiwa ni pamoja na cheti cha daktari na fomu za madai.

Hata hivyo, licha ya ahadi ya kulipa ndani ya kipindi cha miezi miwili, hadi sasa malipo hayo bado hayajafanyika, na hakuna mawasiliano kuhusu ucheleweshaji huu. Hali hii imeleta changamoto kubwa, hasa kwa kuwa fedha hizo zinahitajika kwa maandalizi ya haraka ya kujifungua na mahitaji ya mtoto.

Tunaomba yafuatayo:
  1. NSSF ihakikishe kuwa malipo yote ya faida za uzazi yanashughulikiwa kwa haraka ili kusaidia wanachama walioko katika hali nyeti kama wajawazito.
  2. Kuwe na uwazi na mawasiliano bora kuhusu ucheleweshaji wa malipo kwa wanachama wanaosubiri.
  3. Kuboresha mifumo ya ndani ili kuhakikisha madai yote yanashughulikiwa kwa ufanisi na kwa wakati unaofaa.
Malalamiko haya ni kwa nia ya kujenga, ili kuhakikisha kuwa wanachama wa NSSF wanahudumiwa kwa haki na ufanisi.
hawana hela hao umbwa zote wamejipendekezea kwa masiisiiemu bila kujali kuwa wanachama na wanufaika ndio priority ya kwanza , sio wewe tu kuna watu kibaaao wanadai hiyo miofuko ya kijamii yaani utashangaa wanavyozungushwa utadhani walikuwa hawakatwi michango yao , kimsingi mifuko imegeuka ya kisiasa sana, utakuta wanadai viambatanishi ambavyo havina kichwa wala miguu wakati wanapokukata hela zako wala hawadai nyaraka yoyote ila wakati wa madai utajua hujui, any way pole kwa hilo ndio nchi yetu hiyo.
 
Hana mume au mimba za bahati mbaya

Kuna mistari nimepitia hivi unawezaje kumlipa mtu ambaye kiambata Cha mtoto hakipo bado(majina ya mtoto ,ulijifungua sangapi

Na utaratibu ni ndani ya siku 90 ,baada ya kujifungua

Sijajua huo mfuko ,unatoaje pesa mtu hajajifungua

mkewangu bwana ,akishika tu mimba ,kila mwezi lazima 150000 x9 uzazi wa kwanza nikatarajia huo ujinga najutaga mpaka Leo ....uzazi wa pili na kuendelea sijawahi hata kumuuliza mkewangu kwamba amefatilia au la
 
Back
Top Bottom