Malisa GJ: Umuhimu wa Katiba Mpya

Malisa GJ: Umuhimu wa Katiba Mpya

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
Muda wangu wa kuchangia nimeutumia kujibu maswali matano yanayoulizwa na wengi huko mtaani kuhusu Katiba (5 common questions).

1. Kwanini mchakato huu umeandaliwa na BAVICHA? Mnapigania Katiba ya nchi au ya Chadema?

#Jibu: Mchakato wowote wa katiba ni wa kisheria na kisiasa. Katiba ni jambo linalogusa watu wote, hivyo kila kundi lina haki ya kujadili. Vijana wa chama cha zamani, badala ya kuwaonea gere BAVICHA, nanyi mnaweza kuandaa kongamano lenu. Muhimu kila mtu apate nafasi ya kuamua muastakabali wa taifa letu.

2. Katiba mpya sio kipaumbele cha Rais, kwanini msiachane nayo?

#Jibu: Katiba sio mali ya Rais ni mali ya wananchi. Hivyo kama wananchi wanataka katiba mpya, Rais hawezi kuzuia kwa namna yoyote. Kama wananchi wakisema Katiba mpya ni kipaumbele chao, Rais atake asitake atalazimishwa (kwa sauti ya kimbunga Jobo).

3. Je, Katiba mpya ina umuhimu wowote?

#Jibu: Ndio. Itatuwezesha kupata tume huru ya uchaguzi, ambayo mchezaji wa timu pinzani hataweza kujigeuza refa kama ilivyo sasa. Itaimarisha uchumi kwa sababu wawekezaji wote wakubwa duniani hupenda kuinvest mitaji yao mahali penye stability ya kisiasa. Pamoja na faida nyingine nyingi (ambazo zimetajwa na wazungunzaji wengine) katiba mpya itamfunga "breki" Rais asiteue majambazi kama Sabaya na kuwapa ofisi za umma.

4. Kwanini tusifanye marekebisho kidogo ya Katiba iliyopo badala ya kudai mpya?

#Jibu: Katiba iliyopo imeshafanyiwa marekebisho mengi sana. Kati ya mwaka 1980 hadi 1995 ikifanyiwa marekebisho mara 13. Kama ni nguo basi imechakaa na ina viraka vingi sana. Kwahiyo badala ya kutafuta mahali pengine pa kuweka kiraka, ni bora tununue nguo mpya.

5. Kwanini Mchakato wa Katiba usisubiri kwanza ili tujenge uchumi kama alivyosema mama Samia?

#Jibu: Wakati akiongea na waandishi wa habari, Mama Samia alisema kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, uchumi wa nchi uliporomoka kutoka 7.2% hadi 4.8%. Kumbuka kipindi hicho mchakato wa katiba ulikua umesimamishwa. Kama kuzuia Katiba mpya kunasaidia kujenga uchumi, basi ilitakiwa kipindi cha mwendazake uchumi uimarike kuliko wakati mwingine wowote, lakini haikua hivyo.

AA4DC34A-7756-461E-9EB9-3D0B71F10764.jpeg
 
Kabla uongo wake wa list feki ya Lissu kulipwa mafao yake na bunge haujakauka vizuri leo malisa ameamua kuhara uongo mwingine!

Haya ngoja tuone mauzo ya cocaine yatqkavyokuwa mitaani baada ya punda kuachiwa huru na mahakama.
 
Naunga mkono 1000% uwepo wa katiba mpya utaondoa haya makandokando. hakuna kitu kinaboa kama muungano wa TANGANYIKA na ZANZIBAR usanii mwingi ulifanyika kwenye kutengeneza hii kitu MUUNGANO sasa jamii imeamka na inaanza kudai katiba kwa njia swahihi. Kwa kesi hii tutaangukia tu lazima kwenye katiba ya JMT na kitaeleweka.

 
Akili za UVCCM hizi. Umoja wote ule hakuna mwenye akili ya kusimama na Malisa..Hakuna.. maelezo yako haya ni mfano halisi..
Chama chetu kimechoka kweli kweli.
Kabla uongo wake wa list feki ya Lissu kulipwa mafao yake na bunge haujakauka vizuri leo malisa ameamua kuhara uongo mwingine!

Haya ngoja tuone mauzo ya cocaine yatqkavyokuwa mitaani baada ya punda kuachiwa huru na mahakama.
 
Ninayo maswal machache,

1) Hitajia la katiba mpya nilakisiasa, au la kijamii? Ukijibu njoo na majibu vivid

2) Kwanini katiba mpya uwe Sasa? Kwa Nini haikuwa miaka5 iliyopita? Nini kimepelekea kuidai sasa?

