Malipo ya mrahaba kwa Wasanii

platozoom

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2012
Posts
9,424
Reaction score
11,320
Nilikuwa natazama Tv ya burudani hapa Tanzania. Kuna maelezo kuwa kwa sasa wanamuziki watakuwa wanalipwa mrahaba kwa kazi zao zinazochezwa redioni.

Lakini imeelezwa kuwa kuna kampuni anayoitwa ECMA ambayo CEO wake ni Pfunk itakuwa inatruck nyimbo zinazopigwa na kushauri Basata kwa ajili ya kufuatilia malipo. Ni imeungwa mkono na Wadau kama MwanaFa na Ruge.

Wasiwasi wangu ni kwa nini kampuni binafsi ifanye kazi ya kufuatilia idadi ya rekodi zilizochezwa na si Basata wenyewe, kwa sababu Basata ni taasisi ya serikali.

Sheria inasemaje juu ya ufuatiliaji wa idadi ya kuchezwa redioni kwa nyimbo?

Nani amewapa ECMA mamlaka hayo?

Ikitokea kutokubaliana na kazi ya ECMA wanaondolewa na nani? Nani atakuwa anawafanyia monitoring?

Cc matumbo Muuza Sura Nje ya Mada chige
 
Last edited by a moderator:
Infact, hao ECMA, ni Kampuni iliyo chini ya Push Mobile, wale wale jamaa zetu wa siku nyingi, Pfunk is just this person ambaye wamehisi wakimwka as CEO ita appel vyema kwa wasanii na kwa jamii.

Ni kwamba Push mobile wana mitambo ambayo ina track redio, TV nchi nzima,Mitambo hii ndo ambayo imekuwa ikitumika na Advertsing agency pamoja na clients wao, kufuatilia namna ambavyo redio na TV zinapiga matangazo yao kwa akdri walivyokubaliana na walivyolipia.

Sasa baada ya hii ishu ya Mirahaba kuanza kunukia jamaa ndo wakaona fursa, wakijiongeza, na Kwa sababu Push as Push jina lao lina demage kidogo hasa kwa upande huo wa wasanii kutokana na figisu figisu zilizoibukaga kipindi cha mgogoro wa Ringtonse & Callertons ndo maana ikabidi ka entity kengine katakako simamia hii issue kazaliwa ndo hako ka ECMA, Nani ana uelewa, uzoefu, exposure na credibility ya kuappear kwa wadau wa bongo. Ni the man himself mwenye Bongo fleva yake Pfunk Majan. ndo wakamvuta na kumpa dili.
 
Mkuu platozoom,

Kwanza niweke kumbukumbu sawa manake kuna wengine wanadhani hili ni jambo jipya!!!! In short, sio jambo jipya!! Kiasi cha miaka takribani 3 iliyopita, wasanii walitaka kulipwa lakini kwa maajabu ya wadau; vituo vya redio vikadai wamekusanya mirabaha lakini tatizo hakukuwa na taarifa kamili za nani anastahili kulipwa kiasi gani kupitia hayo makusanyo!!!!

Biashara ndo ikaishia hapo lakini sidhani kama kuna wa kulaumiwa hapo zaidi ya COSOTA!!!

Sasa nadhani ni kutokana na huo udhaifu ndipo wanaingia watu kama akina Majani! In short, CMEA ni kampuni ya kibiashara... na kwa jinsi ninavyoiona haina tofauti sana na watu kama Push Mobile!

CMEA ni copyright management company.... kwamba wewe platozoom unafanya kazi ya muziki lakini una mashaka Clouds watakupiga changa la macho hivyo unaamua haki zako kwenye eneo husika ziwe zinasimamiwa na CMEA ambao kutokana na maelezo yao; wanadai wanavyo vifaa vyenye uwezo wa ku-truck nyimbo zinazopigwa kila siku! So, ikiwa hiyo technolojia wanayo; ina maana ule usanii kwamba pesa tumekusanya lakini hatufahamu nani anapaswa kulipwa ngapi utakuwa hauna maana tena provided radio and/or tv stations nazo zinakubaliana na ufanisi wa hiyo teknolojia!

