KWELI Malaria inaweza kusababisha kuona mauza uza na kuota ndoto za ajabu

KWELI Malaria inaweza kusababisha kuona mauza uza na kuota ndoto za ajabu

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Hivi malaria inaweza kusababisha kuona mauza uza na kuota ndoto za ajabu?

29DFE869-00EF-49A0-AA3D-85B897F5C470.jpeg

Yaani ndoto za kutisha na kuwa na wasiwasi uliopitiliza

Pia mauza uza hasa ya kukabwa shingo, chumba kuwaka moto n.k

Nawasilisha
 
Tunachokijua
Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vya Plasmodium ambavyo husambazwa na mbu.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), mwaka 2021 pekee, zaidi ya visa vya Malaria milioni 247 viliripotiwa kutokea duniani, ambapo watu 619,000 walipoteza uhai kutokana na maambukizi hayo.

Ingawa maelezo ya mapema ya athari za kiakili za malaria yalionekana kwa mara ya kwanza katika fasihi ya kale ya matibabu ya Hippocrates na Galen, ilichukua karne nyingi baadae ambapo maelezo ya athari hizi yalifahamika zaidi.

Taarifa za kina zilienea sana baada ya Vita ya Kwanza ya Dunia (WWI), ambapo Malaria, janga la eneo la Makedonia, kati ya mwaka 1916 na 1918, ilionekana bila kutarajiwa kuwa sababu kuu ya magonjwa ya akili miongoni mwa askari waliopigana maeneo hayo.

Tangu miaka hiyo, tafiti nyingi za afya zimeelezea baadhi ya athari kama kusahau na kuchanganyikiwa kwa watu wanaopatwa na Malaria kali. Pia, maambukizi ya malaria ya muda mrefu au ya muda mfupi yametajwa kuwa na uwezo wa kusababisha mfadhaiko, wenge, wasiwasi, vurugu, fadhaa, kukosa usingizi na kuota ndoto mbaya.

Hivyo, kwa kuzingatia rejea hizi, pamoja na maelezo mengine ya kitaalamu ambayo JamiiForums imepata, imebainika kuwa ugonjwa wa Malaria unaweza kumsababishia mhusika aone mauzauza na kuota ndoto mbaya (za ajabu).
Hii kitu iliwahi kunitokea baada ya kutibiwa ikaisha
 
Nafikiri hata mitume wengi waliosema wamesikia sauti ya Mungu walikuwa na matatizo kama haya.
 
Yaani ndoto za kutisha na kuwa na wasiwasi uliopitiliza

Pia mauza uza hasa ya kukabwa shingo, chumba kuwaka moto n.k
Huyo ni 'falciperum' ambaye anatembea mpaka kwenye ubongo na kukuletea mauzauza.

Kwenye miaka ya themanini mpaka mwanzo tisini kulikuwa na outbreak kubwa ya malaria na wengine walipata kichaa kabisa, hasa wale waliochelewa kutibiwa.
 
Na typhoid pia. Hawa wanaosema walienda mbinguni wengi huwa ni mawenge ya malaria na typhoid
 
Back
Top Bottom