3) Eleza hoja yenye mashiko katiba mpya itasaidiaje kuleta maendeleo ya Tanzania na watanzania? Eleza japo kwa mifano hai ni nchi zipi kwa kuwa na katiba(nzuri) zinamaendeleo kwa sababu ya katiba?

4) Unakubali au kukanusha juu ya ukwel kuwa katiba iliyopo inapangufu katika tume ya uchaguzi na si katiba yote? Ukanushaji au ukubali uwe na majib yaliyo na vielelezo hai.

5) Tuambie kwa faida au kwa hasara Nini kitatokea kama tusipokuwa na katiba nyingine kwa miaka 10 ijayo? Mwananchi alieko kule nyakahoze au mugumu Serengeti au kule songwe kijijini ataathirika vipi?

Nasubri majibu

Mr bonny
 
Kabla uongo wake wa list feki ya Lissu kulipwa mafao yake na bunge haujakauka vizuri leo malisa ameamua kuhara uongo mwingine!

Haya ngoja tuone mauzo ya cocaine yatqkavyokuwa mitaani baada ya punda kuachiwa huru na mahakama.
Hii id inaonekana umejiunga hapa jukwaani siku 3 baada ya kifo cha dhalimu kutangazwa. Hizi ni baadhi ya id zilizojiunga humu jukwaani wakati wa msiba ili kumtetea yule kiongozi muovu. Na sasa naona zinaendelea na siasa majitaka humu jukwaani.
 
Ninayo maswal machache..

1)hitajia la katiba mpya nilakisiasa, au la kijamii?? Ukijib njoo na majib vivid

2)kwa nini katiba mpya uwe Sasa?? Kwa Nini haikuwa miaka5 iliyopita?? Nini kimepelekea kuidai sasa??

3)eleza hoja yenye mashiko katiba mpya itasaidiaje kuleta maendeleo ya Tanzania na watanzania?? Eleza japo kwa mifano hai ni nchi zipi kwa kuwa na katiba(nzuri) zinamaendeleo kwa sababu ya katiba??

4) unakubali au kukanusha juu ya ukwel kuwa katiba iliyopo inapangufu katika tume ya uchaguzi na si katiba yote? Ukanushaji au ukubali uwe na majib yaliyo na vielelezo hai..

5) tuambie kwa faida au kwa hasara Nini kitatokea Kama tusipokuwa na katiba nyingine kwa miaka 10 ijayo?? Mwananchi alieko kule nyakahoze au mugumu Serengeti au kule songwe kijijini ataathirika vipi??

Nasubri majib

Mr bonny
  1. Katiba mpya ni takwa la kijamii, na linapata msukumo mkubwa na wanasiasa kwani katiba ni mchakato wa kisiasa.
  2. Katiba imeanza kudaiwa toka 1992 mfumo wa vyama vingi uliporejea hapa nchini. Huenda wakati huo hukuwa umezaliwa. 2010-2015 kulifanyika msukumo mkubwa wa kupata katiba mpya, hatimaye ilitungwa sheria ya mabadiliko ya katiba mpya, na tume ya Jaji Warioba ilizunguka nchi nzima, kukusanya maoni ya wananchi. Hatimaye kukawa na katiba pendekezwa ambayo ilikuwa inasubiri kupigiwa kura japo rasimu ya Warioba ilichezewa. Miaka mitano iliyopita nchi hii ilikuwa mikononi mwa rais muovu, aliyekuwa hataki katiba ya kumzuia kwenye uovu wake. Ila kwenye ilani ya ccm mchakato wa katiba pendekezwa ulikuwepo,lakini rais mwenye kiburi cha madaraka aliigomea. Tunashukuru Mungu kwa kutuondolea yule mtu muovu bila damu kumwagika.
  3. Katiba mpya italeta maendeleo maana itatoa viongozi wenye uhalali wa umma, na wataweza kuwajibishwa iwapo watakosea. nchi za Kenya, Afrika kusini na Ghana ni mifano halisi wa nchi zenye katiba bora, na zinaaminika hata na wawekezaji, kwani zinajali utawala wa sheria, na sio utashi wa rais aliye madarakani.
  4. Tume ya uchaguzi ni sehemu tu ya mapungufu ya hiyo katiba, lakini kuna madaraka makubwa ya urais ambayo yanatumika vibaya, na kwa maslahi binafsi ya rais na genge lake. Udhaifu huo umedhibitika wazi wakati wa JK, na rais muovu aliyefariki hivi karibuni.
  5. Bila utawala wa sheria ni ngumu muwekazaji makini kuwekeza, mfano hali ni wakati wa Magufuli wawekezaji wengi waliondoka. Kama hakuna wawekezaji ni ngumu uchumi kukua. Pia ni rahisi nchi kuingia machafuko ni, kwani hakuna haki. Kama katiba mpya haisaidii mtu wa kijijini, hayo maVX ya serikalini yanawasaidia nini hao wananchi?
 