Mwenye mamlaka ya kuipiga chini CMEA ni msanii mwenyewe! Kwa mfano, zamani linapokuja suala la caller tunes; msanii alikuwa anaingia mkataba na Push Mobile na Push Mobile ndie anaingia mkataba na kampuni za simu! Ingawaje sina uhakika, lakini ndivyo inahisi itakavyokuwa kwa CMEA... kwamba ni CMEA ndio wanaingia mkataba na radio/tv. Lakini ule utaratibu wa kwamba ni lazima msanii aingie mkataba na middleman(Push Mobile) hivi sasa umeondolewa na msanii anaweza kuingia mkataba moja kwa moja na kampuni za simu! I hope kwa CMEA ndivyo itakavyokuwa... kwamba, msanii umeingia mkataba na CMEA wasimamie hakimiliki zako lakini ukiona wanakuzingua; unawapiga chini!

Huyu CMEA ni mdau tu kwa COSOTA!!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu chige bado hilo ni tatizo. Nafikiria kwa nini tusiwe na mfumo rasmi chini ya taasisi ya Serikali utakaofuatilia records hizo. Kwa mfano sote tunajua CMEA na kampuni kama hizo zimejikita Dar es Salaam, mathalani Mwanamuziki wa Kigoma ambaye ametoa nyimbo kwa kuhangaika sana hata nauli shida, ghafla nyimbo yake inapigwa kila radio station, maana yake atapoteza mapato yake mpaka pale atakapokutana na CMEA.

Na hata hivyo kwa msanii wa aina hiyo itakuwa vigumu sana kuwafikia, pili hata haki zake pengine itakuwa vigumu kuzijua.

Tatu ni suala pia la kuwa na hakika kama atalindiwa haki zake kwenye kampuni binafsi kwa sababu ni wazi walio nyuma ya CMEA ni wadau wa Music industry ambao wanamiliki radios/Tv's.

Ndiyo maana napendekeza iwepo taasisi rasmi ya Serikali hata kama chini ya COSOTA itakayokuwa inaratibu then report zao wanaziwasilisha COSOTA kwa ajili ya madai.
 
Mkuu platozoom,

Sitarajii kwamba kufanya kazi na CMEA itakuwa ni lazima... HAPANA bali ulazima wa CMEA utaonekana na msanii mwenyewe kama anavyoona itafaa ingawaje pia hakuna kinachoshindikana! Serikali kama serikali ita-play part yake ya ku-monitor lakini CMEA nao; hususani kama atakuwa na wanamuziki bila shaka atalazimika kujiridhisha ikiwa data zinazotolewa na wadau wengine nazo ni sahii kwa mujibu wa taarifa walizonazo wao. Chukua Diamond kwa mfano; miezi kadhaa iliyopita amelipwa mrabaha wake kutoka Kenya! Hata kama yeye ndie aliyepata pesa ndefu kuliko yeyote Afrika Mashariki; nani ana uhakika ikiwa alichopata ndicho hasa alistahili kupata? Idea ya uwepo wa CMEA ndo ipo hapo na ndio maana mwisho wanaiita "East Africa" ili waweze ku-monitor kote kote!!!

Kwa upande mwingine, kama nilivyosema hapo awali, CMEA ni Copyright Management Company..! Sasa suala la copyright haliishii kwenye muziki kupigwa tv na radio peke yake bali ni zaidi ya hapo! Kwa mfano, mpango ulikuwepo (au bado upo) wa kuzitaka hata kumbi za starehee, baa n.k nao kulipa mrabaha! Sasa ikiwa msanii atajiona kuna baadhi ya haki zinazotokana na kazi zake hataweza kuzifuatilia; hapo ndipo anaweza kuamua kuwa signed na CMEA!

Kiukweli, haya mambo mengine yanakera sana lakini kwa bahati mbaya mfumo wenyewe ndo upo hivyo kila utakaoenda! Labda kwa wasanii wakubwa kama akina Diamond ambao wanaweza kuingia popote lakini sidhani hata kama hizo radio na tv station
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…