MALARIA ! MALARIA ! MALARIA ! @ mwezi ,for 20yrs , MUHAS-msaada, Zawadi shs 2mln.MUHAS

MALARIA ! MALARIA ! MALARIA ! @ mwezi ,for 20yrs , MUHAS-msaada, Zawadi shs 2mln.MUHAS

Risk vs Return

Senior Member
Joined
Apr 23, 2012
Posts
106
Reaction score
71
MUHIMBILI UNIVERSITY - MADAKTARI NA WATAFITI WA AFYA TUNAOMBA MSAADA WENU

Wakuu naomba msaada wa tiba ya malaria sugu tangu ujana wangu hadi leo nakaribia 50yrs nimekuwa nauguwa na kutibu malaria kila mwezi, tangu wakati wa chroloquine, fansider, Halfan,Metakhafin, Amodiaquine, mseto,,,,dawa za asili mshana, mwarobaini, soku-masai, n.k kwa yeyote atakae niwezesha kukaa angalau kila baada ya mwaka mmoja naahidi kutoa zawadi nono shs 100,000 hadi shs 2,000,000.

Hupima kuhakiki ni malaria kabla matibabu wadudu mara nyingi 3,4,5, pia namshukuru mungu sijawahi kulazwa kwa malaria, naomba msaada hata wa ushauri tu.

Nimekuwa na mawazo kuwa immunity yangu kwa malaria ni very weak, sababu sijasumbuliwa na magonjwa mengine labda kdg tonslitis kwa mwaka x2, minyoo x3 kwa mwaka, Mafua ndio mara kwa mara kila dalili za malaria tu

Swali langu je pana namna yeyote ya kuongeza immunity(kinga) ya mwili hasa dhidi ya malaria ?
 
Pole sana. Sasa hii tiba yenye donge nono hairuhusiwi. Manake tutakufanya guinea pig tukujaribishie hadi uji wa cement!

Kitu muhimu kwenye dozi huwa ni uzito wa mwili. Kama una kg zaidi ya 100, dose unayopewa inakuwa haikutoshi. Una uzito gani?
 
Unaweza kuishinda malaria kwa kufanya yafuatatyo.
1. Fanya detoxification-unaweza kufanya mwenyewe au kwa kuwaona wajuzi
2. Acha kutumia vyakula/vitu vyenye kuongeza sumu mwilini kama nyama nyekundu, bia, soda, chumvi, sukari mafuta yatokanayo na wanyama au ambayo yana cholestrol
3. anza kutumia vyakula vya asili kama viazi vitamu, viazi mviringo, ndizi, mchicha etc
4. Tumia karoti au tomato juice glass 1 mara tatu kwa siku
5. kula matunda kwa wingi-orange, pawpaw, avocado, etc
6. Badala ya sukari tumia asali
7. neti ya mbu ni muhimu usiku
8. dawa nzuri za malaria kwa sasa ni za mseto. na ikiwa wakati unaendelea na hiyo transition diet na ukaungua malaria tumia dawa mseto kwa ushauri wangu tumia :co-malafin
 
ivi si kuna jukwaa la JF DOCTOR!! huu uzi uko pahala pake kwel??? MODs vp???
 
ivi si kuna jukwaa la JF DOCTOR!! huu uzi uko pahala pake kwel??? MODs vp???

Bahati mbaya sanaa huko kwa JF DOCTORS watu hawa respond ndio maana tunajaribu hapa kwa nia nzuri tu wanafunzi wa MUHAS wachagie kupitia jukwaa la elimu, tunaomba msamaha
 
Wakuu tunawashukuru wote waliotoa michango yao ya mawazo na ushauri lakini bado tunahitaji misaada hiyo zaidi na hasa ya kitaalam, TUNAOMBA USHIRIKIANO WENU
 
Jamani mradi wa kutokomeza malaria haona tija ? umeishia wapi ? kwa wale wenzetu walioko maeneo yaliyonyunyizia dawa za huo mradi kuna mafanikio yeyote ? tunaomba taarifa tafadhali ili tuhamie huko ! ! !
 
Back
Top Bottom