DOKEZO Malamba Mawili Msikitini hakuna maji bombani kwa miezi miwili, DAWASA ukiwapigia wanajibu tumepokea taarifa tutaiwasilisha sehemu husika inaishia hapo

DOKEZO Malamba Mawili Msikitini hakuna maji bombani kwa miezi miwili, DAWASA ukiwapigia wanajibu tumepokea taarifa tutaiwasilisha sehemu husika inaishia hapo

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Malamba Mawili Msikitini hakuna maji bombani kwa miezi miwili, DAWASA ukiwapigia wanajibu wamepokea taarifa wataiwasilisha sehemu husika inaishia hapo, ukipiga tena wanakuuliza taarifa mpya kabisa na wanasema ndio taarifa ya kupokea, ni kama ukimaliza kuongea nao hakuna chochote wanachofanya.

Kila muhudumu anaonesha kutokuwa na taarifa, ina maana huwa wanajibu tu kuonesha wamejibu baada ya hapo wanaendelea na maisha yao hawajali wala hawachukui hatua ndio maana kila mtu anajibu mara tutatuma mafundi, mara tutatuma wataalamu waje kujua tatizo, mara tunapeleka taarifa sehemu husika ifanyiwe kazi na kila mtu na jibu lake na inabidi ueleze shida upya huku akionesha kutokuwepo kwa taarifa za jambo hilo na unakuwa usharipoti zaidi ya mara moja.

Huku maji hayatoki bombani miezi miwili sasa ila wanatuma bili na kutaka zilipwe, na maji hawaleti, kifupi hawatambui kuwa maji ni huduma ya muhimu sana ambayo haikutakiwa kuletewa mzaha. Kwa nini hamleti maji? Yaani mnakaa mwezi hamjasukuma maji mnategemea watu waishije? Au kuna mbadala wa maji tuambieni basi maana mngejua hakuna mbadala msingetulia tu na hamjaleta maji miezi miwili licha ya wananchi kuwapa taarifa ya kukosa huduma.

Tanzania leo bado tunahangaika na kitu kinaitwa maji tena Dar, Aibu sana na uchungu mwingi kwetu wananchi sijui kwa nini mnatuchukulia kama hatuna umuhimu wa kupewa huduma za muhimu, tunajikuta tunaingia gharama kubwa za kununua maji Lita 1000 kwa 20000 mpaka 25000, au ununue ya kwenye madimbwi kwa lita 1000 ambayo sawa na 15000, hivi mnataka tufe kwa magonjwa kwa kutumia maji machafu?

Wizara ya Maji na DAWASA Mna mpango gani na Malamba Mawili msikitini? Au mnataka tufe kwa magonjwa ya mlipuko kwa kutumia maji machafu? Au mnafurahia tunavyonunua maji kwenye yale magari ambayo madumu hata kuoshwa sijui kama yanaoshwa? Au mnaona raha tunavyohangaika na ndoo vichwani?

Kama mnaona hamuwezi kutuletea maji semeni mmeshindwa ili tufute mawazo kuwa tuna mabomba basi maana hayana faida.

Pia soma:DOKEZO - Maji Malamba Mawili hayajatoka kwa mwezi 1 sasa, shida nini?
 
Malamba Mawili Msikitini hakuna maji bombani kwa miezi miwili, DAWASA ukiwapigia wanajibu wamepokea taarifa wataiwasilisha sehemu husika inaishia hapo, ukipiga tena wanakuuliza taarifa mpya kabisa na wanasema ndio taarifa ya kupokea, ni kama ukimaliza kuongea nao hakuna chochote wanachofanya.
Mitano tena, 4R
 
Jiongezeni mchimbe kisima..... Nunueni matank, weka mfumo wa umeme kwa ajili ya kupandishia maji kwenye matank...
 
Msijali Mama atawaletea Land Rover kutatua kero yenu, Mama ni msikivu
 
Jiongezeni mchimbe kisima..... Nunueni matank, weka mfumo wa umeme kwa ajili ya kupandishisha maji kwenye matank...
Kwa nini usiyanunue hayo matanki ukayasambaza kwa kuyagawa kwetu maana unaongea kama umekatika kichwa, hayo matanki yanagawiwa bure? Kila mtu ana uwezo wa kuyanunua? Acha majibu ya usingizini wakati uko macho
 
FaizaFoxy Malaria 2 Ritz leteni muongozo waumini wachukuaje udhu kunapokuwa hakuna maji wakati ChoiceVariable na chiembe wanapiga jaramba la visima vya PPP kwa Kafulila😁
Misikiti mingi hawategemei maji ya dawasa pekee, huws ins bisimw jwpo vya mkonk na mahodhi ya kuhifadhi maji.

Kama hakuna maji kabisa basi wanatayamam.

Uislam ni mwema sana, haujawacha kitu hanging.
 
Misikiti mingi hawategemei maji ya dawasa pekee, huws ins bisimw jwpo vya mkonk na mahodhi ya kuhifadhi maji.

Kama hakuna maji kabisa basi wanatayamam.

Uislam ni mwema sana, haujawacha kitu hanging.
Msikitini ni eneo linaitwa hivyo, siyo msikiti kama nyumba ya ibada,
 
Back
Top Bottom