Kabla uongo wake wa list feki ya Lissu kulipwa mafao yake na bunge haujakauka vizuri leo malisa ameamua kuhara uongo mwingine!

Haya ngoja tuone mauzo ya cocaine yatqkavyokuwa mitaani baada ya punda kuachiwa huru na mahakama.
bado hujaacha kuinamishwa
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Maswali ya kitoto majibu ya kitoto

Wacha tujenge uchumi kwanza
 
  1. Katiba mpya ni takwa la kijamii, na linapata msukumo mkubwa na wanasiasa kwani katiba ni mchakato wa kisiasa.
  2. Katiba imeanza kudaiwa toka 1992 mfumo wa vyama vingi uliporejea hapa nchini. Huenda wakati huo hukuwa umezaliwa. 2010-2015 kulifanyika msukumo mkubwa wa kupata katiba mpya, hatimaye ilitungwa sheria ya mabadiliko ya katiba mpya, na tume ya Jaji Warioba ilizunguka nchi nzima, kukusanya maoni ya wananchi. Hatimaye kukawa na katiba pendekezwa ambayo ilikuwa inasubiri kupigiwa kura japo rasimu ya Warioba ilichezewa. Miaka mitano iliyopita nchi hii ilikuwa mikononi mwa rais muovu, aliyekuwa hataki katiba ya kumzuia kwenye uovu wake. Ila kwenye ilani ya ccm mchakato wa katiba pendekezwa ulikuwepo,lakini rais mwenye kiburi cha madaraka aliigomea. Tunashukuru Mungu kwa kutuondolea yule mtu muovu bila damu kumwagika.
  3. Katiba mpya italeta maendeleo maana itatoa viongozi wenye uhalali wa umma, na wataweza kuwajibishwa iwapo watakosea. nchi za Kenya, Afrika kusini na Ghana ni mifano halisi wa nchi zenye katiba bora, na zinaaminika hata na wawekezaji, kwani zinajali utawala wa sheria, na sio utashi wa rais aliye madarakani.
  4. Tume ya uchaguzi ni sehemu tu ya mapungufu ya hiyo katiba, lakini kuna madaraka makubwa ya urais ambayo yanatumika vibaya, na kwa maslahi binafsi ya rais na genge lake. Udhaifu huo umedhibitika wazi wakati wa JK, na rais muovu aliyefariki hivi karibuni.
  5. Bila utawala wa sheria ni ngumu muwekazaji makini kuwekeza, mfano hali ni wakati wa Magufuli wawekezaji wengi waliondoka. Kama hakuna wawekezaji ni ngumu uchumi kukua. Pia ni rahisi nchi kuingia machafuko ni, kwani hakuna haki. Kama katiba mpya haisaidii mtu wa kijijini, hayo maVX ya serikalini yanawasaidia nini hao wananchi?
Mkuu umejibu kwa hisia za kisiasa au kwa matink?? Kwa hyo Sasa hv tunaviongoz wabovu??
 
