Mali yapiga marufuku Mashirika yasiyo ya serikali yanayofadhiliwa na Ufaransa

Mali yapiga marufuku Mashirika yasiyo ya serikali yanayofadhiliwa na Ufaransa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Serikali ya kijeshi ya Mali Jumatatu ilipiga marufuku shughuli za mashirika yasiyo ya serikali yanayofadhiliwa au kuungwa mkono na Ufaransa, ikiwa ni pamoja na mashirika ya kibinadamu, huku kukiwa na mzozo unaozidi kuwa mbaya kati ya Paris na Bamako.

Waziri Mkuu wa muda wa taifa hilo la Afrika Magharibi Kanali Abdoulaye Maiga alihalalisha hatua hiyo katika taarifa yake kwenye mitandao ya kijamii, na kuitaja kuwa ni jibu kwa Ufaransa kusitisha misaada ya maendeleo kwa Mali hivi karibuni.

Wizara ya mambo ya nje ya Ufaransa ilisema wiki iliyopita ilifanya uamuzi huo, ambao ulikuja miezi mitatu baada ya kukamilisha mchakato wa kuviondoa vikosi vyake, vya kupambana na wapiganaji wa Kiislamu, kutoka nchi hiyo, juu ya madai ya Bamako ya kutumia wanamgambo wa kundi la Wagner la Russia.

Wiki iliyopita, chanzo cha wizara ya mambo ya nje kilisema Ufaransa itadumisha misaada yake ya kibinadamu pamoja na kufadhili "mashirika ya kiraia" nchini Mali.

==========

Mali junta bans activities of NGOs funded by France

Mali's junta announced on Monday a ban on the activities of NGOs funded or supported by France, including humanitarian groups, amid a worsening row between Paris and Bamako.

The West African nation's interim Prime Minister Colonel Abdoulaye Maiga justified the move in a statement on social media, calling it a response to France's recent halt to development aid for Mali.

The French foreign ministry said last week it had made the decision, which came three months after finalising its pull-out of anti-jihadist forces from the country, over Bamako's alleged use of paramilitaries from Russian group Wagner.

Bamako denies this, acknowledging only the support of Russian military "instructors".

Maiga spoke in his statement of "fanciful allegations" and "subterfuge intended to deceive and manipulate national and international public opinion for the purpose of destabilising and isolating Mali".

"As a result, the transitional government has decided to ban, with immediate effect, all activities carried out by NGOs operating in Mali with funding or material or technical support from France, including in the humanitarian field," it said.

Last week a foreign ministry source said France would maintain its humanitarian aid as well as financing for "civil society organisations" in Mali.

Source: France24
 
Uhuru ni gharama, wamefanya jambo jema la kibabe lakini litakuja na gharama ya kulipa, hawa mabeberu washafanya mifumo ifanye kazi kwa kuwategemea wao bila wao lazima tuumie kidogo.
 
Back
Top Bottom