Malikusema like food service - DSM

God knows

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2011
Posts
276
Reaction score
173
Habarini Wadau,

Nimekuwa nikitembelea mara kadhaa jiji la Mwanza kikazi na kuvutiwa mno na huduma ya chakula inayotolewa pale Malikusema, naamini wadau wengi humu waliofika mwanza wanapafahamu.

Ugali + Kuku mzima wa kienyeji aliyandaliwa kwa njia za asili kabisa + Mboga za majani na pepsi ya baridi (Optional πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€)

Natamani kuileta ile huduma hapa DSM, eneo la city center kwa ajili ya lunch, ingawa nahitaji bado mawazo na ushauri wenu wadau wa jukwaa hili.

Hiki ndicho ninachokiwaza:
- Eneo - natamani iwe city center kwa sababu target customers ni wafanyakazi na wafanyabiashara ambao muda mwingi wa mchana wanakuwepo either posta au kariakoo.
- Unlike Malikusema, vendor atakuwa mmoja tu.
- Kuku wawe pure wa kienyeji (Kuku atauzwa mzima tu, wataamua wateja kushare wawili, watatu nk.)
- Ugali utakaokuwa unapatikana ni wa dona, sembe, mhogo, wa msoma, ....... Natumaini nitasaidiwa hapa kama kuna aina nyingine.
- Mboga majani ambazo zinatakiwa ziwe zinapatikana ni kama: Chinese, mchicha, figiri.
- Kila Meal itakuja na soda kubwa ya Pepsi/Coca as mandatory service.

Additional Services:
- Sanduku la maoni, preorder services, free lunch vouchers and etc.

Sina chochote kati ya nilivyovitaja hapo juu, nina hilo wazo tu.

Nakaribisha maoni, ushauri nk. Pia kama unaweza kuwa supplier wa chochote hapo unakaribishwa pia with proposed prices.

Ila la msingi na la kuanza nalo ni eneo, then mengine yatafuata.

Naomba Mungu idea hii ifikie maturity ndani ya jukwaa hili.

My promise: I will offer free lunch to 25 JF Members on the opening date, If I am successful with it.

Karibuni.
 
Wazo lako ni zuri sana, Mungu akusaidie ulitimize
 
Vipi matunda? Malikusema nilishawahi kula dongo kuku.
 
Utamu wa msosi wa pale "Malikusema-Mwanza" unatokana na lile eneo husika hasa kwa kiwango kile cha uchafu.........naomba uzingatie hilo.
 
Utamu wa msosi wa pale "Malikusema-Mwanza" unatokana na lile eneo husika hasa kwa kiwango kile cha uchafu.........naomba uzingatie hilo.
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€

Wanaume wa Dar hawapendi uchafu.
 
Huku kwenye mikoa ya kuku og tunanunua kwa elfu 12 mtetea hadi 15 jogoo sasa Dar tena posta sijui kama bei yako ya kuku plus chakula (ugali/wali) itakuwa rafiki hasa kipindi hichi cha Ngosha
 
Upo maeneo gani kwa hapa dsm mkuu
kama hutojali tuwasiliane kwani namimi nina correspondence project so sio mbaya tukiyajenga
 
Pure kienyeji au ni X Layers? Layers walio choka kutaga
 
Upo maeneo gani kwa hapa dsm mkuu
kama hutojali tuwasiliane kwani namimi nina correspondence project so sio mbaya tukiyajenga
Sawa mkuu. Nitakurudia. Bado naangalia viability ya idea.
 
Huku kwenye mikoa ya kuku og tunanunua kwa elfu 12 mtetea hadi 15 jogoo sasa Dar tena posta sijui kama bei yako ya kuku plus chakula (ugali/wali) itakuwa rafiki hasa kipindi hichi cha Ngosha
Pure kienyeji au ni X Layers? Layers walio choka kutaga

My preference kuku wa kienyeji. Najua kupata kuku mjini ni changamoto ila naamini kama nanunua in bulk, say 100, bei inaweza kuwa chini kidogo.
 
Wazo Zuri Malikusema pako poa kuliko Chako ni Chako Dodoma.

lakini.....

Be Careful kuku wa pale ni 16000/= TZS pamoja na ugali.

Eneo la pale linamilikiwa na nani????
Baada ya hapo jifikirie kama unaweza kupataje competitive advantage kama ile.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…