  1. Katiba mpya ni takwa la kijamii, na linapata msukumo mkubwa na wanasiasa kwani katiba ni mchakato wa kisiasa.
  2. Katiba imeanza kudaiwa toka 1992 mfumo wa vyama vingi uliporejea hapa nchini. Huenda wakati huo hukuwa umezaliwa. 2010-2015 kulifanyika msukumo mkubwa wa kupata katiba mpya, hatimaye ilitungwa sheria ya mabadiliko ya katiba mpya, na tume ya Jaji Warioba ilizunguka nchi nzima, kukusanya maoni ya wananchi. Hatimaye kukawa na katiba pendekezwa ambayo ilikuwa inasubiri kupigiwa kura japo rasimu ya Warioba ilichezewa. Miaka mitano iliyopita nchi hii ilikuwa mikononi mwa rais muovu, aliyekuwa hataki katiba ya kumzuia kwenye uovu wake. Ila kwenye ilani ya ccm mchakato wa katiba pendekezwa ulikuwepo,lakini rais mwenye kiburi cha madaraka aliigomea. Tunashukuru Mungu kwa kutuondolea yule mtu muovu bila damu kumwagika.
  3. Katiba mpya italeta maendeleo maana itatoa viongozi wenye uhalali wa umma, na wataweza kuwajibishwa iwapo watakosea. nchi za Kenya, Afrika kusini na Ghana ni mifano halisi wa nchi zenye katiba bora, na zinaaminika hata na wawekezaji, kwani zinajali utawala wa sheria, na sio utashi wa rais aliye madarakani.
  4. Tume ya uchaguzi ni sehemu tu ya mapungufu ya hiyo katiba, lakini kuna madaraka makubwa ya urais ambayo yanatumika vibaya, na kwa maslahi binafsi ya rais na genge lake. Udhaifu huo umedhibitika wazi wakati wa JK, na rais muovu aliyefariki hivi karibuni.
  5. Bila utawala wa sheria ni ngumu muwekazaji makini kuwekeza, mfano hali ni wakati wa Magufuli wawekezaji wengi waliondoka. Kama hakuna wawekezaji ni ngumu uchumi kukua. Pia ni rahisi nchi kuingia machafuko ni, kwani hakuna haki. Kama katiba mpya haisaidii mtu wa kijijini, hayo maVX ya serikalini yanawasaidia nini hao wananchi?
Itoshe tu kusema majib yako hayajani enea... Hayana uhalisia na mifano halisi ila yanahisia za kisiasa na mitazamo bila kuwa na utafiti was matokeo ya kizaz hiki na kijacho...
 
Ninayo maswal machache,

1) Hitajia la katiba mpya nilakisiasa, au la kijamii? Ukijibu njoo na majibu vivid

#Muuliza maswali kwanza naomba utambue kwamba siasa na jamii ni pande mbili za sarafu hivyo ni vitu ambavyo huwezi kuvitenganisha. Kwa mantiki hiyo siasa ni sehemu ya maisha ya mwanajamii.

# kwa muktadha huo hapo juu Katiba mpya siyo jambo la kisiasa ni la kijamii kwa sababu sababu tukiwa na katiba nzuri hakika tutapata viongozi ambao wapo makini sana. Pia itasaidia kupunguza matumizi mabaya ya mali za umma( jamii) mfano mzuri ni Rais mstaafu wa SA ambaye amehukumiwa hivi karibuni kwa matumizi mabaya ya mali za umma.

2) Kwanini katiba mpya uwe Sasa? Kwa Nini haikuwa miaka5 iliyopita? Nini kimepelekea kuidai sasa?

# Huu ndiyo muda mwafaka kwani jamii imeaza kuelewa kiundani kwamba siasa ni maisha na sehemu muhimu sana katika maisha ya mwanadamu. Hivyo tukiwa na katiba nzuri hakika jamii nayo itapata haki zake za msingi(Fundamental rights). Mfano katika katiba mpya tutahitaji kwamba suala la kuwa na maji safi, afya, n.k viwekwe kama ni haki za msingi ambapo serikali inatakiwa kuhakikisha watu wote awe kijijini au mjini wanavyo.

3) Eleza hoja yenye mashiko katiba mpya itasaidiaje kuleta maendeleo ya Tanzania na watanzania? Eleza japo kwa mifano hai ni nchi zipi kwa kuwa na katiba(nzuri) zinamaendeleo kwa sababu ya katiba?

# Katiba itakuwa ni chachu katika maendeleo ya wananchi kwa sababu tukiweka mambo kama jambo la afya, kuwa na maji safi ni haki za msingi hakika serikali itahakikisha wananchi wote wanakuwa na maji safi, patakuwepo na vituo vya afya nchini nzima pasipo kubagua eneo ulilopo yaani mjini au kijijini.

# kadhalika katiba itaondoa kinga kwa viongozi ambao siyo waaminifu na ambao wanatumia maharaka yao vibaya na mali za umma mfano Katiba ya Ghana, Kenya & SA haina kinga dhidi ya viongozi wanaotumia madaraka yao vibaya. Juzi tu tumeona huko SA Rais amehukumiwa kwenda jela miezi 15. Kwa huku Tanzania hicho kitu hakipo maana yake tunakumbatia uozo wa viongozi wenye nia mbaya na nchi yetu.

# Pia tutapendekeza pawepo na Ibara ambayo itaruhusu wananchi kumuadibisha Mbunge pale anapoenda kinyume na matakwa ya waliomchagua.

