Malengo yangu na mipango

Malengo yangu na mipango

mwanga mweusi

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2020
Posts
276
Reaction score
452
Habari?

Nipo hapa kushirikisha mipango yangu kidoogo.

Katika mipango yangu kwa mwaka huu 2023 ni mwaka wa akiba nataka niweke akiba pia akiba iwe inajizungusha bila mimi kuhusika nitafanya kazi hii ya ujenzi hadi huu mwaka uishe pesa nitakayo pata naweka akiba tu sijengi bahati nzuri sisomeshi lengo langu la mwaka huu ni 8 hadi 10 kama mmbo yataenda vibaya hata 5 nawaomba mods woote ikifika mwisho wa mwaka huu niwaonyeshe vielelezo vya akiba ya zaidi ya 7m kama nikifeli basi itakua nimeshindwa kutumia jf vizuri nitakua sina haja tena mnipige ban ya mwaka hadi nifanikishe hili asante. Hadi sasa nina 3.5m naweka mazao stoo mtaji haupotei hapo sina mpango wa kuuza nyanya mm.

Mwaka 2024 nu mwaka wa kuandaa mazingira ya familia mungu akinijalia uzima na afya na baraka zake nataka nijenge niweke akiba ya mtoto kwaajili ya shule pia niweke akiba kwaajili ya familia iweze kujitegemea na kiongozi atakua mke kwa sasa nina kiwanja pia mimi mwenyewe ni fundi nafanya kila kitu kuhusu huo ujenzi kasoro vichache sana. Nitaendelea kufanya kazii hii ya ujenzi kutimiza hayo mungu akijalia.

Mwaka 2025 ni mwaka wa kua kwenye harakati za kuachana na hizi kazi za ujenzi asikwambie mtu hizi kazi zinachokesha zinaumiza zinazeesha kujenga block inch 6 kupiga plasta mara hardcore mara kenchi yaani kwenye hii kazi hakuna siku utaenda nyumbani hujachoka na kama ukirudi hujachoka basi huna pesa kila siku unalala umechoka huo mwaka nitaachana na kazi hiii nitafanya mambo mengine naimani nikitumia jf vizuri nitafanikisha pia ndio mwaka niliokula kiapo cha chozi na uchungu hadi kung'ata meno hadi yakabonyea kwamba ndio mwaka nitarudi nyumbani na hakuna cha kunifanya niende labda matatizo makubwa yaani iwe ni ile ya lazima kabisa hata mtu akiwa hali gani lazima mtu afike ndio nitaenda kabla ya mwaka huo niliweka ahadi ya miaka 8 niliweka 10 nikapunguza hadi 8 ikadondokea 2025 sasa ni miaka 5 asanteni tuombeane uzima pia tutakuwepo hapahapa japo nakaaga madawati ya nyuma.
 
Nakuombea kila lililo jema kwako na familia yako ufike unapohitajia.

WEka na baadhi ya kazi zako tuone, isije tukawa tunamuunga mkono fundi maiko
 
Mafundi mtatuibia sana mifuko ya cement na vifaa vya ujenzi kwa ujumla,mnaturudisha sana nyuma,kweli msingi wa nyumba ya vyumba viwili ndio milioni 5 iishe kweli [emoji276][emoji276]!!,hata sikuombea sana mema
 
Mafundi mtatuibia sana mifuko ya cement na vifaa vya ujenzi kwa ujumla,mnaturudisha sana nyuma,kweli msingi wa nyumba ya vyumba viwili ndio milioni 5 iishe kweli [emoji276][emoji276]!!,hata sikuombea sana mema
Mkuu nakiri nilikua fundi wa namna hiyo ila nikajifikiria sana maana tamaa ya kitu kidogo unakosa kikubwa ndio njia wanaotumia baadhi ya mafundi ila nikaamua nipite njia sahihi pia nikazingatia UAMINIFU NI MTAJI toka nimechagua njia hii naona mafanikio hadi furaha.

Ndio inanipigisha hatua kadhaa hua sinaga tamaa hata ya msumari 1 na ndio sababu napata kazi hata mtu hatujuani zaidi ya mawasiliano na ninampa kazi yake nzuri na ukitenda uaminifu kwa bosi 1 utatambulika ni mwaminifu kwa mabosi 10 pia kwenye ubaya hivyohivyo

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Nakuombea kila lililo jema kwako na familia yako ufike unapohitajia.

WEka na baadhi ya kazi zako tuone, isije tukawa tunamuunga mkono fundi maiko
Maadhi ya majengo ya serikali View attachment 2601362View attachment 2601363View attachment 2601365View attachment 2601364View attachment 2601366View attachment 2601367View attachment 2601368
IMG_20230324_183425_911.jpg
View attachment 2601369

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom