Malawi Wameonyesha Njia - Je Tanzania Tutaweza?

Malawi Wameonyesha Njia - Je Tanzania Tutaweza?

Keykey

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2006
Posts
3,251
Reaction score
747
Wakati Dr. Bingu wa Mutharika alipoamua kupambana na mafisadi nchini mwake, wengi hawakuamini kama atafanikiwa. Mambo yalikuwa magumu hadi akalazimika kukiacha CHAMA kilichomweka madarakani.

Mafisadi nao wakatangaza vita dhidi ya raisi huyo na ikapita mizengwe mingi sana bungeni wakijaribu kuifanya serikali yake ishindwe kufanya kazi na wakati fulani wabunge ambao wengi wao ni mafisadi walijaribu kukwamisha miswada ya serikali ikiwemo bajeti.

Sasa katika uchaguzi huu wananchi wa Malawi wamesema kwa kauli nzito kwamba wako nyuma ya kiongozi wao katika mapambano haya kwa kumchagua kwa karibia 70%

SWALI hapa ni kama hata sisi tunaweza? JK yuko tayari kuiacha CCM tukamuunga mkono? Wadau Tujadili!



Malawi president wins re-election
_45807828_mutharikapa.jpg
images

Malawi's President Bingu wa Mutharika has won a second five-year term in office, according to the country's electoral commission. The commission said that he had won 2.7 million votes, with his nearest rival John Tembo winning 1.2 million.
Mr Tembo has alleged that there was election fraud.
The new president is due to be inaugurated on Friday, and several regional leaders are already in Malawi to attend the swearing-in ceremony.
"I declare Bingu wa Mutharika, president of the DPP (Democratic Progressive Party), winner of 2009 presidential elections," said commission head Anastacia Msosa.
The result was declared after 93% of polling stations had submitted their figures.
Mr Mutharika, a 75-year-old former World Bank official, saw his DPP taking a clear lead in parliamentary elections as well.

BBC News
 
Wakati Dr. Bingu wa Mutharika alipoamua kupambana na mafisadi nchini mwake, wengi hawakuamini kama atafanikiwa. Mambo yalikuwa magumu hadi akalazimika kukiacha CHAMA kilichomweka madarakani.

Mafisadi nao wakatangaza vita dhidi ya raisi huyo na ikapita mizengwe mingi sana bungeni wakijaribu kuifanya serikali yake ishindwe kufanya kazi na wakati fulani wabunge ambao wengi wao ni mafisadi walijaribu kukwamisha miswada ya serikali ikiwemo bajeti.

Sasa katika uchaguzi huu wananchi wa Malawi wamesema kwa kauli nzito kwamba wako nyuma ya kiongozi wao katika mapambano haya kwa kumchagua kwa karibia 70%

SWALI hapa ni kama hata sisi tunaweza? JK yuko tayari kuiacha CCM tukamuunga mkono? Wadau Tujadili!


YES-WE CAN!

Hiyo Mjomba tunaiweza- just the matter of deciding na

kuweka hasira zetu kwenye ballot box.

Ila JK mmmhhh!!, si rahisi akabadilika, coz anaogopa

kuhukumiwa na historia ya chama!

Labda akina Kingunge et al wawe wamesafiri!
 
Tuangalie mazoea yetu katika uchaguzi;

Je, watanzania wako tayari kumchagua mtu bila kupewa zawadi za kanga na fulana?

Itawezekana mtu makini kuteuliwa kugombea nafasi ya kisiasa bila kupitisha bahasha za RUSHWA kwa wajumbe wa kamati za vyama? (HILI NI WOTE SISIEMU NA WAPINZANI)

Iwapo tuliwapigia kura viongozi kwa kuhongwa vijizawadi na bakhshishi; tunawashangaa nini wanapoingia ofisini na kuanza kujilimbikizia mali?

Wakati tunapiga kelele kumkimbiza mwizi/fisadi, hakika hayuko peke yake, ana kundi kubwa la watanzania nyuma yake wanaotegemea kufanikisha maisha kwa njia za mkato. Tuliona jinsi wenzetu walivyokimbilia kupanda 'mbegu' kule DECI huku wakijua hakuna biashara yoyote inayozaa faida kiasi hicho.

TUNAHITAJI MAPINDUZI YA UTAMADUNI!
 
Hivi JK akijitoa CCM na kuanzisha chama kingine-katiba yetu inasemaje- bado atakuwa raisi??
 
Back
Top Bottom