#Kadhalika, katiba mpya itaelezea kinagaubaga katika mchakato wa kuwapata viongozi wa umma, tutakuwa na tume huru ya uchaguzi isiyofungamana na chama chochote cha kisiasa.

4) Unakubali au kukanusha juu ya ukwel kuwa katiba iliyopo inapangufu katika tume ya uchaguzi na si katiba yote? Ukanushaji au ukubali uwe na majib yaliyo na vielelezo hai.

# Katiba yetu yote ina mapungufu makubwa sana kwa sababu zifuatazo:-

a) Kwanza ni katiba iliyotungwa wakati nchi ikiwa katika chama kimoja.

b) Pili, katiba hii imepitwa na wakati kwa sababu katiba inasema Tanzania ni nchi ya ujamaa wakati hatupo katika ujamaa.

c) Katiba iliyopo haitoi muongozo pale ambapo Rais aliyepo madarakani akipatwa na umauti ni nini kifanyike kuhusu baraza lake la mawaziri. Livunjwe au lisivunjwe. Hapa katiba ipo kimya. Kwa mantiki hiyo hili ni tatizo.

d) Katiba iliyopo inazuia kufungua kesi dhidi ya matoke ya uchaguzi wa Rais wakati nchini Kenya huwa wanapinga matokeo ya Rais. Nafikiri hivi karibuni uliona kilichotokea nchini Kenya mpaka uchaguzi ukarudiwa.


5) Tuambie kwa faida au kwa hasara Nini kitatokea kama tusipokuwa na katiba nyingine kwa miaka 10 ijayo? Mwananchi alieko kule nyakahoze au mugumu Serengeti au kule songwe kijijini ataathirika vipi?

# Tusipopata katiba mpya maana yake wananchi waliopo vijijini watashindwa kuwa na mahitaji muhimu katika jamii mfano vituo vya afya, maji safi, n.k vitu ambavyo tungependekeza viwe ni haki za msingi kama ilivyo haki ya kuishi hivyo kumnyima mwananchi au mwanajamii maji safi, vituo vya afya ni kinyume na sheria.

# Pia tusipokuwa na katiba mpya kwani tutazidi kuwa na viongozi wenye choyo ambao wanathamini matumbo yao na siyo maendeleo ya jamii kwa ujumla na wenye viburi ambao wanajua hawawezi kuadibishwa na jamii.

# Pia tutazidi kuwa na viongozi wenye dhuluma na wenye kuumiza wananchi mfano Sabaya ambaye aliteuoliwa na mwendazake bila kutambua kama Sabaya ana caliber ya uongozi. Hakika umeshuhudia wananchi walivyoumizwa katika kuporwa mali zao na mateso.


Nasubri majibu

Mr bonny
 
Mkuu walao kiduchu umejib... Tatzo kubwa tu lipo kwenye maelezo na mifano.. hzo nchi zote ulizozitaja ukiwemo na Ghana... Maendeleo yal hayatokani na katiba.. ila inatokana na historia ya eneo...

Mfano...mapungufu yaliyopo yanaweza yasiwe takwa la kijamii ila la kisiasa.. ni mhim ukatambua kuwa jamii yote ya kinzania inaustarab wake.. kwa hyo haiwez ikawa ni sawa na wanasiasa...

Wanasiasa huwa wananuni ya kuongea one agenst 2... Wanachosema sicho wanachokitenda...
 
Itoshe tu kusema majib yako hayajani enea... Hayana uhalisia na mifano halisi ila yanahisia za kisiasa na mitazamo bila kuwa na utafiti was matokeo ya kizaz hiki na kijacho...

Yaani majibu ndio hayo, kizazi kipi unaongelea ww kwa katiba hii ya enzi za ujamaa, na kumgeuza rais Mungu mtu?
 
Mkuu walao kiduchu umejib... Tatzo kubwa tu lipo kwenye maelezo na mifano.. hzo nchi zote ulizozitaja ukiwemo na Ghana... Maendeleo yal hayatokani na katiba.. ila inatokana na historia ya eneo...

Mfano...mapungufu yaliyopo yanaweza yasiwe takwa la kijamii ila la kisiasa.. ni mhim ukatambua kuwa jamii yote ya kinzania inaustarab wake.. kwa hyo haiwez ikawa ni sawa na wanasiasa...

Wanasiasa huwa wananuni ya kuongea one agenst 2... Wanachosema sicho wanachokitenda...
Ndiyo maana tunapendekeza kwamba katiba itupe mamlaka sisi wananchi ya kuwaadibisha wanasiasa(Wabunge) ambao hawatendi wanachokiongea.
 
Back
Top Bottom